Rais Magufuli tunusuru vijana wako tunapitia kipindi kigumu

Rais Magufuli tunusuru vijana wako tunapitia kipindi kigumu

Honorable GPA

Senior Member
Joined
Mar 31, 2019
Posts
149
Reaction score
223
Just imagine upo katika kipindi cha majonzi una tafakari hili na lile baada ya kukosekana kwenye ajira! unaulizwa maswali kama haya na wazazi, ndugu na majirani;

Nasikia ajira zenu zimetoka. Vipi sasa umefanikisha? Unajibu sijafanikisha.
Anaendelea kuuliza, kwanini sasa au hukutuma maombi? Unajibu, maombi nilituma ila imetokea bahati mbaya sijafanikisha. Anauliza tena, mbona wengine wamepata wewe umekosaje? Unashindwa hata ujibu vipi hili swali ila kwakuwa umeulizwa unaamua kujibu kwamba mpangaji ni mwenyezi Mungu huenda hakuamua niwemo kipindi hiki alafu pia yale ni maombi kwahiyo kupata au kukosa ni sehemu ya matokeo.

Kiufupi tu! Ni kwamba ajira zinapotoka wazazi wetu wanaamini kwamba utapata. Sasa inapotokea kama hivi hujapata imani yao kwako inapungua wanaanza kufikiria labda ulifeli shule ila unaficha ndio mantiki ya kuulizwa maswali kama hayo!

Ukiachana na wazazi, jamii ndio kabisaa ukikosa ajira wanakuona si lolote si chochote. Just imagine mtu anakuuliza, umekosa ajira kwahiyo utaishije?

Wengine jinsi ajira hizi zinavyotoka wanaamini una ufaulu mdogo ndio maana umeachwa. Wengine wanasema badala ya kwenda chuo kusoma wewe ulienda kuendekeza umalaya matokeo yake chuo ulifeli ona sasa wenzako wameajiriwa wewe upo upo tu!

In fact vijana tunapitia kipindi kigumu sana. Kudharaulika kwingi, kuseng'enywa kwa sana, kusimangwa ndio usiseme.

Tunaomba mheshimiwa Rais utunusuru na masimango haya. Pamoja na kazi kubwa unayoifanya ya kulipeleka taifa letu mbele pia tukumbuke na sisi vijana wako tunanyanyasika sana mitaani!. Kwenye ajira 13000 ulizosema ni 8000 tu zimetoka, sema japo neno ili 5000 zilizosalia nazo zitoke angalau zitasaidia kupunguza idadi ya vijana wengine mtaani.
 
Mkuu mimi saizi silembi

Kuna siku mzee nilimpa makavu, yeye ni mwanachama wa CCM, nilimchana live bila kujali nitalala wapi akinifukuza!

Alikuwa anauliza maswali Kama hayo, na mimi niko na hasira, baada ya kuona majina ya hovyo ya kujirudia rudia tamisemi .!

Mzee alihisi nimechanganyikiwa ikabidi atulie tu!
 
Hakika umesema ukweli mkuu
Sasa hivi mama ananiambia "naona awamu ya pili utakuwemo mwanangu", yaani wazazi wanaamini ni rahisi, lakini ukweli tunaujua sisi wenyewe wahusika

Hongera kwa kusema bayana[emoji122]
 
Pole sana mkuu pole haya maisha yana hatua huwenda tambo yako haijafika.
 
Tuvilaumu vyuo vyetu kwa kuzalisha matatizo. Vyuo vinajua kabisa kuwa baada ya nchi kuingia kwenye SAP serikali ilijitoa kuwa mwajiri mkuu. Wao badala ya kudahili wanafunzi kwenye program zisizolazimisha ajira serikalini kila siku wanaongeza udahili kwenye kozi hizo hizo. Vyuo vikuu vilazimishwe kubuni program zinazofaa kwa vijana wetu kulingana na mahitaji ya sasa. Program za ualimu zipunguziwe wanafunzi.
 
Wazazi wanachoamini utadhani chuo mlikuwa kumi basi, kumbe kada tu ya ualimu ngazi zote (certificate, diploma na degree) mwaka mmoja tu mnamaliza zaidi ya 60k, sasa imagine miaka imepita mitano no ajira zidisha mara 60k graduates for the average unapata wanafunzi kwenye 300k+ wapo kitaa, halafu mtu anaajiri 13k🤣🤣🤣, mimi nimekimbia maswali ya wazazi nipo huku Sumbawanga sijui hata cha kufanya sina hata mia, nawaza niuze hii simu nipate ata mtaji wa karanga😢😢😢
 
Pole sana kwa unayopitia wewe na wengine wengi. Ajira limekua tatizo kubwa sana Tanzania na hata duniani.
 
Tuvilaumu vyuo vyetu kwa kuzalisha matatitizo. Vyuo vinajua kabisa kuwa baada ya nchi kuingia kwenye SAP serikali ilijitoa kuwa mwajiri mkuu. Wao badala ya kudahili wanafunzi kwenye program zisizolazimisha ajira serikalini kila siku wanaongeza udahili kwenye kozi hizo hizo. Vyuo vikuu vilazimishwe kubuni program zinazofaa kwa vijana wetu kulingana na mahitaji ya sasa. Program za ualimu zipunguziwe wanafunzi.
Msiombe watazifuta wakiona hazilipi
 
Na kundi hili la vijana asilimia kubwa ukiwaeleza uwepo wa Mungu mtapigana!
Ajira inaletwa na mungu. Kwani kuna kiumbe kisicho na mungu. Ndege wana miungu na wanaishi pia
 
Imeniuma sana Hii story,
Kwakuwa Muumba, ajapiga kipenga Cha mwisho, Bado tunapumua, tuchakarike tu, kwa kile nachoweza nikiona fursa, nitakuwa naweka hapa jamvini.

Umeongea maneno mazito, kile kinachoendelea kwenye mioyo ya vijana wengi, umekiweka ktk maneno/maandishi.
 
Back
Top Bottom