Uchaguzi 2020 Rais Magufuli "theoretically" ameutangazia Ulimwengu kuwa tutakuwa na chaguzi zilzo huru, lakini "practically" hatutakuwa na uchaguzi ulio huru!

Huu ni uamuzi mzuri lakini waimba mapambio ya kumsifu yesu mpya wataupinga.

Uchaguzi wa wabunge pia, mambo yakiwa yale ya kwenye primaries tunapotezeana muda tu.

Katika haki muda sio tatizo

Tujifunze kwa Nelson Mandela alipoteza muda lakini sio tu ili apate madaraka, sifa au heshima..
Lakini kwangu Mimi Ni Somo tosha kujua haki haiombwi Bali inatafutwa tena kwa namna yoyote akili na kwa nguvu kubwa ili kuweka usawa wa maisha ya baadae..
 
Nani anastahili kuhakikisha uchaguzi huru,ni anayesimamia uchaguzi ama mmoja wa wagombea?
 
Kitwa-Mulomoni
Ngoja nikuulize swali dogo tu......

Hivi lugha ya matusi inatafsiriwa na mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM?

Hivi unategemea tuwe na uchaguzi huru, huku mmoja wa wagombea, ambaye ndiye Rais aliyeko madarakani, ndiye anayeteua Mwenyekiti na wajumbe wake wote wa Tume ya uchaguzi?
 
Alikuwa anafurahisha umma na pia kutafutakupigiwa makofi.
Anajijua hajui sias na ndiyo maana kakataza siasa, hajui diplomasia na ndiyo maana alimwambia mwenzake anawashwa, ila jana kinafiki kamualika ukumbini.
 
Kama huo siyo mkakati wa CCM kufanya wizi wa kura, tunaweza kuita hiyo mbinu ya kutotoa nakala ya matokeo kuwa ina nia gani haswa?
Mfano mzuri.
Ni nani angalau amekwenda mahakamani kulikataa hili?

Hata kama mahakama watalikataa hili, si huo ni ushahidi kuwa juhudi zilifanyika kukataa mpango huo? Hadi sasa kimya!
 
Hufanya shauri kumwangusha tu katika cheo chake; Huufurahia uongo. Kwa kinywa chao hubariki; Kwa moyo wao hulaani.
They only consult to cast him down from his excellency: they delight in lies: they bless with their mouth, but they curse inwardly. Selah.
 
Hawa watawala wetu wanadhani kwa kuwabambikia kesi na kuwatesa wapinzani, ndiko kutawahakikishia kudumu madarakani?

Watawala wetu wanapaswa kujifunza kwa makaburu wa Afrika Kusini, ambao walimfanyia kila aina ya mateso, shujaa Nelson Mandela, ambaye hatimaye akaja kuwa ni mwafrika wa kwanza mweusi, kuwa Rais wa Afrika Kusini
 
Hii sijui ni uzi wa ngapi ukielezea suala la uchaguzi huru na wa haki. Hapa Afrika uchaguzi huru na haki ni pale uliyegombea unaposhinda au chama unachokishabikia kinaposhinda tu! Kwako CDM ikishinda ndiyo uchaguzi huru na wa haki la sivyo si huru na haki
 
wasiwasi wa nini nanyi mna wagombea watano tayari!
 
kolola
Tumeomba tuwe na Tume huru ya uchaguzi.......

Hivi unadhani ni kitu gani kinachowapa "kigugumizi" cha kuunda Tume huru ya uchaguzi, kama siyo watawala wetu wa CCM kutaka kuuvuga uchaguzi huo?

Hata Afrika Kusini iliendelea kuwapata viongozi waliochaguliwa weupe, hadi pale Tume ya uchaguzi huru ilipoundwa na kuweza kumpata kiongozi mzalendo mwafrika mweusi, shujaa Nelson Mandela
 
Mfano mzuri.
Ni nani angalau amekwenda mahakamani kulikataa hili?

Hata kama mahakama watalikataa hili, si huo ni ushahidi kuwa juhudi zilifanyika kukataa mpango huo? Hadi sasa kimya!

