Tetesi: Rais Magufuli anatamani nchi yetu iwe na Katiba ya nchi mbovu zaidi ya hii tuliyo nayo sasa!

Tetesi: Rais Magufuli anatamani nchi yetu iwe na Katiba ya nchi mbovu zaidi ya hii tuliyo nayo sasa!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Wananchi wengi wa nchi hii wanatamani nchi yetu iwe na Katiba mpya ambayo itaendana na nyakati hizi, tofauti na Katiba tuliyo nayo hivi sasa ambayo ilitungwa mwaka 1977, ambayo wananchi wengi wanaiona kuwa haikidhi matakwa ya sasa ya kisiasa na kijamii

Wakati wananchi wengi wanatamani nchi yetu iwe na Katiba mpya, iliyoboreshwa na itayompunguzia madaraka makubwa mno aliyopewa Rais, hali ni tofauti kwa Rais wa nchi, ambaye anatamani nchi yetu iwe na Katiba mpya, ambayo itazidi kuminya zaidi haki za binadamu na itazidi kumuongezea madaraka

Uthibitisho wa hilo ni kauli aliyoitoa hivi karibuni Rais Magufuli kuwa anashangaa yeye apewe mamlaka kikatiba ya kuteua, lakini anyimwe uwezo wa kutengua!

Maneno hayo aliyoyatamka hadharani hivi karibuni wakati akiwahutubia wananchi

Huo ni ujumbe mzito sana, kuwa Rais huyu, haafikiani na baadhi ya ibara za Katiba hii iliyopo hivi sasa za yeye kupewa mamlaka ya kuteua bila kupewa uwezo wa kuwatumbua wateule wake!

Ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, zipo ibara ambazo zinampa mamlaka ya kuteua kwenye baadhi ya nafasi nyeti za watumishi katika nchi yetu, lakini hazimpi madaraka ya kutengua, kutokana na unyeti wa nafasi hizo

Miongoni ya nafasi hizo alizopewa mamlaka ya kuteua, bila kupewa uwezo wa kutengua ni pamoja na CAG na majaji wa mahakama kuu

Yeye anatamani katika kila nafasi aliyopewa mamlaka ya kuteua, vivyo hivyo apewe uwezo wa kutengua!

Hivi kwa "hobby" yake ya kuteua na kutengua, kama angepewa mamlaka hayo si nafasi zote wangekuwa wanafanya kazi ya "Praise and worship for Magufuli" kwa woga wa kutumbuliwa??

Kwa mwenendo wa kisiasa tunauona unavyoendelea ndani ya nchi yetu kwa hivi sasa, upo uwezekano wa kuwapata wabunge wengi wa CCM, katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, zaidi ya theluthi mbili, ambayo itawawezesha wabunge hao kupitisha muswada wa kuibadilisha Katiba ya nchi yetu

Kama tulivyoona, hali imebadilika hivi sasa, badala ya mkulima asiyejulikana kupeleka kesi mahakamani ya maombi ya kutaka ukomo wa vipindi vya kukaa madarakani kwa Rais uondolewe, hivi sasa yameanza kujitokeza majina maarufu, yaliyojiunga na mkulima huyo na kutamani Rais wetu aongezewe muda wa kutawala

Sote wananchi tumemsikia aliyekuwa Waziri mkuu wa zamani wa nchi hii, Mizengo Pinda, akieleza maoni yake mbele ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa, kilichoketi huko Mwanza, kuwa anatamani Rais Magufuli aongezewe muda wa kutawala nchi hii, angalau kwa kipindi cha miaka 15!

Wakati wananchi tulio wengi nchini tunatamani Katiba hii tuliyo nayo iondolewe kwa kuwa ni Katiba ambayo imempa madaraka makubwa mno Rais wa nchi, kumbe Rais wetu "anatamani" tuwe na Katiba mpya ambayo itakuwa mbovu zaidi ya hii tuliyo nayo hivi sasa, itakayompa madaraka makubwa zaidi sawa na Mungu

Watanzania wote inatubidi tupinge kwa nguvu zetu zote mipango hiyo "inayoandaliwa" kwa siri na watawala wa awamu hiii ya kutaka kurekebisha Katiba ya nchi hii tunayoiona kuwa mbovu, ili watuletee Katiba nyingine mbovu zaidi, itakayompa madaraka makubwa zaidi Rais na itakayoondoa ukomo wa Rais kutawala
 
Nchi ipo shwari Tuache kuzusha uongo
Ipo shwari kwako wewe kada wa Lumumba

Lakini kwa mamilioni ya wananchi wanaishi katika mazingira magumu mno na mateso makubwa ambapo hawajui Mkulu atatamka nini katika majukwaa ya kisiasa, ambapo wateule wake wanatekelsza matamko yake ya kwenye majukwaa ya kisiasa kama vile tayari yamekuwa SHERIA!
 
