Rais Magufuli asikitishwa na vurugu za mechi ya Simba na Yanga,Sasa zazuiwa kutumia Uwanja wa Taifa


Kwa Mujibu wa Nape kupitia ITV habari na Azam two habari saa mbili usiku wa Leo na kasema kapigiwa simu na Rais kuonesha kukasirishwa kwake na tukio Hilo, uharibifu wa Jana unahusisha pia kuvunjwa Mageti wakati wa Kuingia jee nalo hili linawahusu Simba peke Yao?
 
Watatumia uwanja gani? Wekeni njia mbadala za
kutatua matatizo kama ya kadi, kuwaelimisha mashabiki na wakifanya uharibifu basi mzuie pesa zao lakini sio kusema wote waadhibiwe kuto tumia uwanja wa taifa sabb ya wavuta bangi wachache.....
Ulaya wao hutumia camera kuwabaini mashabiki wakorofi na maamuzi ya refa hayawezi kuharibu viti au chochote uwanjani, mashabiki wa simba ndiyo waling'oa viti kwa hiyo pesa zikatwe kwenye mgao wa simba na mageti kila geti walipishwe kwani geti la yanga lilivunjwa na mashabiki wake.
 

Hatubishi kuwa hajapigiwa simu...tunachohoji ni nyie (na siyo comrasde Nape) kusema kuwa Rais amesema kuwa isiondolewe hata senti moja mpaka gharama zifidiwe...Nape hajasema hivyo yaani hajamhusisha Rais kwa maneno hayo....
 
Sasa hapo Yanga inaadhibiwa kwasababu gani? Kitendo cha kuzuia mapato ya Yanga kitawapa kiburi Simba ambao bila shaka wangekuwa tayari kugharamia uharibifu uliofanywa na mashabiki wao. Anyway, Azam wametengenezewa fedha za uwanja.
Ni kweli mkuu washabiki wa simba ndiyo waliharibu viti na simba ndiyo inapaswa kupewa adhabu ikiwemo washabiki wake kuzuiwa kuingia uwanjani lakini kule nje kuna mashabiki wa yanga waliharibu geti huko napo yanga itabeba jukumu la kurekebisha uharibifu huo.
 
Simba walipe gharama za viti pia geti lao lililovunjwa na yanga na wao wakatwe kugharamia geti moja lililovunjwa na mashabiki wake.
 
inafurahisha huku simba wanamsema Mwigulu aache unazi wa Yanga , huku Yanga wanasema Nape aache unazi wa Simba.....

Ningekuwa Magu pesa yote ya Jana wasingepata na kuwafukuzia wakachezee huko mkwakwani na morogoro
Kwanza kuendelea kuwaacha simba na yanga wautumie huo uwanja ni kuwadekeza..
Walipaswa wawe na viwanja vyao..
 
Mkuu ulaya wao hutoa adhabu kwa washabiki husika mfano walioharibu viti ni wa simba hivyo wanapaswa kuwakata simba kufidia hasara na yanga pia kule nje mashabiki walivunja geti nayo wakatwe kidogo kwani ukilinganisha uharibifu wa mashabiki wa simba ulikuwa mkubwa zaidi
 
kwa upande wa mageti ni pande zote kwani mageti ya yanga na mageti ya simba yalivunjwa
 
barafu. "kuchambisha" huu Msamiati mpya? Hata hivyo ni maamuzi ya Jazba Uwanja siyo wa aliye JUU au Nape, ni Mali yetu itafutwe njia ya adhabu.

Kwa Tanzania ya viwanda Hilo linawezekana.
 
hivi ninyi Simba na Yanga huku kunyanyapaliwa ni hadi lini?

badala ya kulialia hapa, tumieni unyanyapaaji huu kama fursa ya kupiga maendeleo kwa kujenga viwanja vyenu wenyewe.

ebo!!!
 
Kama Juma Punda Maharage hajui Simba na Yanga zina wafuasi wengi kuliko CCM na UKAWA kwa pamoja
Tusimlaumu sana, ukitoka mfano Rwanda utayajuaje haya?
 
Sisi wabantu ule uwanja ulitakiwa ujengewe viti vya zege, hatuna ustaarabu hata kidogo!
 
Kwanza kuendelea kuwaacha simba na yanga wautumie huo uwanja ni kuwadekeza..
Walipaswa wawe na viwanja vyao..

ni kweli serikali ndo inawaharibu sawa na mzazi anayelidekeza Toto la kiume la miaka 30 linakaa nyumbani na Dada zake
 
Viti vile havina gharama ya laki 2 Nape kaongeza tu namba labda uwe hujawahi fika Taifa ukakaa na kushuhudia mechi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…