Rais Magufuli, tafadhali mpeni Tundu Lissu ushirikiano, msaidieni atulie na baada ya uchaguzi ndio kesi zake ziendelee

Rais Magufuli, tafadhali mpeni Tundu Lissu ushirikiano, msaidieni atulie na baada ya uchaguzi ndio kesi zake ziendelee

S.M.P2503

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2008
Posts
2,421
Reaction score
4,344
Tafadhali sana mheshimiwa sana, Raisi wetu, Dkt. Magufuli, yahusu huyu Tundu Lissu atakaporudi nyumbani Tanzania. Kama kweli alikuwa msaliti, ni Mungu tu ajuaye na ni Mungu tu aliye hakimu wa haki.

Mheshimiwa sana, wewe ni Mkatoliki na pia mseminari, waijua vema hadithi ya mwana mpotevu na kondoo aliyepotea.

Tundu Lissu ni Mtanzania kama wewe, baba, kaka na mtoto wa familia Tanzania yetu wewe. Hotuba yako (Uchaguzi House) ya leo 22/07/2020 nimependa na iwe ya kweli kwa vitendo.

Tafadhali, chondechonde, akirudi huyo (Tundu Lissu) Jumatatu, muacheni arudi kwa style yake, afanye anayotaka kufanya bila kuvunja sheria. Hakuna haja ya kutunishiana misuri kwa sasa, muacheni aje, kama figusu, mfanyieni baada ya uchaguzi na sio sasa. Tutachafuka na kuchafuana sote, nyumba yetu sote (Tanzania) itanuka, mpeni Tundu Lissu ushirikiano, msaidieni atulie na baada ya uchaguzi ndio kesi zake ziendelee au figisu zozote.

Mheshimiwa sana Rais Magufuli, kama umesoma, umesomea au kutaarifiwa. Ni hayo tu yangu. Nyumba Tanzania ni yetu sote. Bila matusi au mkwaruzo tuwe kama nguchiro na Mchwa, nyumba moja bila mkwaruzano.

Ni hayo tu kwa leo. Ubarikiwe na Uongozwe kwa niaba aliye juu na amri ya uhai wako kwake.
 
Koma!
Ana harasa amtegemeaye mwanadamu mwenzie.
HAKUNA wa kumtegema mwanadamu mwenzie, sote tu mavumbi na mavumbini tutarudi- haina haja ya kutunishiana misuri iloihali sote twarudi mavumbini na JPJP hana cha kupoteza hata kama atakuwa Raisi wa awamu moja
 
Ni ujumbe muhimu ila kama kawaida unaweza kupuuzwa.

Mwenye macho na asome, mwenye masikio na asikie... we umefanya kwa sehemu yako.
 
HAKUNA wa kumtegema mwanadamu mwenzie, sote tu mavumbi na mavumbini tutarudi- haina haja ya kutunishiana misuri iloihali sote twarudi mavumbini na JPJP hana cha kupoteza hata kama atakuwa Raisi wa awamu moja
'hana cha kupoteza hata kama atakuwa Raisi wa awamu moja'.

Alishasema mwenyewe haoni nani wa kuendeleza miradi yake aliyoianzisha.
 
'hana cha kupoteza hata kama atakuwa Raisi wa awamu moja'.

Alishasema mwenyewe haoni nani wa kuendeleza miradi yake aliyoianzisha.
Miradi ni Miradi, hakuna wa kupambana na nguvu za Muumba hapa chini ya jua... tetemeko likija, miradi yote inakuwa mavumbi, act of nature cant be stopped mbele ya hiyio miradi na ni Mungu tu ajuaye mbele yetu kuna nini...

JPJP ni mtu wa Mungu, mwenye huruma ... na askiie kilio cha anao waongoza nikiwemo mimi... ushauri bila malipo .
 
Miradi ni Miradi, hakuna wa kupambana na nguvu za Muumba hapa chini ya jua... tetemeko likija, miradi yote inakuwa mavumbi, act of nature cant be stopped mbele ya hiyio miradi na ni Mungu tu ajuaye mbele yetu kuna nini...
JPJP ni mtu wa Mungu, mwenye huruma ... na askiie kilio cha anao waongoza nikiwemo mimi... ushauri bila malipo .
Kwamba mzee baba ni mtu wa Mungu na mwenye huruma sio?

Basi kilio chako atakisikia mkuu.
 
'hana cha kupoteza hata kama atakuwa Raisi wa awamu moja'.

Alishasema mwenyewe haoni nani wa kuendeleza miradi yake aliyoianzisha.
Lissu ni level ndogo kwa raisi kuhangaika naye, msafiri mmoja kurudi nyumbani haimsumbui rais. Waambie walio level ya kiprotokali na Mwananchi/raia Lissu.
Rais ana majukumu makubwa kushugulika na Lissu.
 
Uhalifu huwa hauhusiani na kutia nia.
Huwezi omba excuse kuwa kwa kuwa nagombea msinikamate kwa makosa niliyofanya kabla ya kutangaza nia hakuna.

Akikanyaga tu nchini ni segerea hakuna majadiliano ni yeye tu kujiandaa kisaikolojia
 
Lissu ni level ndogo kwa raisi kuhangaika naye, msafiri mmoja kurudi nyumbani haimsumbui rais. Waambie walio level ya kiprotokali na Mwananchi/raia Lissu.
Rais ana majukumu makubwa kushugulika na Lissu.
Najua wajua nguvu zake kama commander in chief na Raisi wa Jamhuri, ukiyajua hayo, utajua maana ya uzi huu...
 
Tutachafuka na kuchafuana sote, nyumba yetu sote (Tanzania) itanuka, mpeni Tundu Lissu ushirikiano, msaidieni atulie na baada ya uchaguzi ndio kesi zake ziendelee au figisu zozote.

.
Naona unatishia nyau kuwa tutachafuana tusipomuachia free!!! unamtishia raisi kama kinyago chako cha kumtisha!!!

Umesema akija asaidiwe atulie usipate shida akifika atapelekwa Segerea akatulie kule hadi uchaguzi upite ndipo kesi zake ziendelee.Hilo ombi linakubalika.Akitulia Segerea hadi uchaguzi ukishapita atakuwa katulia vya kutosha
 
Uhalifu huwa hauhusiani na kutia nia.
Huwezi omba excuse kuwa kwa kuwa nagombea msinikamate kwa makosa niliyofanya kabla ya kutangaza nia hakuna.

Akikanyaga tu nchini ni segerea hakuna majadiliano ni yeye tu kujiandaa kisaikolojia
Uhalifu Uhusiane AU USIHUSIANE na kutia nia; Akikanyaga au Asikanyage; ajiandae kisaikolojia au la, ni maoni yangu mimi pangu pakavu tia mchuzi... figusu afanyiwe baada ya uchaguzi... kuchafukiwa au kuchafuliwa wakati huu wa uchaguzi hatutaki kama wana familia wa nyumba yetu sote Tanzania
 
Wataanza kuyadhibiti mapokezi yake, uoga.

Mleta uzi umesema vizuri. Ngoja tutulie tuone.


Jesus is Lord!
 
Kweli ila akimuweka ndani ntaamini kuwa mzee magu muoga sana .
Sio woga no order ya mahakama.Mahakama na Raisi ni vitu tofauti na Chadema SIKU ZOTE HUWA HAMTAKI RAISI AINGILIE MAAMUZI YA BUNGE WALA mahakama.

La Lisu hataingilia kama alivyofanya kwa Kabendera pamoja na mama kabendera kuomba sanaaaaa.

Lisu ajiandae tu.Alivyoligema atalinywa
 
Back
Top Bottom