Rais Magufuli nisikilize kwa makini, Sitaki upoteze muda bure

Rais Magufuli nisikilize kwa makini, Sitaki upoteze muda bure

Sijaandika ili nipewe like au watu wakoment, nimeandika watu wasome, watakaopenda wapende, watakaochukia wachukie, watakaojifunnza wajifunze, watakaopuuzia wapuuzie.
Bila shaka na "watakao shauri" na watakao'criticise', nao kwako watakuwa sawa, au sio?

Naona kama 'ngozi' yako kidogo ni nyembamba kutokana na majibu unayowapa wanaodhani andiko lako haliko kamilifu. Najua, kwa umri wa miaka 26, pengine jambo hili sio la ajabu sana. Lakini ukitaka kukomaa katika fani hiyo ya uandishi, bila shaka hata hao wanao'critic' maoni yao utayapima kwa kina na sio kuwashambulia kama unavyofanya kwa kuamini kwamba "...kila mtu unam'treat' jinsi anavyokuja." na kwamba "hiyo ndio haki"?
Nitakubaliana na dhana hii kama mhusika katukana, au kaandika upuuzi usioendana na mada yenyewe. Lakini kama ni kupishana misimamo tu, utakuwa unapoteza fursa ya kujifunza toka kwa wengine.

Nimeona nikupe tu ushauri huu kama unataka kuwa mwandishi mahiri.
Hamna Mkuu, kila mtu unamtreat jinsi anavyokuja hiyo ndio haki
 
Bila shaka na "watakao shauri" na watakao'criticise', nao kwako watakuwa sawa, au sio?

Naona kama 'ngozi' yako kidogo ni nyembamba kutokana na majibu unayowapa wanaodhani andiko lako haliko kamilifu. Najua, kwa umri wa miaka 26, pengine jambo hili sio la ajabu sana. Lakini ukitaka kukomaa katika fani hiyo ya uandishi, bila shaka hata hao wanao'critic' maoni yao utayapima kwa kina na sio kuwashambulia kama unavyofanya kwa kuamini kwamba "...kila mtu unam'treat' jinsi anavyokuja." na kwamba "hiyo ndio haki"?
Nitakubaliana na dhana hii kama mhusika katukana, au kaandika upuuzi usioendana na mada yenyewe. Lakini kama ni kupishana misimamo tu, utakuwa unapoteza fursa ya kujifunza toka kwa wengine.

Nimeona nikupe tu ushauri huu kama unataka kuwa mwandishi mahiri.

Mkuu, kwenye mijadala mtu akiku-criticise huwezi kukubali na kupokea kirahisi, hii inaua mjadala, hivyo ni lazima ushambulie zaidi ili mjadala uwe mzuri kwa kumfanya aliyeku-criticise azidi kushusha nondo zitakazokufanya ujione mjinga, na hapa ndipo watu wengine watajifunza.

Sasa mtu anakuambia hujui historia bila kushusha nondo yoyote inayothibitisha kuwa sijui historia unafikiri nitakubali
 
Kweli wewe bado mtoto mdogo. Ujeruman, China na Korea Kaskazini ziko hapo zilipo kwa juhudi za watu kufanya kazi kwa bidii.

Mao aliwachimbisha wachina visima vya mafuta hila ya mitambo.

Hitler aliwakusanya wasomi na kuwaweka kambini kisha kuwaamuru watengeneze mitambo ama mifumo kulingana na taaluma zao.

Kasome tena kisha urudi hapa.
Huku Tanganyika Wajerumani walikuja kufanya nini,pili Wachina wamekuja wengi huko Tanzania na AFRIKA kufanya nini?
 
Kuitumikisha nchi nyingine sio lazima uende na jeshi lako huko.

Niliowashauri wanajua nazungumzia nini,

Hakuna sehemu niliyosema watu wasifanye kazi kwa bidii, lakini msingi wa mada yangu umejikita zaidi katika kuwatumikisha na watu wa mataifa mengine, na hapo ndipo ulipo utajiri, maendeleo na kujitawala
Kweli we bado mtoto...unawatumikishaje raia wa nchi nyingine wakati tatizo la nchi yetu ni sisi wenyewe akili zina walakini....sababu nchi ina utajiri wooote lakini bado ni masikini wa kutupwa...sasa hapo kuna uhusiano gani na kuwatumikisha wengine ambao wana akili kuliko wewe?huwa wanakuja kama wawekezaji na wanaiba wanaondoka....toa mfano wa hiyo nadharia yako ya la Saba B
 
Mtoa mada pengine ana pointi lakini amezunguka mno....lakini huwezi kuwatumikisha raia wa nje na ukapata maendeleo. hasa wanaokuzidi kiakili ,kimtazamo,kiuchumi nk .....China ilipata maendeleo baada ya kuruhusu wawekezaji wakubwa wa nje kuwekeza kwao ....ila wao ndiyo wakatumikishwa kama cheap labour ...na soko kubwa la bidhaa zinazotengenezwa kule ni soko la ndani kwanza hivyo population yao ikawabeba.....hapo waka boost uchumi fasta.....sasa mtoa mada anaongelea kitu gani sijui.
 
Mtoa mada pengine ana pointi lakini amezunguka mno....lakini huwezi kuwatumikisha raia wa nje na ukapata maendeleo. hasa wanaokuzidi kiakili ,kimtazamo,kiuchumi nk .....China ilipata maendeleo baada ya kuruhusu wawekezaji wakubwa wa nje kuwekeza kwao ....ila wao ndiyo wakatumikishwa kama cheap labour ...na soko kubwa la bidhaa zinazotengenezwa kule ni soko la ndani kwanza hivyo population yao ikawabeba.....hapo waka boost uchumi fasta.....sasa mtoa mada anaongelea kitu gani sijui.

Nashukuru kwa umaliziaji wako, hasa uliposema hujui ninaongelea nini, kwani umeonyesha dhahiri ni kweli hujui
 
Una mawazo mazuri sana mkuu.
Mawazo haya hayakuja hivi hivi inaonekana umeyafanyiakazi kwa utafiti mzuri ulioufanya.

Aina ya maendeleo unayoiangazia inakuwa na nguvu sana kwa nchi ambazo zimeshaendelea maana hawana recources tena na wanachokifanya ni hila za kubakia kileleni mwa uchumi na kijeshi.

Watanzania wakibweteka itakuwa vigumu sana kwa kusimamia utumikishaji wa mataifa mengine hivyo kwanza tujenge msingi wa kujitumikisha ili tuje kuwa manyapara wazuri....
 
Kweli we bado mtoto...unawatumikishaje raia wa nchi nyingine wakati tatizo la nchi yetu ni sisi wenyewe akili zina walakini....sababu nchi ina utajiri wooote lakini bado ni masikini wa kutupwa...sasa hapo kuna uhusiano gani na kuwatumikisha wengine ambao wana akili kuliko wewe?huwa wanakuja kama wawekezaji na wanaiba wanaondoka....toa mfano wa hiyo nadharia yako ya la Saba B
Utajiri ni watu, na watu ndio utajiri.
Ukijua hilo litakusaidia
 
Una mawazo mazuri sana mkuu.
Mawazo haya hayakuja hivi hivi inaonekana umeyafanyiakazi kwa utafiti mzuri ulioufanya.

Aina ya maendeleo unayoiangazia inakuwa na nguvu sana kwa nchi ambazo zimeshaendelea maana hawana recources tena na wanachokifanya ni hila za kubakia kileleni mwa uchumi na kijeshi.

Watanzania wakibweteka itakuwa vigumu sana kwa kusimamia utumikishaji wa mataifa mengine hivyo kwanza tujenge msingi wa kujitumikisha ili tuje kuwa manyapara wazuri....

Naam Mkuu,

Rais Magufuli anafanya vizuri, nafikiri baada ya kuwapasha watanzania akili, itakuwa ndio Turning point ya kuvamia nchi zingine na kuendelea.

Watanzania bado tuna mawazo madogo mno, imagine mtu akinunua kigari ndio kafanikiwa.
 
Kutawala watu wengine kunahitaji mfumo
Lakini pia maendeleo ni matokeo chanya ya kuwa na mifumo imara ambayo haiwezi kiingiliwa na mtu, kundi la watu, taasisi, za ndani na nje ya Taifa, n.k. na zaidi ya yote mifumo hiyo imara iwe na checks and balances, vinginevyo Mh Rais ataimba sana.
 
