Rais mteule wa Kenya Dkt. William Rutto namuona kama Hayati Magufuli aliyechangamka kutokana na sera yake kwa watu wa Kenya

RWANDES

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2019
Posts
1,788
Reaction score
4,401
Kipaumbele cha kwanza mahakama ziwezeshwe ili kesi za mafisadi zifanyiwe kazi haraka Kenya kwanza, wanyonge wainuliwe.

DCI akimaanisha Mkurugenzi wa upelelezi nchini Kenya awe independent afanye kazi bila remote control kutoka Serikalini achunguze kila majizi bila maelekezo kutoka juu.

Mazungumzo yake na mwandishi hayo hapo mnaweza kumsikiliza nadhani majizi sahivi roho zao zipo jujuu hata hivyo alishasema yeye siyo mtu wa visasi lakini pia ameshasema hana huruma kwa wezi wa fedha za umma.

Your browser is not able to display this video.
 
Ruto aliahidi kufurusha wachina wote, sasa matumbo joto!
 
Ruto ni mwizi mkubwa ni bilionea hapo Kenya

Magufuli naye alikuwa mwizi mkubwa hadi hawara yake tu alimjengea hoteli ya mabilioni pale Mwenge

Sema wanyonge sijui mnakuwa na akili kama za misukule kuamini sana hawa wanasiasa
 
Ruto ni mwizi mkubwa ni bilionea hapo Kenya,
Magufuli naye alikuwa mwizi mkubwa hadi hawara yake tu alimjengea hoteli ya mabilioni pale Mwenge

Sema wanyonge sijui mnakuwa na akili kama za misukule kuamini sana hawa wanasiasa
Hili nalo neno aisee
 
Ruto aliahidi kufurusha wachina wote, sasa matumbo joto!

Hawezi kufanya hivyo, nchi ina madeni makubwa sana kwa China.

Kuhusu ufisadi inawezekana atatumia huo mwanya, sheria kuwadhibiti wapinzani wake wa kisiasa. Sababu hakuna fisadi mkubwa Kenya kuliko yeye Mr Ruto.
 
Wananchi wamemchagua mtu wanayempenda, hivyo wameweka matumaini makubwa mno kwake.

Atakapokalia tu hicho kiti, atauona ugumu ktk uhalisia wake,

Tunamwombea afanye vizuri maana inaonekana mwisho wake atachukiwa sana sababu ya Imani kubwa alopewa na umma.

Ameeeen
 
Ruto is Ruto.

Magufuli was Magufuli.

Ni watu wawili tofauti wenye fikra tofauti na uwezo tofauti.
 
siku zote ukiwa kwenye mfumo wa kifisadi unakula nao ukisha rungu ndoo mwanzo wa kuanza kuwashughulikia kwani wakati huo uwezo wa kushughulikia mafisadi unakuwa huna soon utaona wembe wa rutto utakavyo wanyoa majizi ! wa kenya wana imani kubwa na wanamjuwa vizuri na wanajuwa alikuwa kwenye mfumo mgumu wakuweza kutekeleza kazi yake ilibidi aende nao hivohivo.
 

Kuna changamoto nyingi atakutana nazo..

Mfano kwa mara ya kwanza Kenya itakuwa inalipa pesa nyingi kulipia madeni yake kuliko shughuli za kawaida za serikali.

Wananchi milioni nne wa Kenya hawana chakula, sababu ya ukame.

Changamoto za Covid, bei za mafuta nk zitapunguza pesa kwa matumizi mengine ya maendeleo.

Ila nafikiri akiamua, akiwa very serious, bold, hacheki na mtu anaweza kufanya mengi kuwasaidia Wakenya hasa wa hali ya Chini. Kuwadhibiti mafisadi itakuwa mtihani mkubwa sana kwake, urais wake na kwa maisha yake. Ila Ruto is streetwise kwahiyo anaweza kuwadhibiti wapinzani wake.

Kenya have massive potential to be hub of East and Central Africa in all sorts of areas.
 
Ruto ni mwizi mkubwa ni bilionea hapo Kenya

Magufuli naye alikuwa mwizi mkubwa hadi hawara yake tu alimjengea hoteli ya mabilioni pale Mwenge

Sema wanyonge sijui mnakuwa na akili kama za misukule kuamini sana hawa wanasiasa

Wanyonge ndio watu rahisi kuwaongoza chini ya jua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…