Rais Samia afanya uteuzi: Masauni aondolewa Wizara ya Mambo ya ndani, Kabudi apelekwa Wizara ya Habari na Michezo, Janabi kuwa mshauri wa Rais

Afadhali matinyi ameteuliwa na kurudishwa kwenye game.
 
Huyo Atatupa Tabu Upande Wa Chakula
Utasikia "ili kupunguza kasi ya magonjwa yasiyoambukiza, nashauri bei ya sukari na mafuta ya kupikia iwe juu ili wananchi wajifunze kula visivyoungwa"

Mama: sawa sawa. (Anachukua simu anampigia waziri wa biashara) toa tamko kuadimika kwa sukari na mafuta nchini.

Wafanyabiasha: mafuta lita moja tsh elf 12. Sukari 1kg 7000. Nyama 1kg elf 17.

Raia: mmmhhh, hapo bora tule mboga za majani na uji usio na sukari. 😀😀
 
Suala la wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama kupewa nafasi za kisiasa linachochea sana uvunjifu wa amani wakati wa uchaguzi ili kuwafurahisha wanasiasa na kujipendekeza ili wapate uteuzi.
Rais aache kabisa kuwateua na awaache watumike kwenye majukumu yao ya msingi bila kujiingiza kwenye siasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…