Rais Magufuli ni Jemedari kweli wa Vita ya Ufisadi na Rushwa-Jua fedha, majengo, na vitu vingine kibao vilivyorejeshwa Serikalini. Big up JPM

Rais Magufuli ni Jemedari kweli wa Vita ya Ufisadi na Rushwa-Jua fedha, majengo, na vitu vingine kibao vilivyorejeshwa Serikalini. Big up JPM

Securelens

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2020
Posts
316
Reaction score
541
Moja ya kazi nzuri aliyofanya Mheshimiwa Rais Magufuli ni kupiga vita ufisadi na rushwa kwa vitendo. Mashauri makubwa ya ufisadi 407 yamepelekwa mahakama ya mafisadi na mashauri 385 yamesikilizwa.

Aidha kupitia Takukuru mashauri 2,256 yalifunguliwa ambapo mashauri 1,926 tayari yametolewa uamuzi na serikali imeshinda mashauri 1,013. Tayari Serikali imeokoa bilioni 273.38 zikiwemo fedha walizo dhulumiwa wakulima sehemu mbalimbali. Takukuru imetaifisha fedha taslim shilingi milioni 899, $1,191,651, €4,301,399, nyumba 8 za thamani ya bilioni 11.6, magari , viwanja na mali zingine.

Aidha serikali imerejesha mali za serikali zilizochukuliwa isivyo halali na watu binafsi zikiwemo nyumba na majengo 98 ikiwemo Mbeya Hotel, viiwanja 298, kampuni 3 na maghala 69. Pia zuio limewekwa kusubiria kukamilika kwa taratibu za kisheria za utaifishaji wa mali mbalimbali zikiwemo fedha kiasi cha shilingi bilioni 52.7, $ milioni 55.5, € miloni 4.3, magari 75, nyumba 41, viwanja 47 na Mashamba 13.

Kwa kweli hakuna kama Rais Magufuli. Watanzania wote tunaochukia ufisadi na rushwa tunakwenda na Rais Magufuli hadi 2025 kwa kumpa kura nyingi. Amethubutu na Ameweza (Source za Takwimu zote ni Hotuba ya Mheshimiwa Rais Magufuli alipokuwa akivunja Bunge tarehe 16 Juni 2020).

Mafisadi na wala rushwa kadhaa walioumia wakati wa utawala huu wanahangaika huku na kule laying wameshindwa. Watanzania tumeamua tunakwenda na jemedari huyu wa vita ya ufisadi na rushwa. Oktoba 28 tunampa kura za mafuriko Rais Magufuli. Jiunge na kundi la watanzania la ushindi kwa JPM.
 
Chenge alikula hela ya rada kafanywaje?
Fisadi Rostam , lowasa, Karamagi wote wapo ccm kawachukulia hatua gani na yeye anasema ameanzisha mahakama ya mafisadi? Au hiyo mahakama ni ya kuwanyoosha wapinzani wake? Na yeye mwenyewe fisadi ajipeleke kwenye hiyo mahakama yake ya mafisadi
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hafai huyu aondoke. Hatutaki Maendeleo ya vitu, tunataka ya watu
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Nyumba za serikali zinarejeshwa lini? Nani aliziuza kwa Bei ya kuku?
 
Hivi kuna nyumba flani hivi za serekal ziliuzwa wakati flani na yeye au??? Nauliza sijui kucha zangu nzuri nazipenda
 
Ndugu yangu Kinyungu, utawala wa JPM ni wa kisheria na haki. Ni vyombo vya sheria pekee vinavyomtia mtu hatiani siyo hisia wala mhemuko wa mtu. Huo ndio utawala wa sheria na utoaji wa haki anaosimamia Rais JPM na ndiyo maana watanzania wanampenda na watampa kura nyingi.
 
Vipi kivuko kibovu alichonunua kwa mabilioni ya fedha?Watu walioanza kupiga kelele akaamua kukikabidhi kwa jeshi ili kisizungumziwe tena!
Kampuni ya ujenzi manyanga construction company iliyojenga uwanja wa ndege chato ni ya nani?
 
Ndugu yangu Kinyungu, utawala wa JPM ni wa kisheria na haki. Ni vyombo vya sheria pekee vinavyomtia mtu hatiani siyo hisia wala mhemuko wa mtu. Huo ndio utawala wa sheria na utoaji wa haki anaosimamia Rais JPM na ndiyo maana watanzania wanampenda na watampa kura nyingi.
Yeye ni Kafisadi kajenga uwanja wa kimataifa kijijini kwao.

Kafisadi kahamishia mbuga kijijini kwao.

Kafisadi hela za tetemeko.

Kafisadi ile 1.5 trillion kwenye hesabu ya CAG.

Bora lowassa na chenge kwakweli.
 
Vipi kivuko kibovu alichonunua kwa mabilioni ya fedha?Watu walioanza kupiga kelele akaamua kukikabidhi kwa jeshi ili kisizungumziwe tena!
Una ushahidi na unachokisema au ni hisia zako tu mkuu. Please weka ushahidi as kama hauna bora kunyamaza ndugu yangu. Nayo ni ustarabu wa kisomi
 
Yeye ni Kafisadi kajenga uwanja wa kimataifa kijijini kwao.

Kafisadi kahamishia mbuga kijijini kwao.

Kafisadi hela za tetemeko.

Kafisadi ile 1.5 trillion kwenye hesabu ya CAG.

Bora lowassa na chenge kwakweli.
Hizi ni kauli za kuokota mitaani, njoo kidogo kisomi ndugu tujadiliane ukiwa na ushahidi
 
Kama kafanya yote hayo kuna haja gani anapiga magoti kaa zezeta..?!
Rais wa ovyo kabisa kuwahi kutokea tangu iwepo nchi ya Tz.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom