Rais Magufuli, ulipotaja kuwa umezalisha ajira milioni 6 huoni kuwa unanidanganya hata mimi?

Rais Magufuli, ulipotaja kuwa umezalisha ajira milioni 6 huoni kuwa unanidanganya hata mimi?

Rais wangu, hivi unajua kuwa pamoja na kukupinga sana ila ni miongoni mwa watendaji wako wasaidizi wakuu ndani ya serikali? Kwa taarifa yako ninasimamia moja ya taasisi ambazo kwa siku za hivi karibuni umeelekeza macho yako yote pale. Nipo na vijana wako unaowatuma kila siku na mambo yanaenda vizuri sana kwao chini ya usimamizi wangu usiofuata mkumbo wala ulambaji viatu. Pale ofisi ya msajili mkuu wa Hazina ni nyumbani kwangu na tunafanya vikao kila mara.

Twende kwenye mada.

Unajua kuwa mimi ni mwenyeji mkubwa pale Hazina? Unajua kuwa naelewa madudu yote uliyofanya dhidi ya sekta binafsi kuanzia mwaka 2016 mpaka jana? Unajua kuwa ninazo taarifa za uhakika kuwa kwa utaifishaji holela na uvurugaji wa mipango uliofanya nchi nzima umegharimu ajira za watu siyo chini ya elfu 50?

Naomba nikueleze kuwa siyo kila msaidizi wako anafurahishwa na jinsi unavyoendesha nchi! Naomba kwa leo niishie hapo ila nyongo ikizidi itatoka!

Tukutane Dodoma kesho kwenye ripoti muhimu uliyotutuma kuifanyia kazi Dar!
Mkuu andiko lako sijapenda kwa nini umeamua kuandika haya leo na juzi ,hii pana sijaipenda kama mkuu anakufaham vizuri na mnafamiana why ulete hapa kwa nini usimfuate ukamnongoneza
 
Hivyo ndiyo viwanda vyetu
Tukitumia scale ya cherehani nne ni kiwanda jiwe atakuwa yuko sahihi, ukiona majiko manne ya kuchoma chips mtaani kwako hicho ni kiwanda cha kutengeneza kihepe, kaya nne zenye friji hicho nacho ni kiwanda cha kutengeneza barafu, ukiwa na blenda nne hicho nacho ni kiwanda cha juisi, kwa hiyo Mzee yuko sahihi kabisa nami nakubali
 
Mkuu andiko lako sijapenda kwa nini umeamua kuandika haya leo na juzi ,hii pana sijaipenda kama mkuu anakufaham vizuri na mnafamiana why ulete hapa kwa nini usimfuate ukamnongoneza

Ukweli huwekwa hadharani maana hataki ushauri.
 
Kusema kweli, yaliyosomwa kwenye Hotuba yangekuwa yamefanyika kweli, watanzania Leo tungekuwa tunafurahia. Binafsi huwa sielewi hizo data wazee wanazitoa wapi au chief cooker anahusika.
Anyway, amalize tuu aondoke.
Bahati nzuri sana watanzania wote wanajua uhovyo wa serikali hii. HAKUNA CHA KUWADANGANYA

ajira 6M. 😄😄
 
Bahati nzuri sana watanzania wote wanajua uhovyo wa serikali hii. HAKUNA CHA KUWADANGANYA

ajira 6M. 😄😄
Wakiajiri watu wote hao tusingelala kwa matarumbeta ya wasifiaji kama kwenye Corona kulivyotungwa mistari.Hakuna hizo ajira Bali anafurahisha genge.
Alisema akimaliza uhakiki anapandisha mishahara hadi leo hakuna.Sifa za Jukwaani zinazoambatana na stress.
 
Kataifisha fedha za wafanyabiashasha maduka ya ubadilishaji fedha, nk
Uthibitishie umma kuwa magu kateta uongo..?
Hata ukiweza kututhibitishia hapohapo jiulize swali hili "kwanini watu wanachepuka"
Ukijijibu hilo then fatilia mfumo tulioiga wa siasa unaendeshwaje hapo hautapata tabu kujisumbua!

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
 
S
Ukweli huwekwa hadharani maana hataki ushauri.
Sawa Mkuu ,sikatai lakini huoni mtoa mada au mada imekaa kinafiki,namanisha kwa nini hakuyasema haya hata mwezi mmoja kabla kasubili mpaka bunge limevunjwa ndo anayasema? Lakini kama si unafiki kwa nini kuendelea fanya kazi na mtu ambae hukubaliani nae ,why usiachie nafasi unayoitumikia ili kujitenga na dhambi iyo maana ata ukifa njaa bado hutaonekana shujaa kuliko kujificha nyuma ya kibodi huku bado unaendelea lipwa na posho za kusafili na huyo huyo ambaye amempa za uso .
Mwisho kama kweli ameona kuna tatizo na kiongozi husika alie mtaja ok anatusaidiaje?
 
-Mwenendo wa AJIRA sekta binafsi/waliojiajiri;
2013/14 - 408,756
2014/15 - 257,323
2015/16 - 195,002
2016/17 - 239,017
2017/18 - 137,054

IMG_20200617_071124.jpg

-Serikali iliajiri only 1.1% ya walioiomba kazi toka Nov 2015-Dec 2018, sawa na mtu 1 kati ya 100
 
Barakoa ,wanauza mitaani

Sent using Jamii Forums mobile app
Zamani nilikuwa nikiwadharau mama ntilie, nilipokuja kufanya utafiti wa kipato chao cha siku ns kushuhuda maendeleo yao ilijikuta najutia maono yangu. Ujinga wetu ni kutojua kuona fulsa, unakuja situkia barakoa zimebadili maisha ya watu. Ndipo unaanza kumkumbuka marehemu Ruge😂😂
 
Rais wangu, hivi unajua kuwa pamoja na kukupinga sana ila ni miongoni mwa watendaji wako wasaidizi wakuu ndani ya serikali? Kwa taarifa yako ninasimamia moja ya taasisi ambazo kwa siku za hivi karibuni umeelekeza macho yako yote pale. Nipo na vijana wako unaowatuma kila siku na mambo yanaenda vizuri sana kwao chini ya usimamizi wangu usiofuata mkumbo wala ulambaji viatu. Pale ofisi ya msajili mkuu wa Hazina ni nyumbani kwangu na tunafanya vikao kila mara.

Twende kwenye mada.

Unajua kuwa mimi ni mwenyeji mkubwa pale Hazina? Unajua kuwa naelewa madudu yote uliyofanya dhidi ya sekta binafsi kuanzia mwaka 2016 mpaka jana? Unajua kuwa ninazo taarifa za uhakika kuwa kwa utaifishaji holela na uvurugaji wa mipango uliofanya nchi nzima umegharimu ajira za watu siyo chini ya elfu 50?

Naomba nikueleze kuwa siyo kila msaidizi wako anafurahishwa na jinsi unavyoendesha nchi! Naomba kwa leo niishie hapo ila nyongo ikizidi itatoka!

Tukutane Dodoma kesho kwenye ripoti muhimu uliyotutuma kuifanyia kazi Dar!
Binamu kulikoni tena binadamu!!! Bado nakupenda binadamu
 
Bahati nzuri nilishajiapisha kuwa kamwe sitosikiliza hotuba za Jiwe baada ya kugundua huwa kuna chai birika zina,sukari kijiko kimoja.

Mnajitakia wenyewe kumsikiliza,msilie.

Sent from my Redmi Note 5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom