Rais Mobotu alimtumia Nguli wa Muziki Franco Luambo Luanzo Makiadi katika kampeni za kuwania Urais wa Zaïre

Rais Mobotu alimtumia Nguli wa Muziki Franco Luambo Luanzo Makiadi katika kampeni za kuwania Urais wa Zaïre

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Inaelezwa kuwa huu ni moja ya wimbo mkubwa zaidi wa kueneza propaganda iliyowahi kutengenezwa Afrika na Duniani kwa ujumla. Wimbo huu uliimbwa na Mwanamuziki Nguli wa Muziki wa Rhumba kutoka nchini Zaire(DR Congo kwa sasa), Franco Luambo Luanzo Makiadi mnamo 1984 wakati wa vuguvugu la uchaguzi wa Urais wa Zaire.

Mobutu alikuwa ndiye mgombea pekee na uchaguzi huo ulikua na aina mbili tu ya kura ya "ndio" au "hapana". Kulingana na matokeo rasmi, 99% walipiga Ndio kwa Mobutu.

Ingawa Mobutu alikuwa ndiye mgombea pekee, laikini inaelezwa kuwa alipiga kampeni kali nchini kote akipeleka ujumbe wake katika ukingo wa kwanza wa nchi na wa mwisho. Na wimbo huu ulikuwa nguzo yake muhimu ya propaganda.

Wmbo huu una takribani dakika 19 hata albamu ya wimbo huu ilipotolewa, wimbo ulirudiwa kwa pande zote A na Upande B.

Ulisambazwa bure kwa Wazaire wote. Kava ya albamu haikuwa na jina la Franco lakini wimbo ulipewa sifa.


 
Alikuwa mgombea peke wa kiti cha u Rais na wanamuziki mashughuri walitunga nyimbo za kampeni.

Baadhi ya maudhui ya wimbo wa Luambo ni:
Mgombea wetu ni Mobutu, tunamchagua Mobutu, Rais wetu ni Mobutu.
Hakuna mwenye uchungu na Zaïre kama Mobutu. Nyinyi mnaosafiri kwa mabasi na matreni, kwa ndege na kwa meli sisi tunamchagua Mobutu.
Wqchezaji, wafanyabiaahara, wakulima, sisi tunamchagua Mobutu.
 
Wimbo mzuri, tatizo mlengwa(message).Wa zaire kuimba wanajua, na walianza siku nyingi sana.

Funzo:Kila kitu kinapita katika hii dunia.
 
NI HIVII...


Sio siri huu wimbo huwa unanishangaza sana:

kidogo kuhusu tafsiri ya huu wimbo ni kwamba:

- Franco aliuimba baada ya kumkosea Rais Mubutu Sesessecko kwa kutandika chini zulia (kama red carpet) yenye rangi sawa kabisa na suti ya Rais Mobutu, kisha wanabendi wake wakasimama juu ya zulia hilo wakati wa perfomance yao stejini, hiyo ilimuuma sana Rais Mubutu akichukulia kuwa wamefanya makusudi kumdharau, kumkanyaga.

Mobutu akiamuru Franco akamatwe na kufungwa, Franco akakimbilia Ubelgiji, maisha yakawa magumu huko, mziki umebuma wakati wa kampeni ya urais akarudi Zaire na alianza kutunga huo wimbo wa kumsifia sanaa Mobutu Sesesecko na katika tungo zake anasema:

- Rais wetu ni Mobutu, Zaire yote ifahamu hilo

-Wazee kwa Vijana, Wababa kwa Wamama tumchague Mtukufu Mubutu peke yake, nani kama Mubutu???

-Watoto wote mashuleni, tunajua kuwa hampaswi kupiga kura lakini tunawatuma kwa wazazi wenu, waambieni tumekubaliana kumpigia kura Mobutu Sesesecko,

-Pia kuna mahala anasema Mubutu ni chaguo la Mungu kwa Wanazaire.

Hayo maneno yalimkosha sana Rais Mobutu Sesesecko na akamnunulia Franco Vifaa vya mziki vya gharama kubwa sana kutokea Ufaransa, na akamtumia Franco Luambo Makiadi katika kampeni zake zote Zaire.

Vyombo hivyo vya mziki Franco alikuja navyo Arusha-Tanzania na kuperform live uwanja wa Sheikh Amr Abeid.
 
Jiwe ni zaidi ya mobutu....

cc: Jamhuri ya watu wa chato
 
Tunakumbuka historia tu
Afrika Afrika Eheeee...
tapatalk_1560572585463.jpg
 
Mobutu kawatumia sana wanamuziki wa nchi yake kueneza sifa na propaganda zake.

Hii mbinu inatumiwa sana na madikteta wengi sio mobutu tu.

Huu wimbo candidat na biso mobutu ni moja ya nyimbo kali sana, binafsi naikubali sana.
 
Alikuwa mgombea peke wa kiti cha u Rais na wanamuziki mashughuri walitunga nyimbo za kampeni.

Baadhi ya maudhui ya wimbo wa Luambo ni:
Mgombea wetu ni Mobutu, tunamchagua Mobutu, Rais wetu ni Mobutu.
Hakuna mwenye uchungu na Zaïre kama Mobutu. Nyinyi mnaosafiri kwa mabasi na matreni, kwa ndege na kwa meli sisi tunamchagua Mobutu.
Wqchezaji, wafanyabiaahara, wakulima, sisi tunamchagua Mobutu.
Unajua kabla ya hizo nyimbo za kumsifu Luambo alikuwa akiimba nyimbo za Kumponda Mabutu hadi akawekwa Lupango alivyotolewa akapelekwa Ikulu na kufanyiwa sherehe hapo akaqnza kutunga nyimbo za kumsifia!!!
 
Sky Eclat Mh. Rais alikukosea nini mbona una mpinga sana...
 
Unajua kabla ya hizo nyimbo za kumsifu Luambo alikuwa akiimba nyimbo za Kumponda Mabutu hadi akawekwa Lupango alivyotolewa akapelekwa Ikulu na kufanyiwa sherehe hapo akaqnza kutunga nyimbo za kumsifia!!!
Naam,mojawapo ya nyimbo alizomponda Mobutu Ni Ile ya Helena, République du Zaïre
 
Back
Top Bottom