Rais Mteule Barack H. Obama!

Rais Mteule Barack H. Obama!

Huu ni ujinga wa hali ya juu. Ni kujidhalilisha kusio na mfano. Laiti Bush angelikuwa na akili ya kufanya hili kwa wamarekani kutoenda kazini kesho basi ni wazi wamarekani wangelisahau mafyongo yake yote.....

Walioko DC na watakuwepo kesho ama siku ya OBAMA kuingia hapo naomba tuwasiliane kwa PM.

Tanzanianjema

Acha wafurahi!Kwani Watanzania-Bara wanapopumzika Karume Day inakuwaje?
 
Obama ndio chaguo la Mungu....lakini nawatahadharisha kwamba msitegemee mambo mengi sana, ni mapema mno!
 
Acha wafurahie! Acha wasifanye kazi kesho! Ni mara ngapi sisi waafrika tuna kitu cha kufurahia? Baada ya kusheherekea tuanze kazi ya kuthibitishia ulimwengu kuwa wakati wetu umewadia.
Mungu ambariki Obama! Mungu aibariki Afrika!

Amandla...........
 
nililengwa na chozi pale ilipotimu saa moja kamili saa za afrika mashariki, walipotangaza kuwa Obama amechukua majimbo ya california na mengineyo kukamilisha idadi inayotakiwa ya kura za majimbo, nilijisikia bahati sana na bado najisikia bahati sana kuishi wakati historia inawekwa, kwa hilo tu naomba niseme ndilo lilonifanya niwe emotional, the rest i dont care, its great to live in that moment, kama ambavyo nilijisikia kuwa na bahati kushuhudia kifo, mazishi ya Nyerere na papa John Paul 2, na kuchaguliwa papa mpya Benedict, that feeling u get haiji kila siku.......naomba niseme tena najisikia furaha ya ajabu kuishi katika kipindi ambacho historia kubwa kubwa zinaandikwa si kwa Obama tu, ila hata Hamilton aliposhinda ubingwa wa formula one, kama nikiishi muda wa kutosha kupata wajukuu nitakuwa na mambo mengi ya kuwasimulia.
 
lakini alitia huruma na kuna wakati alionekana anawaza sana pale alipomshika mama yake Michele kwa sababu yaani mama, Baba, babu na Bibi ndio woote hawapo. (I wish bibi yake ange-hang on mpaka leoo.)
 
Furaha ya watu Weusi, mimi nikiwa mmoja wapo ni kule kuushinda Unyonge uliojengwa ndani yetu, ule wa Nyani wa Ngabu kusema ndivyo tulivyo, unyonge wa kuonekana kuwa hatuna thamani wala uwezo wowote.

Ushindi wa Obama si kwa watu Weusi na Waafrika tuu, bali ni kwa kila mtu ambaye siku zote amelelewa na kukuwa katika mazingira yanayomwambia kuwa yeye ni batili, nusu na hana thamani.

Ushindi wa Obama ni sawa na kuvunja minyororo ya utumwa na ukoloni. Pamoja na kuwa ni kweli kuwa si yeye pekee ambaye ataongoza nchi ya Marekani, lakini kitendo cha yeye kuwashinda wale ambao siku zote wamekuwa wakidharau na kukandamiza binadamu wa rangi, dini, jinsia na aina nyingine kwa kujifanya wao ndio wateule, ni dalili tosha kuwa nyakati zinabadilika na kila tunaloambiwa haliwezekani, linawezekana.
Acha undumilakutatu! Kila unapopata nafasi ya kukanyaga race yangu kwa madai kwamba haina thamani unairukia kwa kila aina ya kejeli, kashfa na matusi kuonyesha imekosa utashi wa kuitwa ya watu.

Posted by Rev. Kishoka:
``Mjaluo wetu anachechemea, yuko hoi bin taaban, kathibitisha maneno ya Nyani "ndivyo Tulivyo" ngoja nikamdai refund ya mchango wangu kama Kikwete na BAE! ´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´visa hivi vinaelemea sana kumuonyesha kuwa kauli ya "Ndivyo Tulivyo" ina uhalali!

