Rais Samia akagua ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa ndege cha Songea, Tsh. bilioni 40.87 zimetumika

Rais Samia akagua ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa ndege cha Songea, Tsh. bilioni 40.87 zimetumika

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amekagua na kupokea taarifa ya ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Songea ambao umekamilika kwa asilimia 100% Mkoani Ruvuma.
WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.35_91ffb0a7.jpg

WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.41_6f24a089.jpg
Rais Dkt. Samia amekagua Kiwanja hicho, leo Septemba 23, 2024 mara baada ya kuwasili Mkoani Ruvuma kwa ziara ya kikazi ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo, kuweka mawe ya msingi ya miradi na kuzungumza na wananchi.

Rais Dkt. Samia amepokea taarifa ya ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Songea uliohusisha upanuzi na kuongeza urefu wa barabara ya kuruka na kutua Ndege, ujenzi maegesho mapya ya Ndege (Apron), ujenzi wa barabara moja ya kiungio, ujenzi wa mnara wa waongoza ndege (Control Tower), kuimarisha maeneo ya usalama kiwanjani pamoja na Ununuzi, usimikaji wa taa za kuongozea ndege na gari la zimamoto.
WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.42_7c8f971b.jpg

WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.34_e4cb2a13.jpg

WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.29_4ec1506c.jpg

Akitoa taarifa mbele ya Rais, Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali ilitoa kiasi cha Shilingi Bilioni 40.87 kukarabati na upanuzi Kiwanja cha Ndege cha Songea ambao hivi sasa utekelezaji wake umekamilika kwa asilimia 100.

Bashungwa ameeleza kuwa kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Songea umerahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kutoka ndani na nje ya nchi ambapo hivi sasa ndege za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) zinatua mara 3 kwa wiki.
WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.34_e4cb2a13.jpg
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara (TANROADS) Mhandisi Mohamed Besta ameeleza kuwa kazi zilizofanyika za uboreshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Songea ni pamoja na ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege (runway) kutoka Mita 1,625 na upana wa 23 hadi kufikia Mita 1,860 na upana wa Mita 30 pamoja na ujenzi wa maegesho ya ndege (Apron) unaoruhusu ndege nne (4) aina ya Q400 Bombadier pamoja na ndege ndogo tatu (3) kupaki kwa wakati mmoja na hivyo kufanya Kiwanja hicho kufikia Kiwango cha 3C kwa mujibu wa viwango vya ICAO.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Abdul Mombokaleo ameeleza kuwa baada ya kukamilika kwa uboreshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Songea matarajio ni idadi ya abiria kuongezeka ambapo takwimu zimeoneshwa toka mwaka 2021 abiria walikuwa 3,900 na sasa wamefikia abiria 19,620.

Mradi wa Ukarabati na Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Songea ni utekelezaji wa mikakati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuongeza ufanisi katika sekta ya usafiri na usafirishaji ili kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.29_4ec1506c.jpg
    WhatsApp Image 2024-09-23 at 14.20.29_4ec1506c.jpg
    285.9 KB · Views: 5
Back
Top Bottom