Huyu wa bara sioni hata kitu kimoja alichofanikiwa. Muhimu kuangalia vitendo / matendo na kauli zake zimejaa taarabu, visingizio, mipasho.
Toka aingie haya ni matokeo ya utawala wake:-
Mfumuko wa bei, kuongozeka matatizo umeme, maji, mbolea madawa ya kulevya, kuwafungulia wauza sembe, kuanzisha tozo, kuchukua mikopo kwa mambo yasiyo na tija.
Teuzi, tenguzi, ufisadi, na mafisadi kurudishwa rasmi kuongoza CCM na serikali, gharama za chakula, ujenzi, usafiri kuongezeka, nidhamu serikalini kushuka, udini.
Mafanikio yake mengine ni masoko kuchomwa moto usiku, ajali za magari za kutisha kila siku, polisi kuongeza uporaji wa mali za raia na kuua raia, machinga, mama ntilie kufukuzwa bila kuwapa alternative, uwiano wa kitoto na upendeleo wa wazi wa vyeo, pesa, ajira kwa watu wa Zanzibar.
Mkakati wa kuwafukuza wamasai na kuuza eneo lao la Loliondo kwa majangiri wa UAE kuwinda na kuua wanyama muhimu, nyara za serikali, urithi wa Watanzania na vizazi vijavyo., Kasi ya kujenga na kuendeleza miradi ya kimkakati imepungua sana. Ukiritimba, rushwa, kucheleweshwa vimerudi kwa kasi Bandarini, kemikali zinatiririka huko Mara ndani Ziwa watu mifugo na samaki wanaumwa na kufariki, tume inakuja na sababu / majibu ya ajabu ajabu, Rais yuko kimya.
Kwa vitendo na kauli zake naonekana hajali maisha ya Watanzania wengi hana uwezo wala malengo, maono, mikakati, nia ya ukweli / dhati, uthubutu wowote na nchi hii zaidi ya kutawala for the sake of kutawala.