Posted by Rev. Kishoka:
´´Siku moja, Mwafrika, Mwarabu, Mwasia na Mzungu walikuwa kijiweni, Mungu akaja akawaambia nina vitu vinne inabidi niwagawie, kubalianeni nani anataka nini. Vitu hivyo vilikuwa ni Utajiri, Maarifa, Biashara na Ngoma. Mzungu akadamka, mimi nataka Akili...

Mwafrika akakimbilia ngoma yake akaikumbatia akaanza kutumbuiza huku Mzungu akitafakari nini cha kufanya, Mwarabu akiufurahia utajiri wake na Mwasia akipanga mipango ya biashara!
Mpaka leo tumeendela kukumbatia Ngoma na ndio maana tu mahiri kwenye sanaa!
... ni ile laana ya mtoto wa Nuhu (aliyejenga safina)aliyemcheka baba yake kuwa uchi baada ya kulewa. Mchungaji akatuambia kuwa uzao wa yule mtoto aliyelaaniwa ndio chimbuko la Waafrika na sisi ni watu tuliolaaniwa kuwa watumwa na watumishi wa wenzetu! ´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´Nyani Ngabu kasema, Ndivyo tulivyo, kauli mbiu hiyo inaelekea kuwa ni kweli kila siku!´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´Saidia Maskini, saidia baba! Ndivyo Tulivyo!´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´Nyani,
Tulishapigwa Limbwata na Mkoloni kuwa sisi ni Uzao wa Kaanani, mtoto wa Ham ambaye alipewa laana ya milele na Babu yake Nuhu kuwa tutakuwa watumwa!...ni laana hizo ndio maana tuna nywele Kipilipili!´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´Wee Nyani, mbona huachi ujinga😉 Yaani you made me believe for a minute Ndivyo Tulivyo!´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´The fact that we are allowing all these foreign companies to come and operate in Tanzania and provide them with "healthy" accomodations such as 5-10 years Income and Tax Break, in addition to other "incentives" to plush the red carpet fibre so they can walk like emperors to rescue Tanzania from its own failures, is enough to acknowledge that Ndivyo Tulivyo na ni Wajinga waliwao! ´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´Nyani,
Ndivyo tulivyo.
Tunashindwa kufanya self examination ya mioyo yetu na kuanza kujituma na tunakimbilia misaada maana ndio njia fupi kwa kuwa hatutaki kufanya kazi kwa bidii na kujituma ili tukishachuma juani, tule kivulini.´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´You are being too dismissive without even making a single effort to try if option presented at the table could work. Huu ndio what Nyani Ngabu calls "ndivyo tulivyo"! ´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´Tumechoka kusubiri na kukumbushwa na Nyani Ngabu kuwa ndivyo tulivyo, tunaanza wote kushiriki katika ujenzi wa Taifa kwa hali, mali na fikra.´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´yes ndivyo tulivyo!´´

Posted by Rev. Kishoka:
´´Swali ni lini tutaacha kulaumu na kuishi kama "ndivyo tulivyo" na kuleta mabadiliko? je wewe uko tayari kuanza mabadiliko ambayo Nyani anayadai kama Tomaso ndipo aamini kwa kuanza badili mwenendo wako wa kuonekana "ndivyo ulivyo"?´´

Rev. Kishoka, unapataje balls za kuiambia race yangu "ndio maana tuna nywele kipilipili"?
 
Bado sina cha kujivunia. Sijamwona mtu mwenye asili ya Tanzania huko Ulaya/Marekani akipata mafanikio ya maana kimichezo/kisiasa/kitaaluma kama walivyo wenzetu hapa jirani Kenya. Na hili tuwatupie lawama akina Mwalimu na TANU/CCM yao?
 
Wapo ni wewe huwajui tu! Uliza Joachim Manyara pale France alikuwa nani. Utaambiwa,,,,
Hayo tuyaache kubwa ni pale Mzee Mzima Rev. Jesse alipomwaga chozi,,, ana raha kuliko,,,, Raha.com
 
Mchungaji Jesse ana wivu mbaya. Mara kadhaa amenaswa akimbananga Rais Mteule BHO.
Mzee huyu pamoja na kuwa "mchungaji", ni mnafiki wa kutupa! Nifahamishe Mkuu, Manyara kafanikisha lipi tujivunie?
 
