Rais Magufuli huhitaji kujieleza unapomtoa Waziri. Kwa January Makamba jikalie kimya

Rais Magufuli huhitaji kujieleza unapomtoa Waziri. Kwa January Makamba jikalie kimya

Kwenye swala la mifuko ya plastic nampongeza sana Makamba.Hakuna kitu kinachoharibu mazingira kama mifuko ya Plastic. Kenya wameweza na hivi sasa nchi za Ulaya ziko katika hatua za kupiga marufuku mifuko ya Plastic na Kenya ikitolewa mfano kama nchi iliyofanikisha upigwaji marufuku wa mifuko hiyo

Natumaini waziri huyu mpya ataona umuhimu wa kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastic.
Kweli ukisikia wadanganyika ujue wapo wengi. Mifuko ya plastic ni mkakati wa Makamba? Hujui amedakia juu kwa juu tena baada ya kuchelewa sana? Na hata kama angekuwa ni yeye, muda wote aliokaa serikalini wewe unaona hilo jambo dogo kabisa linahalalisha kumpa sifa? Wengine naona mlikuwa mahawara ndiyo maana mnajitoa ufahamu.
 
Makamba yupo vizuri hao jamaa wa NEMC walikua kikwazo sana kwenye viwanda na faini za hovyo hovyo na mambo mengi ya ajabu ajabu sema ndio hivyo kufanya kazi na watu wasiotaka maendeleo wanataka siasa hawawezi kukuelewa kabisa...kama Makamba hafai hakuna anaefaa huko
Nyumbu toa maelezo kidogo. Hebu tueleze ushupavu wa huyu mtu wako.
 
Dah aisee sishangai haya maana sio mara ya kwanza Magufuli kusema uongo ....Alishasema alikuta sukari kilo ni 5000 wakati yeye ndiye aliyesababisha sukari kupanda bei.
Hivi ile salary slip yake ya mil9 alishaitoa???
 
Kazito kanafki sana kwakweli, mama samiha anatikisa kichwa kukubali kuwa la mifuko ya plastiki lilicheleweshwa kenyewe kanapinga utadhani ndiye makamu wa raisi. Siasa za unafiki zitatuumiza!! Rais akifukuza shida enzi hawafukuzi wanafosi maumbea ili afukuze what a shame. Mlifosi lowassa akafukuzwa kisa mjisifu mmejenga hoja sana leo imedhihirika alionewa...akiwa mwenyekiti PAC mashirika ya umma yalikuwa corrupt balaa kakashindwa kubadili huku kakijidai kako makini kumbe kanavutiwa mapepa kanatulia. Kwendraaaaa mwanasiasa feki na baradhuli.
 
Tafadhali sana ndugu zito,
Usije ukamshauri bwana January kujiunga na upinzani.

Tunataka abakie huko huko ccm.

Januari usije ukaenda chama chochote ch upinzani.

Usije ukathubutu.

Baki hapo hapo.
Chezeni karata zenu vizuri.

Ndiko anakoelekea huko...
 
Kavutabangi toka ACT kalipokosa ulaji kupitia zitto kanaingia CCM na kutamka wakongwe waondoke...
Sikuhizi kila MTU ni msemaji na mchambuzi wa siasa. Member hajafanya lolote bays na anahaki ya kuamini yeye ni bora,anapoona chama kinavurugika anahaki ya kuongea faragha na mwenzake juu ya anachokiona. Tuache unafiki
 
Zitto angalia usije kumponza January .... Kama kuchemsha kachemsha sana. Hakuna Kiongozi yeyote ambaye angemuacha madarakani kwa kitendo alichokifanya.

Rais ameonyesha ustarabu kwa kuongelea mengine na kuiacha sababu ya msingi ... Labda atakuwa ansubiri awafanyie kazi ndani ya vikao vya chama.
Kama mh rais haikumpendeza kutoa sababu za kumfukuza haikuwa na haja kutoa sababu zisizo. lazima zitajadiliwa
 
Makamba aliyemponza ni baba yake, zile audio na mipango yake dhidi ya mwenyekiti wake ni ushahidi tosha wa kufutwa uwaziri
 
Makamba aliyemponza ni baba yake, zile audio na mipango yake dhidi ya mwenyekiti wake ni ushahidi tosha wa kufutwa uwaziri
J makamba alikuwa anafanya wajibu na kazi aliyoagizwa nana baba yake...!! Asingeweza kupinga wala kukataa maana lile jambo halikuwa na ubaya wowote... Maana musiba ni kweli anawatukana na kuwadhalilisha wastaafu so ingekuwa haina maana wazidi kukaa kimya
 
Mimi nimeamua kuwa mtazamaji na msikilizaji mzuri tuu katika siasa za sasa za hii nchi.
 
Rais Magufuli kwenye sababu za kumuondoa January Makamba bora jikalie zako kimya.

Nimekusikia Rais leo ukijaribu kuelezea sababu za kumuondoa Uwaziri Bwana January Makamba. Kwa kweli hukuwa umejiandaa na maelezo ya kuridhisha.

