Rais Putin amekosea hatua?

Rais Putin amekosea hatua?

Wewe kaa subiria uone madhara ya Russia kudefault,ndani ya siku chache kutoka sasa walionunua dollars denominated bonds za mrusi ambao wengi ni mabengi na taasisi za ulaya wataanza kufeel the heat
 
Wajinga bado ni wengi duniani, hatuwezi kushangaa,
Hata yule nayesema wapigane mpaka Nyuklia, kisha Afrika ndiyo tutakuwa super power ,naye pia hajijui.
Hivi ni nchi gani Afrika inaweza kutengeneza hata Baiskeli?
Kama si uwepo wa wazungu au wachina au wahindi ,basi nchi zetu zitabaki kama mbuga za wanyama tuu.
isi bado hatuwezi wala hatutoweza.
Ni tegemezi mbele kwa mbele.

Watu kama hawa sio wakuwajibu unawaacha tu waandike wanachojisikia
 
kwanini uamini IRAN anaweza akakubali nasio kukataaa
mtasema vyote ila PUTIN anapeleka tu moto
kila leo mnamsumbua PUTIN kwavisimu vyenu UCHWARA
acha iendelee kunyesha ili tuone wapi panavuja
 
Kwa mwendo huu wanaoelekea Europe na Marekani, na jinsi Urusi inavyo sua sua katika diplomasia, na kuzua propaganda za silaha za sumu ,
Naona kama Putin anazidi kuchemsha.\
Mwisho wa Russia unakaribia ,asipo fanya Busara na kukubali matokeo yaKuivamia Yukrain ki Upumbavu
 
Kila mtu anaandika anavyojua
Worse enough wapo nyuma ya keyboard! Siasa na mahusaiano wanayojua ni kati ya CCM Na CDM hata mahusaiano ya kimataifa ktk Jumuiya ya Afrika Mashariki hawana habari nayo, Leo wanaandika mambo ya mbali. Eastern Europe! Kweli? Miluzi tu humu, no contents!
 
endelea kusikitika wakati wenzako wanapata mkong'oto walioukimbilia kwa mikono miwili huku Russia ikiendelea na maisha ya kawaida ya kila siku
 
Mimi naomba tu vita isiishe waendelee kutwangana hatimae walipuane na nyuklia halafu tuanze upya haki ya nani waafrika weusi wataibuka superpower. Kama humankind tutaanza upya mmatumbi tutatawala dunia na kuwa super. Hakuna qayngay yeyote atatudanganya tena nakutugawanya kwasabab tumepitia, yote, tumeona na kujifunza. Na tumewajua mbinu zao.

Hii vita ni kuniombea tu isiishe na nyuklia zitumike.
Kwa akili hizi kweli hata ukibakia peke yako duniani huwezi kuwa superpower.
 
Ndugu wana ukumbi na wafuatiliaji mada za vita vya Russia na Ukrain.

Mimi siiangalii Vita vya Ukrain katika mtazamo wa kivita ,bali mtazamo wa kiuchumi na mgeuko wa mfumo wa uchumi Dunuani.

Nasikitika sana na maamuzi aliyofanya Raisi wa Russia kwa kuivamia Ukrain.

Nahisi ali under estimate reaction ya nchi za Magharibi. Huenda vita hii ika iingiza Urusi kwenye mgogoro mzito na hatimae ikamlazimu atumie silaha nzito za maangamizi.

Kosa lake la kwanza :

1. Mfumo wa Uchumi unadhibitiwa na Marekani na ndugu zake wa Magharibi.

2. Monetary system iko chini ya banki kuu ya Washington na US $ ndiyo inayohukumu transanction ya dunia .

3. Vikwazo vya kuuza na kununua vitaiangusha Russia na hatimae raia wake wataingia mitaani na kumletea vugu vugu la Civil War.

Kosa la pili.

1. Pale Urusi iliposhindwa kuihami Libya na Kumtetea Ghadafi ilifanya kosa kubwa la jinai. Kwani Ghadafi alikuwa na mpango wa kuanzisha New World monetary System. Badala ya kutumia US $ katika biashara za kimataifa ,alitaka itumike Dhahabu.

2. Putin akitaka kusalimika na Mfumo huu uliopo ilimbidi aanzishe mfumo mpya wa uchumi ambao ungelikuw huru na Taifa fulani, na yo ni kutumia sarafu ya Dhabu badala ya US $.

3. Kama hilo halitofanyika kabla puttin kuliwa na Russia kutekwa na Western Block basi Urussi ijiandae kwa maangamizi au vita kuu ya 3.

Hitimisho;-
Kama China itakuwa tayari kumsaidia mrusi, basi ni kubadili mfumo wa uchumi, kuiporomosha US $ isiwe tena World currency kibiashara , na badala yake watumie mfumo aliotaka kuaanzisha Marehemu Ghadafi na Mwenzake Raisi wa Malasia ( Makhatir Muhammad).

Putin Awashawishi waarabu waache kuuza mafuta kwa $ na badala yake watumie Gold, hii itakuwa sete back kubwa kwa Marekani na ndi Mwisho wake.

Lakin Tayari marekani ameanza kufanya Mazungumzo na Iran ili amuondoshee vikwazo na aanze kuuza Mafuta yake ili kuondoa pengo la Urusi.

Naamini Iran anaweza kukubali, lakini Kama Mrusi atacheza vizuri mchezo wke na mchina , anawza kumshawishi Muiran asikubali mtego wa Magharibi wa kimaslahi.

Waarabu nao ni tatizo, kwani endapo Russia itaweza kuwalobby waarabu na kuwahakikishia usalama wa uchumi wao, Mrusi anaweza ku win, lakini Marekani tayari ndiye Allies wa Waarabu, wao huuza mafuta yao kw US $ na kujilimbikizia pesa nyingi katika mabenki ya Ulaya na Marekani.

Kimtazamo si rahisi kwa waarabu kumuunga mkono Mrusi, Labda Iraq ambayo Saadamu alikuwa na mchakato huo na kumsababishia kuuwawa na nchi yake kupindulwa na kuwekwa utawla mwingine..

Swali la Kujiuliza
Jee Mrusi atafaulu pekeyake?
Naishia hapo kwa sasa
Putin as his name is gone... Take from me.
 
Back
Top Bottom