Kama wapo kimya ndio maana nakwambia huu Ni mikakati wa kuwa na siasa za maigizo na hizi chaguzi za maigizo...

Suluhu Ni kudai haki mahakamani hata Kama mahakama za nchini zitatoa hukumu batili lakini zipo mahakama za juu zaidi... Za kudai haki na ikapatika hata ikichelewa.

Na mkubumbuka Sana Rev. Mtikila(RIP) na hoja yake ya mgombea binafsi kwa ngazi zote za uchaguzi lakini hakuna Hadi leo mpinzani au raia aliyetetea na kudai Hilo Jambo...

Mkuu wakudai haya Ni wewe, Mimi na Yule kuanzia popote pale ulipo Hadi mahakamani..
 
kolola
Tumeomba tuwe na Tume huru ya uchaguzi.......

Hivi unadhani ni kitu gani kinachowapa "kigugumizi" cha kuunda Tume huru ya uchaguzi, kama siyo watawala wetu wa CCM kutaka kuuvuga uchaguzi huo?
Hakuna kitu kama hicho duniani period, pambana na hali yako
 
Na hapo ndipo ninaposhangaa kwa nini vyama vya upinzani vishiriki uchafuzi huo? Maana huo siyo uchaguzi. Huwezi kupinga matokeo ya urais mahakamani yakishatangazwa na tume, hapo unategemea nini? Hayo yote yamekuwepo ktk chaguzi zilizopita na sasa limeongezwa hili la nakala ya matokeo. Bado tu vyama vya upinzani vinakwenda kushiriki uchaguzi ambao wanajua hawatatendewa haki!?!?
Kama kuna mbunge wa upinzani atakayerudi bungeni kwa uchaguzi huu ujao itakuwa ni kwa hisani ya CCM tu, Na watahakikisha ni wale wasio na madhara kwao kisiasa. Tusubiri tuone.
 
Exactly

Hilo ndilo litakakotokea, kwa wenyewe watawala "kuwapa" ubunge wale inaowataka wao, wabunge wa NCCR Mageuzi na CUF.........

Vyama shiriki na CCM
 
Vipaumbele vya kujenga nchi vimeshindwa kuinasua nchi kutoka kwenye listi ya LDC (Least Developed Countries).

Hatudanganyiki na propaganda, kadanganye mambumbu wenzako.
Haya sasa mmeamka..😂
 
Ccm wakitoboa mwaka huu ntaamini kuwa wizi wa kura hupo.
 
Zuio mahakamani ndio suluhisho... Tukisubiri uchaguzi wa maigizo ndio tumeshakubari matokeo.... Maana matokeo ya uchaguzi kwa rais hayana rufaa Wala kudai haki mahakamani.
Mahakama ipo hiyo itaruhusu hilo zuio? Au ya nje ya nchi?
 
Mahakama ipo hiyo itaruhusu hilo zuio? Au ya nje ya nchi?

Zipo ngazi za kimahakama... Kumbuka wapo watu wanadai haki ya Zanzibar kujitenga.. na ipo siku watapata haki yao

Acha woga Mkuu, kuelimishana na kujua haki zako Ni Jambo la msingi na elewa kwamba haki ikishapitwa na wakati Ni nadra Sana kuipata...

Wasiwasi wako Ni kwamba Ni heri usidai haki kwa sababu utoipata elewa huo Ni unyonge na uzuzu...

Zipo taratibu za kufuata kisheria na haki ikapatikana....
 
Ccm wakitoboa mwaka huu ntaamini kuwa wizi wa kura hupo.

Hayo Ni maigizo ya siku zote...
Kama uchaguzi wa serikali za mitaa walishinda kwa 99%.. unategemea nn!!

Na wasiwasi na Hawa wapinzani inawezekana na wao Ni moja wa waigizaji wakisiasa....

Kususia uchaguzi wa serikali za mtaa na zile chaguzi ndogo za ubunge Ni UDHAIFU.... Kususia bunge na kutoka nje ule nao Ni UDHAIFU...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…