Kwanini tusiwavamie wakenya tuchukue vinavyofaa kuchukua? 🤔
 
Lakini pia maendeleo ni matokeo chanya ya kuwa na mifumo imara ambayo haiwezi kiingiliwa na mtu, kundi la watu, taasisi, za ndani na nje ya Taifa, n.k. na zaidi ya yote mifumo hiyo imara iwe na checks and balances, vinginevyo Mh Rais ataimba sana.
naam mkuu
 
Philosophy iliyotumika kwa huyu jamaa ni kubwa, anaposema mada hii imelenga baadhi ya watu yuko sahihi, Jack Ma tajiri wachina anatumia sana concept hiyo
 
Asante ni mada nzuri ila haujafanya comparative economic developmental path analysis ya kutosha. Yafuatayo ndio ndio ya kuangalia kwa undani, ni lazima ujue.

1) Uwezo wako kiutendaji ambao unao na wengine hawana au umewapita kwa ufanisi

2) Unatakiwa uzijue vizuri sana resources zako zote na hasa zile ambazo ni distinct.

3) Ufahama majirani zako na uwezo wao.

4) Ujue majirani zako wanatamani nini kwako.

5) Legeza sana sheria kwa mambo yote unayo yaweza au umewashinda wenzako na yanafanywa na watu wako kwa ufanisi.

6) Weka sheria ngumu kidogo kwa ambo usio yaweza ili uweze kuyadhibiti na upate nafasi ya kujifunza na kuyatawala.

7) Tengeneza nguzo nzito za uchumi ki taasisi na wananchi na ikiwezekana wape bure au kwa upendeleo mkubwa kwa wateule kwa mwananchi au taasisi.

8) Hakikisha watu wengi wazuri na watu maskini kutoka njee ya nchi yako wanamiminika nchini kwako, kwa kuwa cheap labour ni moja ya vishawishi kwa matajiri kuendelea kuwekeza kwako, ukashinda hakikisha kuna jamii nchini kwako hazitoki kwenye umasikini ili kuwa na pool kubwa ya kuwa tumikisha.

9) Hakikisha resources zote za ndani na za nje unazitumia kikamilifu.

10) Angalia soko la Nje sana kuliko soko la ndani.

11) Hakikisha post secondary practical training inaimarishwa sana sana ili uwe na skilled labour.

Jaribu kuangalia haya mambo niliyo pendekeza kwa upana na uone utaimarishaje utajiri wa nchi.

Maendeleo ni mchakato na muda Unatakiwa, kila mara uangalie hakuna short cut ila kuna kupunguza muda ambao kwa kawaida ungehitajika nchi kuimarika kiuchumi.
Well said,mambo ndo haya sasa!
 
Mkuu nakupongeza kwa kuibua mjadala mzito na fikirishi.

Katika Scenario ya uchumi...maliasili ni fixed yaan haziongezeki. Zinatumika inafika muda zinaisha yaan ni Scarce. Ndo maana inaibuka concept ya one tobe better off someone should be worse off

Nchi za ulaya waliweza kutumia resources zao zikaisha na kwa vile supply ya resources ni fixed zikaamua kuzitafuta overseas. Ndo wakaja Africa na kwingneko. Baadae wakabadilisha mbinu ikawa neo-colonialism (strartegic influence)

Case study yetu ni Tz.
Kabla ya kutoka nje ya mipaka yetu, je resources zetu tunazitumia optimumly? Au huko nje tunaenda kuchukua kitu gan ambacho sisi hatuna? Coal? Gas? Diamond? Uranium? Or what else?

Tatzo la nchi yetu ni Technology . We are lacking modern techn. Na hii inasababishwa na sera mfu. Korosho, kahawa, tumbaku, mbaazi, mahindi, viazi, mchele, matunda etc. Hivi vyote vinaozeana huku ndani ilihal vinatakiwa kwa wingi huko nje. Sera zetu ni za kukomoana. Sio ajabu kumkuta mtu ana semi 4 amezuiliwa kusafirisha mahindi kenya ilhal ndanibyapo ya kutosha yenye kuuzea bei chee. Yaan at expense ya mkulima watu wanauziwa vyakula bei ya kutupwa ilhal industrial finished goods vinauzwa kwa bei kubwa. Yousee the problem.

Mtu ameanzisha biashara unampigiamakodi beyond the limit. Ado unataka uwatatawale majirani zako ilhal ww mwenyewe huwezi kujtawala? Marekani yule unavyomuona yuko radhi kutumia hundred billions dollars kumtafuta a lay-man American citizen. Vip ww, unawajali watu wako?

Hitimisho. Tutatue haya tuliyonayo kwanza kabla hatujavuka mipaka. Kama familia yako inakushinda kuongoza, utaweza kuongoza familia 5 jirani?
 
Back
Top Bottom