Rais, kwenye suala la mifuko ya plastiki tunajua ukweli kwamba wewe ndiye ulizuia lisiendelee ulipoambiwa kwamba litaua viwanda. Tunajua kwamba January ndiye ametumia miaka mitatu kuwaandaa wenye viwanda vya mifuko ili wabadilishe teknolojia na wasipate hasara. Tunajua kwamba January alifanya vikao vya umma (public hearings) kuanzia Karimjee mwaka 2017 hadi Mwanza mwaka 2018 na kwingineko kushirikisha wananchi kwenye jambo hili. Tunajua kwamba hatukusikia kauli yako kwenye mifuko ya plastiki hadi baada ya suala hili kufanikiwa. Hii sio kawaida yako maana wewe ni very predictable.

Tunajua kwamba mlimtegea Makamba ili afeli halafu mumtimue. Hakufeli. Sasa mnamtimua kwa kukamilisha kazi kwa weledi mkubwa! Mhe Rais wewe ni mkali maelekezo yako yasipotekelezwa. Umemuachaje Waziri miaka minne kwa kutotii maelekezo halafu unamtoa baada ya utekelezaji? Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kukubali hoja yako hii dhaifu sana.

Bwana Rais ulikutana na wafanyabiashara kote nchini kutwa nzima. Walitaja kero zao zote, nami nikaziorodhesha. Sikusikia hata mmoja akilalamikia NEMC. Kwasababu gani? Kwasababu January ameibadilisha NEMC. Alitaka kuibadilisha huko nyuma na akavunja bodi na kuondoa menejimenti lakini kwakuwa inasemekana kulikuwa na ndugu zako walioguswa ukaagiza uamuzi ule ubatilishwe. Unadhani Watanzania wamesahau?

Bwana Rais fedha zinazotolewa na wahisani kwenye miradi ya mazingira zinakaguliwa na CAG na hakuna popote palipoonyesha ubadhirifu au upotevu. Kama upo uweke hadharani kama sisi tulivyoweka hadharani ubadhirifu wa TZS 1.5 Trilioni. Wacha wahisani, Serikali yako haijaweka hata senti tano kwenye miradi ya mazingira nchini. Mimi ni Mbunge na ninapitia kila Bajeti ya Serikali na Taarifa za CAG. Hujawahi kutenga fedha za Mazingira. Kwa kifupi, tunajua wewe binafsi sio mpenzi wa mazingira na umesema hivyo mara kadhaa. Hata huyo January mwenyewe “ulimtupa” kwenye mazingira ili apotee lakini ghafla kila Mtanzania leo anaongea mazingira. Hata wewe nawe leo unayaongea.

Bwana Rais hulazimiki kutoa sababu unapomuondoa Waziri. Kwa kutafuta kutoa sababu zisizoshiba leo, umeonyesha kwamba umesikia hisia za Watanzania kuhusu kuondolewa January Makamba. Umeondoa Waziri kipenzi cha Watanzania na Waziri weledi. Tunajua umemfukuza kwasababu nyingine, sio uchapakazi. Watanzania wote tunajua kwamba siku zote alikuwa anatafutiwa sababu tu ya kuondolewa. Ukisema uchapakazi ndio sababu Watanzania tunakushangaa kwasababu hawa mawaziri umewateua wewe lakini tathmini tunafanya sisi Watanzania. Na January Makamba ndiye alikuwa Waziri mbunifu na bora kabisa. Na ataendelea kuwa maarufu miongoni mwa Watanzania. Hakika ana nafasi kwenye uongozi siku sio nyingi sana zijazo. Mabadiliko ni lazima na January naamini atakuwa sehemu ya mabadiliko ili kujenga Tanzania inayojali watu wake na yenye Demokrasia iliyokomaa

Zitto ZR Kabwe
Mbunge Kigoma Mjini
Ningeamini anastahili sifa unazompa JM kama angekuwa na msimamo imara kuhusu:
1. Steiglers Gorge hydro electric power project.
2. Uranium mining Bahi na huko Selous National Park
3. Asbestos removal from Dampo Ilala and else where
Lead contamination in building materials.
3. Mercury poison in gold mining areas.
4. PCB ground water pollution from industrial and automotive waste.
5. Annual flooding of the Msimbazi creek and it's impact on housing and infrastructure at Jangwani, Vingunguti and other areas.
6. Strict implementation of project environmental impact assessments in compliance with the existing laws.
7. Comprehensive public participation in the environmental assessments process.
Maana ya hayo mambo yote juu ni kuipa meno NEMC. Kitu ambacho JM, kama watangulizi wake, hakufanikiwa.
 
J makamba alikuwa anafanya wajibu na kazi aliyoagizwa nana baba yake...!! Asingeweza kupinga wala kukataa maana lile jambo halikuwa na ubaya wowote... Maana musiba ni kweli anawatukana na kuwadhalilisha wastaafu so ingekuwa haina maana wazidi kukaa kimya
Kwa level ya wazaziri kupanga mambo kama yale ni utoto, na hao wote wanafutwa uanachama wa ccm, mda utakapo fika

Sasa unatumwaje na mzee wako ufanye mambo kama yale? kwann yeye asifanye na wazee wenzake?
 
Back
Top Bottom