Askari mbona aliangushwa kizembe vileUtake usiteke hata kama mimi ndiye ningekua Sanya, jana ningeuwa Simba maana hakuna namna, huku nikijua natembelea pikipiki, watu waniahidi gari, na mbumba za kutosha. Urefa nini wananifungia kipindi cha mwaka mmoja, kwa kuzuga ila nikiwa nimekusanya maslahi ya miaka mitano, kwa sanya ni askari hategemei kuishi kwa kazi ya urefa. Kama mnategemea kilichotokea ni bahati mbaya poleni mashabiki wa Simba, wala wanaosimamia mpira mjue kuwa mengine nyie ndiyo chanzo, na mjuwe watu wanapenda mpira kuliko mnavyodhani. Mtu ataachana na mke au mumewe ila sio mapenzi ya Timu yake, angalia mipango mipango yenu isije leta dhahama.
Wakati mwinyi yupo rais wa tanzania aliwahi kuhudhuria mechi ya simba na yanga
Ile mechi haikumalizika mwenyekiti wa yanga wakat huo bw tarimba aliamuru timu yake itoke nje kabla ya mpira kwisha
Mwinyi alichukulia ni hali ya mpira tu
Magu angefanyaje...
Wewe kila kona siasa.... Unatia kinyaa mkuu2020 watabadili msimamo!
Bora umewapasha wanatetea ujinga, uharibufu wote huu bado mtu ana thubutu kuutetea!? Tena kwa hoja na mifano isiyo na mashiko hovyo sanaKuna watu mtaiponda serikali kwa hili lakini mimi naiunga mkono 100%. Watanzania imejaa wajinga wengi sana, viwanja vikiwa hamna wa kwanza kulaumu serikali, sasa vimetengenezwa mnaanza tabia za nyani mnavunja viti makusudi, alafu waafrika wakiitwa nyani wanakua wa kwanza kulalamika, hehehe! hizi tabia ni za myama gani sasa?
Ukweli unaumu!Wewe kila kona siasa.... Unatia kinyaa mkuu
Kwa nini ving'olewe? Kwa nini wavitoe sehemu yake na kuvitupa hii tabia lazima itafutiwe tiba adhabu hiyo halitoshi kabisa mkuu,Viti ni vizima tusikuze mambo sehemu za kufungia bolts ni laini sana ukivuta tu kiti kinaachana na bolt lakini vile viti ni vizima tu
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Hata huyo refarii wajana ni boya naye wamfungie miaka mitatu kwa kuharibu mechi
Ningeungana na wewe kuiponda serikali kama viti vile vingekuwa kwa ajili ya nyani maana yule ni hayawani chochote angeweza kufanya sio kwa binadam mwenye akili timamu afanye upuuzi huo uiponde serikali hapana mkuuMi naiponda serkal kwa kutengeneza viti visivyo imara. Ova
View attachment 410879 Kupitia Waziri mwenye dhamana ya Michezo Mh.Nape Nnauye leo akiwa ndani ya uwanja wa Taifa kuangalia uharibifu uliofanyika ktk mechi ya Simba na Yanga,Nnauye anasema jana alipigiwa simu na Mh.Rais JPM na akawa amekasirika sana kwa kitendo kilichofanywa na mashabiki wa pande zote mbili,upande wa nje karibu mageti nane ya upande wa Simba na Yanga yamevunjwa na ndani upande wa Simba kuna viti karibu 1782 zimeharibiwa.
Ghalama ya kila kiti ni shilingi laki mbili,hivyo kwa jumla ya ghalama ya viti tu bila mageti ni karibu milioni 300.Mh.Nape Nnauye anasema Rais amekasirika sana kwa kitendo hicho na alitaka adhabu iwe kali zaidi lkn wakaamua kama serikali ni kufungia Simba na Yanga kutumia uwanja wa Taifa mpaka hapo serikali itakaposema vinginevyo.Pia serikali imeamua kuzuia mapato yote ya Simba na Yanga mpaka hapo watakapothibitisha kulipa uharibifu wote uliofanywa na mashabiki wao.
Mh.Nnauye anasema wataenda mbele zaidi kwa kuweka kamera uwanjani ili waweze kunasa sura za mashabiki watakaokuwa wanafanya vitendo vya uharibifu.
Chanzo kikubwa cha vurugu katika mechi ya jana ilikuwa ni mambo mawili;kwanza ni mfumo wa kadi kufeli,kadi nyingi "ukichambisha" zilikuwa zinasema kadi fake na hapo mtu katoka kununua kwenye kituo halali na kwa watu halali,na kadi nyingine zinasema huna salio la kutosha.Na hata ukienda kwa polisi basi unaambulia kirungu au kofi kwa kudhaniwa ni "usanii"
.Hali hii ndio ilisababisha watu waanze kuvamia mageti kwa kuona hakuna namna.Kadi umekata na uwanjani usiingie.Serikali imtazame upya mzabuni aliyepewa kazi ya kuuweka mfumo wa kielectroniki ambaye majaribio yake ilikuwa ni mechi kubwa ya Simba na Yanga.Mfumo ulionyesha kushindwa kabusa kabisa.Mpaka saa kumi jioni,upande niliokuwepo watu karibu 500 kadi zao zilikuwa zinagoma.
Sababu ya pili ni Refa Saanya.Huyu maamuzi aliyoyafanya anastahili adhabu.Hili si la kuongelea sana maana lipo mikononi mwa bodi ya ligi,TFF na Chama cha Waamuzi.