Rais Magufuli azindua umeme wa gesi asilia Kinyerezi II, asema ataendelea kushirikiana na wananchi kulinda amani

Rais Magufuli azindua umeme wa gesi asilia Kinyerezi II, asema ataendelea kushirikiana na wananchi kulinda amani

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906


Rais Mhe. Dkt. John Magufuli leo atazinduzi mradi wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia (Kinyerezi II) Jijini Dar es Salaam.

Mradi huu utaingiza megawatts 240 katika gridi ya Taifa. Matangazo ya moja kwa moja yatarushwa na TBC 1 & Azam Two kuanzia saa 3:30 asubuhi hii.
=================================================

Shughuli imeanza

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM , Humphrey Polepole naye yupo kwenyye uzinduzi huo, ansema mradi huu wa umeme utasaidia Tananzania kufikia kwenye uchumi wa kati mwaka 2025 kwa kuzalisha umeme utakaoendesha viwanda vitakavyochakata mazao ghafi

Rais John Magufuli, amabye nimgeni rasmi wa uzinduzi huo anawasili kwenye uzinduzi huo akipokelewa na waziri wa Nishati na Madini pamoja na maafisa wa Tanesco na wajumbe mbalimbali

Mradi huo unatumia gesi asilia kutoa Mtwara, unatarajiwa kuzalisha Megawatt 240 za umeme ambao utaingizwa kwenye gridi ya taifa yenye Megawatt 2200 na kupunguza upungufu wa umeme mikoa ya Kusini kama Mtwara na Lindi

Waziri wa Nishati na Madini anakaribishwa na Mkurugenzi wa Tanesco, ndugu Mwinuka kumpa maelezo ya kiufundi kuhusu mradi huo

Baada ya kumaliza kukagua mradi huo, Rais Magufuli ameuzindua rasmi mradi huo wa Megwatt 240

Baadae Rais anatarajiwa kuzungumza na wananchi waliohudhuria kushuhudia uzinduzi wa mradi huu

Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda anatoa salamu na kuwatambulisha viongozi waliopo

Makonda anasema baada ya serikali kuhamia Dododma, jiji la Dar limekuwa jiji kubwa la kibiashara na linahitaji umeme wa uhakika

Makonda Jiji la Dar inahitaji Megawatt 548 na sasa wanapokea Megawatt 754 ila kuna changamoto ya kuwapelekea wananchi wautumia, eneo la Mbagala lilikuwa na tatizo la umeme lakini sasa hivi limetetuliwa kutokana na juhudi za serikali ya awamu ya tano

Changamoto nyingine kwenye Wilaya za Kigamboni na Ubungo zinaendelea kutatuliwa


Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco Titus Mwinuka anatoa taarifa fupi ya mradi

Serikali inapanua miradi ya kinyerezi kinatumia teknolojia mpya inayoitwa Combine Cycle ambayo ina ufanisi mkubwa wa kuzalisha umeme kutoka kwenye gesi

Mradi huo ulianza kutekelezwa tarehe 1 Machi mwaka 2016 na unagharimu Shilingi bilioni 700 uliofadhiliwa kwa mkopo kutoka Japan kwa asilimi 85% na fedha kutoka serikalini kwa asilimia 15% serikali imeshalipa fedha yote iliyotakiwa kutoa

Mitambo yote ishaanza kuzalisha umeme na sasa inazalisha megawatt 160 kwenye gridi ya taifa

TANESCO wanaomba kuondolewa gharama za VAT na kodi za usafirishaji wa vifaa na utoaji vifaa bandarini ili kuwapunguzia gharama ambazo kwa sasa wamesema hawawezi kuzimudu

Waziri wa Nishati na Madini, Medard Kalemani anazungumza

Amemkaribisha mwenyekiti wa kamati ya bodi ya wakurugenzi TANESCO, Dk Kyaruzi ambaye anamshukuru Rais kwa kuliwezesha tanesco kuwa na vyanzo mbalimbali ya kuzalisha umeme ikiwemo Stieglers Gorge

Kalemani anasema kukamilika kwa mapema kwa mradi huo ni kutokana na utayari wa rais kutoa fedha fedha kwa wakati na kwa mkupuo

Pia Rais amewawezesha kutekeleza mradi wa kinyerezi namba moja mwaka juzi ambapo unapanuliwa iliuweze kuzalisha nyingine Megawatt 185 na unatarajiwa kuzinduliwa mwakani na utagharimu kiasi cha dola milioni 180, fedha za ndani

Pia kunja Kinyerezi namba 3 ambao utazalisha megawtt 600 utakaotekelezwa kwa awamu mbili na Kinyerezi namba nne uatakaozlisha megawatt 450

Pia kwa sasa kuna njia kuu ya kusafirisha umeme wa backbone unaosafirisha megwatt 600 ambao ndio utakuwa unatumika kwenye viwanda

Pia ndani ya miaka miwili wameweza kuwaunganisha wananchi umeme kutoka milioni 1,054,000 hadi 2,014,000 ikiwa ni ongezeko la asilimia 30


Rais John Magufuli anahutubia,
Anawasalimu wageni waliohudhuria uzinduzi huo

Rais anashukuru wananchi kuhudhuriakwa wingi licha ya mvua kunyesha, pia anawapongeza Tanesco kwa kufanya kazi nzuri na kusema yupo pamoja nao na hatawaangusha.

