Rais Magufuli wewe ni Rais wetu sisi sote Watanzania. IGP Sirro hafai ukiapishwa teua IGP mwingine

Rais Magufuli wewe ni Rais wetu sisi sote Watanzania. IGP Sirro hafai ukiapishwa teua IGP mwingine

Ni kweli askari wa TZ, Wana kazi kubwa sana ya kuwalinda wananchi hasa watawala lakini mbona maisha yao hamyajari kabisa, kwani ukipita kwenye vibanda vyao wanavyoishi, huwezi amini kabisa! Zamani walikuwa hawalipii umeme kabisa, lakini sasa hivi kila mtu na mita yake! Daaa, na awamu hii waliokuwa wana wasemea japo kidogo huko bungeni ndio, hivyo tena! Wamebakia yatima!! Japo walikuwa wana jiriwaza na pombe za nusu bei kwenye makambi yao, awamu hii hakuna! Ila wanatumikaa!
Maisha ya askari wa Tanzania yanaendana na mazingira ya Mtanzania, wote sisi tunaishi hivyo kama askari wetu pia, ...

Unaona kuwa ni sawa?
Unajua maisha ya wale wanaowatuma?
Maisha ya ma IGP wao ,marpc wao na viongozi wao wengine ambao kiuhalisia wanayoyafanya ni kulinda maslahi yao na si vinginevyo?

Je, mali wanazomiliki viongozi wa serikali na wale wa polisi zinatokana na vipato halali au ndio wale wa kufanya manunuzi hewa na kujichotea mabilioni ya pesa ? Shukrani yao kwa serikali ya CCM inayoendana na matendo yao ya wizi ni kuwadhibiti wapinzani kwa nguvu zote ili uovu wao nao ulindwe?

Kama Serikali ya awamu hii ipo siriasi kupambana na rushwa basi ianze na wale waliopigana kifa na kupona kufanya uhalifu wa kuwapa CCM ushindi wa asilimia 95 + wa ubunge na madiwani.

CCM na viongozi wa Dola wametumia watoto wa maskini walioko kwenye vyombo vya Dola kuwatesa maskini wenzao ili hali wao wanajua wazi kuwa kuwaua watanzania wenzao kwa sababu tu wanagombea uongozi kwa kura ni kosa.

Wanacholinda ni maslahi yao mana Wote ni Watanzania lakini wanachofanyiwa wapinzani utafikiri ni Wasomali wamevamia Tanzania . Kwa nini nguvu kubwa itumike kuwazuia watanzania kupata hata udiwani kwa sababu tu ya vyama? Jibu ni rushwa na maslahi yao yasije yakamulikwa na zimwi lisilokujua
 
Binadamu tutasahau kishatendewa mema tutasahau kila kitu ndio faida ya bonadamu. MABAYA HAYO HAYATATOKEA NCHINI KWETU KATIKA JINA LA MUNGU MWENYE REHEMA.... Usiombee mabaya nchi yetu MANENO YAKO YASIFANIKIWE NA YAKAFUTILIKIE BAHARI na TZ ITAENDELEA KUWA YA AMANI. BILA COVID 19
Kwa asili mabaya ndiyo yanayoleta usawa na amani zaidi.

Unajua hata Korona imesaidia sana nchi za Afrika kuheshimiwa baada ya wazungu kufa wengi kuliko Afrika.
Walitegemea waafrika wafe zaidi lakini Mungu muumba hakupanga hivyo.
Hata vita za silaha Kali zimesimama kwa muda wa korona.
Sio kila baya linakuja kujenga ubaya.
MTU aliyezoea kubaka wanawake ukisikia ameshikwa na kisukari na kupoteza nguvu basi watu watamshukuru Mungu.

Ndio maana Mungu aliyewaumba watu aliruhusu washughulikiwe wanapotenda mabaya. Muuaji alipewa hukumu take,mwizi naye pia n.k. Kwa hiyo haitafaa kamwe kwa mtu maskini yeye ndugu zake wauawe kwa maagizo ya matajiri waliojificha kwenye utawala halafu wao wawe salama muda wote. Asili haipo hivyo.

Hitler alipokua anapita mitaani amezungukwa na majeshi imara kabisa hakuwahi kuwaza kuwa atakuja kukimbia na kujificha kusikojulikana akikimbia wababe wasiowaza madaraka wala vyeo bali kuikomboa jamii.

