Omusolopogasi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2017
- 7,101
- 18,051
Bila ushirikiano wa wananchi kwa nguvu zao kamwe hatuwezi kuipata to tume huru na hiyo kazi tukiwaaachia kina Mbowe na Lema tutakuwa tuna waonea tu
Ndugu ukiwalaumu wapunzani sidhani kama utakuwa huwatendei haki.
Siasa za nchi hii unazijua fika, ebu angalia wale woote walio kuwa wana engineer hayo mabadiliko ya katiba leo hii wana kesi ngapi mahakamani?
1:Mbowe
2:Lisu
3:Mdee
4:Zitto
5:Msigwa
6:Lema
7:Sugu
7:Matiko
Ukifuatilia utagundua kuwa wabunge wote walio kuwa wana isumbua serikali wana kesi mahakamani au walisha hukumiwa kutumikia adhabu.
Niwachache sana ambao hawajagusa viunga vya mahakama
Misingi ya haki dunia nzima ni kwamba ni lazima idaiwe. Hata kama ni darasani mwalimu akiwaona mko soft soft anawaburuza. Huu ndio wakati wa kuweka mgombea shupavu mwenye kauli na matendo imara. Ni aibu sana kuendelea kusakamwa na matukio ya kutotendewa haki halafu watu wanaojitambua wakaendelea kukaa kimyaMimi napendekeza kuwa uchaguzi wa mwaka huu ugeuzwe kuwa fursa ya mapinduzi ndani ya nchi yetu. Wapinzani wa kweli ongozeni umma kwenye mapinduzi. Kwa kauli ya Magufuli ni kuwa watafanya kila litakalowezekana pasiwe na upinzani wa kweli mara baada ya uchaguzi.
Kitendo chochote cha kukosa haki ni lazima kikabiliwe na upinzani imara hata kama hiyo itabidi kufanya vurugu. Itisheni civil disobedience. Zile kauli za woga kwamba 'hatutaki kuingia ikulu kwa damu za watu' ziachwe kabisa, kwani sasa ni dhahiri kuwa haki haiwezi kutolewa bali itadaiwa.
Comment safi kabisa. Natamani mgombea urais awe Lissu na muongoza kampeni awe John Heche uwe mwendo wa nyundo tu. CCM Wakipiga nyundo inajibiwa haraka na kwa uhakika na team ya CHADEMA. Hakuna kurembaWatumie wananchi, wasifanye wenyewe. ndio maana ya uongozi. Mbowe tena usimeseme. Ndiye mwoga. Mimi nadhani kuwa Chadema ingeongozwa na Lissu, Heche ama Lema, kungekuwa na mabadiliko ya kweli. Mbowe amekubali kuwa kiongozi wa upinzani bungeni na anaona hiyo inamtosha.
Shetani hajawahi kumshinda Mungu , mimi binafsi kwa maono yangu Magufuli kipindi chake cha Urais kitakwisha baada ya miaka mitano
ni Mungu pekee awezaye kupanga nani atafika keshoLakini ukumbuke utamaduni wao haujabadilika wa kumwacha aliyeko madarkani kumalizia vipindi vyake vyote viwili
Mh, nina wasiwasi sana. Dictators haveno mercy! Nimeishi wakati wa Idd Amin, , najua ninachokiongea! Unless external force imlazimishe kutenda haki, yeye mwenyewe hawezi!
ni Mungu pekee awezaye kupanga nani atafika kesho
Ameen! I get you but "Lucky" may be on his side!Retired, don't retire on this! Mungu ana njia nyingi hata hiyo unayosema anaweza akaiamrisha yeye. Kumbuka kilichofanyika Zimbabwe. Smoothly. Au kwenye mkutano wake wa kwanza wa kampeni akakumbana na chango lililomwondoa Herode duniani. Nani alijua kuondoka kwa Nkurunziza kutakuwa kutokukabidhi ikulu kwa rais mteule. Mungu ni hatari. Hawahi wala hachelewi. Aishiye kwa upanga, hufa kwa huo. Every dog has its appointed day. Let's play cool. God is omniscient, omnipresent and omnipotent. Let everybody shout Ameeeen!
Mpaka sasa tunaingia kwenye uchaguzi ilhali sheria inayohusu muundo na uendeshaji wa tume ya uchaguzi bado haijabadilishwa. Wateule wa tume na makamishna wake watabaki kuwa uteuzi wa rais. Kuna tume huru hapo?Tukiingia kwenye uchaguzi bila ya kutengeneza mazingira ya uchaguzi huru na wa haki (hususani bila tume huru), si rahisi kwa wapiga kura wanaotaka upinzani ushike dola kushiriki kwenye uchaguzi ambao rais tayari keshatoa amri kwa vyombo vyenye wajibu wa kusimamia uchaguzi kuwa ni wabunge wa CCM pekee ndiyo watakaorejea bungeni.
Duuh . . . comment yako imenifadhaisha na kunisikitisha sana kuhusu kule tunakoenda kama taifa. Nimewaza mbali sanaKuna kila dalili hakuna uchaguzi huru na wa haki hata kwa asilimia 40!
raisi ameshapanga wa kurudi ni akina nani!
Ameshakuwa msemaji wa wapiga kura
Msemaji wa tume huru ya uchaguzi
Pia hata wapinzani wakishinda maana yake DED hakuna kuwatangaza tangaza wa ccm!
Nani amekuambia kazi ya chama cha upinzani ni kuimba nyimbo na mapambio ya chama tawala?Acha apotoshe ukweli ni kuwa hawarudi. Nani atachagua Chadema pinga pinga?
Kuna kuimba mapambio na kusema ukweli. Lazima utofautishe. Mradi wa JNHPP ukikamilika utakuwa na manufaa makubwa sana kwa taifa letu. Lakini Chadema walipinga sana usifanyike. Sasa hao unadhani watarudi Bungeni?Nani amekuambia kazi ya chama cha upinzani ni kuimba nyimbo na mapambio ya chama tawala?
Mimi nafikiria exactly kama wewe. Na kushinda haya mapambano ni rahisi sana mkuu! Tena ni rahisi sana!Mimi napendekeza kuwa uchaguzi wa mwaka huu ugeuzwe kuwa fursa ya mapinduzi ndani ya nchi yetu. Wapinzani wa kweli ongozeni umma kwenye mapinduzi. Kwa kauli ya Magufuli ni kuwa watafanya kila litakalowezekana pasiwe na upinzani wa kweli mara baada ya uchaguzi.
Kitendo chochote cha kukosa haki ni lazima kikabiliwe na upinzani imara hata kama hiyo itabidi kufanya vurugu. Itisheni civil disobedience. Zile kauli za woga kwamba 'hatutaki kuingia ikulu kwa damu za watu' ziachwe kabisa, kwani sasa ni dhahiri kuwa haki haiwezi kutolewa bali itadaiwa.
Tujitayarishe kwa mapambano, na kwangu sioni mgombea wa urais anayeweza kuliongoza hili isipokuwa Mh Tundu Lissu. Mbowe ni kiongozi mzuri lakini ni soft sana, na mwoga. Nyalandu ndiyo kabisa hili haliwezi. Tujiandae kwa mapambano, wananchi wataunga mkono wakiona mko makini.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
Yesu kashindwa kumponya mama yake,kaomba tumsaidie kuomba yesu huyu wa sgr ni kwikwiVyama vya upinzani mmeona hicho kigongo kutoka kwa mshika dola?
Maneno haya aliyoyasema Rais yalipaswa yatolewe kwenye CCM campaign rally na siyo ndani ya chombo huru (at least kikatiba) kama bunge. Ana audacity ya kuonyesha upendeleo wa wazi kwa chama chake mahali ambapo si pake (bungeni) na yeye ni rais anayetakiwa kuwaunganisha watu wote hususani tunapoelekea kwenye uchaguzi.
Tukiingia kwenye uchaguzi bila ya kutengeneza mazingira ya uchaguzi huru na wa haki (hususani bila tume huru), si rahisi kwa wapiga kura wanaotaka upinzani ushike dola kushiriki kwenye uchaguzi ambao rais tayari keshatoa amri kwa vyombo vyenye wajibu wa kusimamia uchaguzi kuwa ni wabunge wa CCM pekee ndiyo watakaorejea bungeni.
Zitto Kabwe, John Mnyika na wengineo - you have the whole monster ahead of you to fry.
Ulitaka wafanye nini?Wapinzani walikuwa na miaka 5 ya kutafuta katiba mpya yenye kuweka mazingira ya uchaguzi huru na wa haki. Tena hapo mwanzo 2016 walikuwa na Wabunge wengi sana na nguvu ya kutosha.
Lakini walitulia tuli baada ya kuambiwa kuwa hakuna mikutano na maandamano. Kwa sasa it's too little too late. Siyo siri tena - dikteta atawatoa wote Bungeni. Alikwishawatoa kwenye serikali za mitaa tayari.