Rais anasema hakutegemea kuona mradi umekamilika kwa kiasi kikubwa kama ilivyo na kusema kaulimbiu ya hapa kazi tu inatekelezwa ipasavyo

Pia anashukuru kuwa kwenye wafanyakazi zaidi ya 2000 asilimia 95 ni Watanzania na hivyo fedha zilizogharamia mradi huo zitabaki Tanzania na kuishukuru serikali ya Japan.

Rais anasema matatizo ya umeme nchini sio mabaya sana lakini jitihada kubwa na za makusudi zinahitajika ili kukidhi mahitaji ya uchumi wa kisasa

Bidii inatakiwa kuongezwa katika uzalishaji wa umeme katika nchi yetu

Rais anasema zaidi ya asilimia 60 ya Watanzania hawajaunganishwa na umeme kutokana na gharama za uunganishaji kuwa mkubwa

Mikataba ya uzalishaji ni ya hovyo ndio inayosababisha kuzalisha umeme kwa gaharama kubwa

Bei ya umeme tunaozlisha ipo juu ukilinganishwa na nchi zilizoendela na kusababisha uwekezaji kutoka nje kuwa mgumu

Gharama za mradi huo ni dola za Kimarekani milioni 344, na Japan imetoa mkopo wa dola milioni 294.4 na zilizobaki kutolewa na serikali ya Tanzania

Mbalina mradi wa Kinyrezi 2 kunaupanuzi wa mradi wa Kinyerezi 1 kufikia megawatt 185 ambao utagharamiwa na serikali na utakamilika mwakani

Pia tupo kwenye utekelezaji wa mradi wa Stieglers Gorge utakaozalisha Megawatt 2100 na fedha za utekelezaji wa mradi huo zipo

Tanzania itakuwa na karibia jumla ya Megawatt 5000 kutoka Megawatt 1500 na sasa Wizara ya Nishati itabidi kushusha umeme bei

Sasa bei ya kujiunganishia umeme imeshushwa hadi shilingi 7000 tu na Rais ameiponheza nishati kwa hilo

Rais anasema ameigawa wizara ya Nishati kuwa wizara mbili ili kila waziri awajibike kivyake na asiwe na visingizio

Rais anahimiza Tanesco kuongeza kasi ya kuunganisha wananchi umeme na kusema wananchi wanalalamika kucheleweshewa na saa nyingine kuombwa ruswa

Pia amewataka wananchi kuchangamkia fursa ya kujiunganishia umeme kwani serikali imeshusha bei yakuunganisha

Pia amaezitaka taasisi za serikali kushirikiana kwa karibu hasa katika kutekeleza miradi mikubwa ili isichelewe

Mfano kwenye uzinduzi wa magari ya bohari ya dawa bohari ya dawa ilillalamikia TFDA kutoshirikiana na bohari hiyo na kusababisha magari kukwama bandarini kwa sababu ya kodi

Anawataka watendaji wa serikali kuwasiliana ili kuepusha ucheleweshaji wa miradi na kusema mambo hayo yanamboa kweli kweli

Kama ni kifaa kinatakiwa kutolewa bandarini mara moja au kulipiwa fedha, kamishna wa TRA yupo na wizara ya fedha ipo, hivyo hakuna haja ya kuchelewesha

Rais anasema serikali inahamia dodoma lakini haina maana inaisahau Dar

Sasa Serikali inajenga barabara za juu Ubungo na Tazara ili kupunguza foleni, mradi wa mabasi ya mwendokasi kwenda tazara, ujenzi wa reli ya kisasa na upanuzi wa bandari ya Dar na mwelekeo wake ni mzuri

Pia serikali imepata mkopo wa bilioni 600 kutoa benki ya dunia ambayo itatumika kujenga barabara, masoko na madaraja katika jiji la Dar na inatarajia kukamili mwaka wa 2020

Amewataka wananchi kuendelea kuitunza amani na kushirikiana na serikali, wasiingizwe katika mambo ya udini,ukanda wala ukabila

Rais anasema aliapa kuilinda amani na atailinda amani kwa ajili ya wananchi

Pia amewaambia uongozi wa Tanesco kama kuna mabaki mabaki ya kuwaongeza wafanyakazi wao mshahara waongezewe
 
Hata JK alizindua vingi na vingine vilizinduliwa na mawaziri wake lakini kura zake ziliendelea kuporomoka.

Issue ni ajira,uchumi,watu kupoteza ajira, biashara kufungwa,mazao ya wakulima kukosa soko,bidhaa kupanda bei,kushindwa kuboresha masilahi ya watumishi,kodi zisizo rafiki kwa wafanyabiashara,n.k

Mengine ni sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii,mafao kwa wastaafu na wanaocha kazi,makato ya asilimia 15 kwa ajili ya Bodi ya Mikopo, manyanyaso kwa watumishi na wapinzani,Ma-DC na Ma-RC kuweka watu ndani hovyo hovyo,n.k.

Vile vile mengine ni kama tuhuma za mauji,utekaji,police brutality,lugha za kebehi, viburi,dharau,doublestandard,bomoabomoa,n.k

Sasa ni maendeleo ya vitu na si maendeleo ya watu na hili ndio tatizo.
 
Rais Mhe. Dkt. John Magufuli leo atazinduzi mradi wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia (Kinyerezi II) Jijini Dar es Salaam.

Mradi huu utaingiza megawatts 240 katika gridi ya Taifa. Matangazo ya moja kwa moja yatarushwa na TBC 1 & Azam Two kuanzia saa 3:30 asubuhi hii.
Tunasubiri vituko vipya na kauli za kejeli
 
Hata JK alizindua vingi na vingine vilizinduliwa na mawaziri wake.

Issue ni ajira,uchumi,watu kupoteza ajira, biashara kufungwa,mazao ya wakulima kukosa soko,bidhaa kupanda bei,n.k.

Sasa ni maendeleo ya vitu na si maendeleo ya watu na hili ndio Tatizo.
Huyu ni Rais Magufuli sio JK

Mambo mengine vumilia usije ugua ugonjwa Wa Moyo kwa kujitakia
 
Rais Mhe. Dkt. John Magufuli leo atazinduzi mradi wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia (Kinyerezi II) Jijini Dar es Salaam.

Mradi huu utaingiza megawatts 240 katika gridi ya Taifa. Matangazo ya moja kwa moja yatarushwa na TBC 1 & Azam Two kuanzia saa 3:30 asubuhi hii.
Jambo jema sana hili.
Hii ni hatua ya maana sana aiseeee, big up sana kwake.
 
Hata JK alizindua vingi na vingine vilizinduliwa na mawaziri wake.

Issue ni ajira,uchumi,watu kupoteza ajira, biashara kufungwa,mazao ya wakulima kukosa soko,bidhaa kupanda bei,n.k.

Mengine ni sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii,mafao kwa wastaafu na wanaocha kazi,makato ya asilimia 15 kwa ajili ya Bodi ya Mikopo,n.k.

Sasa ni maendeleo ya vitu na si maendeleo ya watu na hili ndio Tatizo.
Hadi miaka kumi ya Magufuli inakwisha ni either utachanganyikiwa au utapata cancer ya moyo
 
Eeeeh mwenyezi MUNGU msaidie raisi aongee Maneno ya busara na si maneno ya kuligawa taifa ameen .
 
Magufuli ni balaaa...So far he has done wonders so far no one to compare..Ni muda mfupi mno lakini hayafanani na maajabu aliyo yafanya
Kuna mambo ukiyaangalia mabayo imeishaifanyia nchi hii mpaka sasa unaweza stahajabu sana sema sisi binadamu tuna matatzo sana mostly watanzania wa mitandaoni
Chadema mkubali tu....2020 hamtakuwa na la kumsema magufuli juu ya utekelezaji wa aliyohaidi.....I believe mtakalo mnanga nalo ni ahadi ya million 50 kila kijiji hii ndio inaweza kuwa ajenda yenu kuu na kusema mlikuwa mnaonewa kuwekwa ndani....

Miundo mbinu safi...

Elimu mambo safi....

Madawa hospitalini mambo safi...

Rushwa safi...

Ujambazi wa kutumia silaha hata hatusikii zama hizi japokuwa tunaambia na ufipa maisha magumu.....

Rasilimali zetu safi...(na kesho kutwa anaenda kuzindua ahadi yake juu ya ukuta wa mererani)

Umeme siku hizi ni tofauti kabsa na awamu ya nne....

Nidhamu makazini safi....

Alihaidi kuleta ndege kaleta.....

Alihaidi kuhamia Dodoma anataimiza muda si mrefu.....
 
Hata JK alizindua vingi na vingine vilizinduliwa na mawaziri wake.

Issue ni ajira,uchumi,watu kupoteza ajira, biashara kufungwa,mazao ya wakulima kukosa soko,bidhaa kupanda bei,n.k.

Mengine ni sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii,mafao kwa wastaafu na wanaocha kazi,makato ya asilimia 15 kwa ajili ya Bodi ya Mikopo,n.k.

Sasa ni maendeleo ya vitu na si maendeleo ya watu na hili ndio Tatizo.
Mpaka 2025, utakuwa hoi bin taaban. Spidi ya jamaa naona unashindwana nayo.
 
Back
Top Bottom