Obama...Obama...leo nachinja mbuzi ..ohh Obama..!!!!Nakuimbia Obama...nakuwa na hope na wewe Obama...Dunia hii inabadilika ..sababu yako Obama...jina lako linaangaza dunia nzima ehhh Obama....Kagelo inajulikana sasa ..kulioko Nyambiti..asante Obama....
 
Huo ushindi hautarajiwi. I don't care what the pundits say. We are going to defy them tomorrow. McCain is going to win this damn thing

sorry ni msiba mkubwa umekupata imeandikwa kwamba kuna wakati utafika Mtumwa atamtawala Mtwana wake
 
At a speech Nyerere gave on his visit to the White House in 1977, at the invitation of President Carter, Nyerere remarked:

"We in Tanzania, Mr. President, and in Africa generally, follow American politics with close attention. There is the intrinsic interest of the affairs of the most powerful nation the world has ever known. But more to the point, your politics do affect us. Indeed, we in Tanzania sometimes think that the world should somehow join in the process of electing the American President--[laughter]--for though we realize that the American people do not elect an absolute monarch, the world power structure is such that other peoples in other nations have a vital interest in the person whom the American people choose as their executive head of state."

There you have it. Will the Vatican consider a statement like this while they consider sainthood for Nyerere?
 
Oooh Dear Lord!

atleast watu weusi tuanze kuheshimiwa na kupewa matumaini kuwa tupo na tunao uwezo wa kufanya yale ambao wao watu weupe wanafanya. Nimefurahi sana kwa Obama kufanikiwa kushinda uchaguzi huu uliokuwa hautabiriki, kwa kweli ameweka historia na kubadili mitazamo ya watu wengi.

Mungu ampe maisha marefu yenye Afya tele na fanaka aweze kuthibitisha kuwa anaweza kwa vitendo, Akamuongoze katika kuwaza na kuamua kwake kama Rais, asiache atumiwe kama rais wetu fidodido, asimame daima imara akiilinda na kuitetea katiba ya nchi yao, haki za watu bila ubaguzi.

NYANI NGABU, NYANI NGABU, NYANI NGABU, NYANI NGABU, Natumaini na uhakika kuwa upo, na unashuhudia yanayotendeka.. ni wakai wako wa kujikubali (kama mtu mweusi-African), na kujiamini kuwa unaweza/tunaweza iwapo tunapewa nafasi.

Mungu Mbariki Obama,
Mungu Ibariki Marekani,
Mungu Tubariki watu weusi tuheshimiwe sawa na weupe.
 
Wakati sisi waafrika tunashangilia tukumbuke kuwa huyu mwana tulimtelekeza kama tulivyowatelekeza wengine. Yote haya ni matokeo ya malezi ya mama yake mzungu, bibi ( mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi), babu yake mzungu, baba yake wa kambo m-indonesia. Wakati huo sisi tulikuwa MIA kama tulivyo kwa mbegu zetu kibao tulizozitelekeza si ughaibuni tu bali hata hapo nyumbani. Ni mara ngapi sisi wanaume tumejitokeza bila aibu kudai damu yetu (ambayo tuliikana toka ikiwa tumboni hadi kuzaliwa) baada ya mzazi mwenzetu kuifikisha mahali ambapo tuna cha kujivunia? Tumekuwa mabingwa wa kuvuna tusichopalilia.

Wakati tunasherehekea inabidi tuone na aibu. Hasa sisi wanaume wa kiafrika! Mwanetu ametusamehe, inabidi na sisi tuonyeshe kuwa tunastahili msamaha huo!

Amandla.......
 
OBAMA BIDEN > McCAIN,PALIN THATS ALL THERE IS TO IT!!
SINA UHAKIKA BADO KAMA WAZUNGU WATAMPA TICK MTU MWEUSI THOUGH.[/QUOTE]

They just did...American people spoke LOUD and make the history, its amazing.
 
Back
Top Bottom