Dawa ya yote ni kutubu kwa mabaya yanapofanyika na kuhakikisha hayafanyiki tena. Lakini kama CCM itakaa kimya na kujifariji kuwa watatumia Risasi kuendelea kuwazuia wengine wasipate kura halali na kupata hata uenyekiti wa mtaa hawataleta mwisho mwema . Amani hawataifurahia vizuri zaidi ya kuishi kwa hofu
 
Kwa Sheria za Tanzania hakuna haki ya Raia kuuwawa tena asiye na hatia eti kwa sababu tu ana interest na chama kingne, na upinzani sio Uadui kama inavyotazamwa kwasasa kwahiyo usihalalishe mauaji ya watu tena kwasababu nyepesi kama hiyo
 
Unachofanya mleta mada ni kumshauri kijana wa boda boda aliyempa mimba mwanafunzi wa kike kwamba yule binti ndio anamuharibu huyu dereva bodaboda
 
Sufurahii kuuwawa kwa ndugu zangu wa Pemba maana hata mimi ndo nilikotokea ingawa chama changu cha kijani... Lakini tusiangalie upande mmoja tuwe tunaangalia na upande mwingine... Nyumbani nakujua mwenyewe jinsi tunavoishi hakujawahi kuwa salama siku za uchaguzi hata kidogo. Nakumbuka kipindi mimi bado mdogo nilinyimwa kuuziwa fenesi kisa babangu ni CCM.

Na kila mwana CCM alikua hauziwi kitu kitendo kile kiliniuma hadi leo maana niliona ni ujinga wa kiwango cha lami. Nina watani zangu huwa nawaambia yoyote atakaekwenda kuandamana wakati serikali imekataza basi kama nitakabiziwa smg naanza na wao ili sadaka ianze nyumbani.
 
Ni kweli askari wa TZ, Wana kazi kubwa sana ya kuwalinda wananchi hasa watawala lakini mbona maisha yao hamyajari kabisa, kwani ukipita kwenye vibanda vyao wanavyoishi, huwezi amini kabisa! Zamani walikuwa hawalipii umeme kabisa, lakini sasa hivi kila mtu na mita yake! Daaa, na awamu hii waliokuwa wana wasemea japo kidogo huko bungeni ndio, hivyo tena! Wamebakia yatima!! Japo walikuwa wana jiriwaza na pombe za nusu bei kwenye makambi yao, awamu hii hakuna! Ila wanatumikaa!
Kati ya viumbe ambao hupaswi wahurumia ni pamoja na Askari wa Tanzania....
 
Mlitaka mfanye fujo kuvunja amani nchini, awaangalie tu?

Upinzani nyie baadae museme IGP hajui kazi mutulie na maumivu ya kushindwa uchaguzi.
IGP Sirro yupo na atazidi kuwepo ili awanyooshe nyie wataka uza nchi yetu.
Mutulie tuishi kwa Amani Dodoma leo upinzani macho yote huko huwa mnamfatilia JPM kupita wanachama wake... eeeeh.. NDIO HIVYO.. TANO TENAAAAAAAAA.. [emoji172] [emoji169] [emoji172] [emoji169]
 
Usilolijua ni kwamba Sirro kafanya hayo kwa kutumwa na huyohuyo unayemtaka amuwajibishe!!.
 
Huyo unae muomba amuondoe IGP Sirro si ndio aliomtuma kufanya kazi hio huko Zanzibar. Kesi ya nyani unampelekea Nyani.

Tusali, Tufunge na Tumuombe Mungu tu "laana/fedheha/adhabu/mateso/maradhi" yawafikie kila alietoa maelekezo, aliesababisha, aliehusika na aliefurahia kuuliwa kwa watu wasio na hatia.
Umenikumbusha aliwahi kusema " I could be an IGP" hawa wanakwaya wangekuja kumwimbia Gwajima hizo nyimbo huko huko lock up.
 
Huyo unae muomba amuondoe IGP Sirro si ndio aliomtuma kufanya kazi hio huko Zanzibar. Kesi ya nyani unampelekea Nyani.

Tusali, Tufunge na Tumuombe Mungu tu "laana/fedheha/adhabu/mateso/maradhi" yawafikie kila alietoa maelekezo, aliesababisha, aliehusika na aliefurahia kuuliwa kwa watu wasio na hatia.
Umemaliza mkuu.
 
Kati ya viumbe ambao hupaswi wahurumia ni pamoja na Askari wa Tanzania....
Wale ni kama NDOMU TU!!! wana tumika pale wanapoonekana wana umuhimu wa kuwa Linda hao!! mtu, baada ya hapo ni kutupwa tu!!
 
Hivi mnavyolalamika ndivyo mwenzenu anapenda mlalamike
 
Back
Top Bottom