Rais Magufuli ameamua nchi ifungue sura mpya ya kimaendeleo kuelekea 2025


Kijana anajtutumua ili wajue kuwa naye "yupo" huenda jicho likammulika
 
Na mbaya zaidi nusu ya bajeti inatumika kulipa madeni rais anasema tunajenga kwa pesa zetu wenyewe
 

Umekosea katika mambo mawili:
1. Uzi huu ungeufungua kabla mwenyekiti wako hajaamua kununua watu (kutoka upinzani).
2. Umesahau kuweka namba ya simu

Haya mawili yangekurahisishia kupata japo u DAS. Hata hivyo, jitahidi ku-post nyuzi nyingine kama hii angalau mara tatu kwa wiki unaweza kuonekana.
 
Mmeshaanza kampeni ,mnataka kufungua sura mpya ya maendeleo ? Maendeleo yapi au ya utekaji na uuaji?
 
Angalau watu wenye kumbukumbu mpo mnatusaidia
 
Nimeshindwa nijibu nini yeye ni msimamizi wa matumizi wa kodi zetu kwa kuna Rais yoyote duniani anaendesha nchi kwa pesa yake ya mfukoni???

Hayo matusi sio utamaduni wetu watanzania badirika ndugu yangu jenga hoja
 
Nimeshindwa nijibu nini yeye ni msimamizi wa matumizi wa kodi zetu kwa kuna Rais yoyote duniani anaendesha nchi kwa pesa yake ya mfukoni???

Hayo matusi sio utamaduni wetu watanzania badirika ndugu yangu jenga hoja

Kuhusu Matusi mbona sijakusikia ukimkosoa Mwenyekiti wa chama chako kwa kuwaita baadhi ya mawaziri wake "wapumbavu"
Au katibu mkuu wa chama chako alipowaita watu "wapumbavu waa mwaka"?
 
Anajenga misingi ya kuhudumia Uchumi ili uzalishe...maendeleo ni mchakato mishahara ashasema Rais wetu ataongeza ameanza na haya niliyotaja baadhi yake
 
Haa haa Haaa Haaa hao wanaomchukia Rais wetu John pombe Magufuli ndio hao wanaangukia kundi nililolitaja mwisho wa post yangu haiwezekani ukamchukia Bure
Tyr ameongeza sababu za kuchukiwa huyo jiwe,mengine ni propaganda tu maana kila siku mnatuorodheshea hayo hayo mtafikiri ni mapya,ni sawa umtongoze mwanamke kila siku una mwambia maneno Yale Yale.
 
Mwambie Comrade
Duh naona umeathirika sana as policies za JPM vumilia sindano imeingia hadi kwenye mfupa huyo unaye muita mshamba ndo kakufanya wewe mtoto wa mjini kulialia na mambo mpaka 2025
 
Comrade umegusia masuala mengi lkn muhimu kujua Rais aliyeko madarakani amepokea kijiti kutoka kwa mtangulizi wake ipo miradi iliyokuwa kwenye hatua ya upembuzi yakinifu kwenda utekelezwaji wake katika Awamu ya Tano ya Rais wetu John pombe Magufuli..

Pili miradi mikubwa ya SGR na wa Umeme MTO Rufiji ni maamuzi Magumu ya Rais wetu John pombe Magufuli dunia inajua kutumia malighafi za chuma ya linganga na mchuchuma zipo sababu za msingi zilizopelekea hilo kushindikana jua hivyo.

Kila ukienda wilaya yoyote hapa nchini kuna mradi mkubwa unaendelea unatoa wapi ujasiri wa kutoona juhudi za Rais wetu katika mapinduzi ya maendeleo nchini

Umeme wa Rea miradi mipya ya maji next time nitakuja na detail za mradi umesainiwa lini na unakamilika lini

Wajasiriamali wamepunguziwa kodi za kero kwa kupewa vitamburisho vya ujasiriamali

Demokrasia ya aina gani unataka ya wanasiasa kufanya mikutano jangwani au Wamachinga kufanya biashara zao popote bila bugudha ya polisi Uhuru wa kufanya kazi au Uhuru wa kutukana Uhuru wa aina gani unataka kila bajeti zinarekebishwa sheria za kodi ili kuchochea sekta binafsi kuwekeza nchini

Mfano bajeti yetu ya 2019/20 kodi 54 zimefutwa kwa lengo la kuchochea sekta binafsi kuwekeza nchini na kuzalisha zaidi Mhe Rais wetu John pombe Magufuli kakutana na wafanyabiasha 5 kutoka kila wilaya lengo kusika kero zao na akachukua hatua palepale

Mnataka nini afanye mbona nia na utashi wake kwa Taifa letu upo wazi Rais wetu John pombe Magufuli kuiona Tanzania inasonga Mbele Kimaendeleo
 
Haaa Haaa Haaa tupo kwenye kilimo tumejiajili na Umri huo bado hatujafika usituzeeshe hivyo samahani
 
[emoji445] ccm ni ile ileeee[emoji448][emoji448][emoji397] oooh ni ile ile[emoji446][emoji441][emoji449][emoji345][emoji981][emoji981][emoji350][emoji351][emoji351][emoji442]. Imba sana maana ndiyo njia yako pekee inayokuletea mkate hapo nyumbani.
Ndio ileee ileee siku hizi tuna na Kwangwaru Magufuli Remix kwangwaruuuuu
 
Mikopo hiyo ipo kwa mujibu wa sheria na utaratibu wa utolewaji wake umewekwa kwenye sheria hivyo kama sheria hiyo ina mapungufu ndio ya kufanyia marekebisho
 
Hilo lishafanyiwa kazi mwakani hamna kitu cha hivyo
Wakulima hatuna soko labuhakika la mazao yetu. Mbaazi ziliozea shambani msimu uliopita . Mustakabali wa korosho mpaka sasa ni kitendawili.

Hizi barabara si za kumkomboa mkulima kutoa mazao kijijini kupeleka tu makao makuu ya wilaya.
 
Maendeleo ya vitu yana uhusiano na maendeleo ya watu kwa sababu watu hao ndio wahitaji wa vitu katika maisha yao ya kila siku
 
Haaa Haaa Haaa tupo kwenye kilimo tumejiajili na Umri huo bado hatujafika usituzeeshe hivyo samahani

Kilimo gani unalima ww. Sana hulimi bali ni mkuna ardhi unayelinda mashamba ya urithi yasichungiwe mifugo. Huna 40 kisa umefoji cheti?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…