Itakapotokea rais yoyote anataka kukiuka katiba nyerere alishasema wazi jwtz iingilie haraka ndani kwa ndani bila hata wananchi kujua na taifa kuyumba fulstoop
Hiyo comment uliyotoa Mkuu Superbug, ina mantiki kubwa sana............

Kwa kuwa nchi hii hivi sasa watawala wetu wanaamini kuwa wao wameumbwa na Mungu ili waje watutawale maisha!

Wakiamini kuwa hakuna mtanzania mwingine mwenye uwezo wa kuongoza nchi hii
 
Hiyo comment uliyotoa Mkuu Superbug, ina mantiki kubwa sana............

Kwa kuwa nchi hii hivi sasa watawala wetu wanaamini kuwa wao wameumbwa na Mungu ili waje watutawale maisha!

Wakiamini kuwa hakuna mtanzania mwingine mwenye uwezo wa kuongoza nchi hii
Nakuapia mbele ya Mungu na wote watakaosoma post hizi kelele za wanasiasa hazitazidi veto ya majenerali wa jwtz ndio maana huwezi kusikia jwtz wameongea chochote ila ukitaka kuthibitisha ninachosema hebu rais yoyote wa jmt aliechaguliwa kwa kura za wanachi hata za wizi Kama walivyofanya 2015 ajiongezee hata mwezi mmoja kinyume na katiba uone itakavyokuwa kila siku makanali hawatatulia vikosini maana vifaru na mizinga vitakuwa vinapashwa joto wanaume watakuwa wanaomba bili kubwa za mafuta ya dizeli na petroli mamaeee bandarini kila siku ving'ora vya Navy vitalia kuuliza oyaaa infatriii tuliamshe dudeeeee ha ha ha ha msiombee mwendawazimu yoyote aongeze muda wa utawala wa kiraia mtalikaribisha jeshi mitaani bila sababu !!! Mungu ibariki Africa /// uzuri wanasiasa wanajua kwamba mipaka ya ujinga wao kulishika jeshi sharubu unaishi wapi!!!!
 
Mlilipwa pesa mwende Dodoma muunde katiba mpya mkakataa mkakimbia na pesa za wananchi mkala leo mnataka katiba ya nini

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Itakapotokea rais yoyote anataka kukiuka katiba nyerere alishasema wazi jwtz iingilie haraka ndani kwa ndani bila hata wananchi kujua na taifa kuyumba fulstoop
Alisema wapi na lini? Weka ushahidi ? Jeshi hili unalolilia dem wako kupigwa akienda nje

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnat
Mlilipwa pesa mwende Dodoma muunde katiba mpya mkakataa mkakimbia na pesa za wananchi mkala leo mnataka katiba ya nini

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
Mnatengeneza mazingira ya kihalifu makusudi ili watu wajivue kwenye dhambi zenu muda c mrefu wataamua kuelea kwenye bahari ya dhambi pamoja nanyi yetu macho.msije mkaomba po.
 
Vishetani vyake vidogo vinamuumbua kwa kuonyesha wazi dhamira aliyonayo Kama kishetani Cha kongwa
2181970_tapatalk_1555245893539.jpg
 
Shetani sifa kuu mojawapo ni kusema uongo, ndio maana kila siku pambio za kuongeza miaka au kufuta ukomo haziishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakika

Safari hii tumejionea siyo tu kwa akina Mkulima asiyejulikana kupeleka kesi mahakamani na akina Mbunge Mkamia kuomba kuondoa ukomo wa kutawala

Bali hivi sasa imehamia kwa majina mazito sana, kama tulivyoshuhudia kwenye kikao cha NEC, kwa aliyekuwa Waziri mkuu aliyestaafu, Mizengo Pinda, naye kujiunga na "Praise and worship team for Magufuli" na kudai eti anapendekeza Rais huyu aongezewe muda, kinyume na Katiba yetu ili atawale hadi miaka 15!
 
Back
Top Bottom