Pre GE2025 Rais Samia ahahidi miradi mikubwa ya maji, barabara na bandari mkoani Tanga

Pre GE2025 Rais Samia ahahidi miradi mikubwa ya maji, barabara na bandari mkoani Tanga

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais Samia akihutubia wananchi Uwanja wa Mkwakwani-Tanga Februari, 2025


Mbunge wa Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuangalia uwezekano kuvirejesha viwanda vya mkoa huo ili kuchochea ajira na maendeleo ya kiuchumi. Amesema kuwa miaka ya 1970 na 1980, mkoa huo ulikuwa miongoni mwa mikoa yenye viwanda vingi nchini, ukiwa wa pili baada ya Dar es Salaam.

"Mama tunakuomba utubebe, utushike mkono tufufue viwanda vya Tanga – kiwanda cha chuma, kiwanda cha mbolea, kiwanda cha saruji, kiwanda cha mablanketi na nguo, pamoja na viwanda vya sisal. Vijana wetu, kina baba na kina mama watapata ajira," amesema Ummy.

Mbali na viwanda, Ummy amesisitiza umuhimu wa jiji la Tanga kuwa na chuo kikuu, akieleza kuwa ni miongoni mwa majiji machache nchini yasiyokuwa na taasisi ya elimu ya juu.

"Tulikuwa tunajenga chuo kikuu Tanga, lakini bahati mbaya kikapelekwa wilaya nyingine. Mheshimiwa Rais, Makao Makuu ya Mkoa yanapaswa kuwa na chuo kikuu. Tunapendekeza kiitwe Chuo Kikuu cha Shaaban Robert, ili kuenzi heshima ya mzee wetu wa Tanga."

Rais Samia Suluhu akihutubia wananchi mkoani Tanga

"Namshukuru Mungu kwamba ukichukulia wastani wa upatikanaji wa maji ndani ya Mkoa wa Tanga hatupungui kwenye asilimia 79, 80."

"Niwahakikishie wana Tanga, Barabara ya Tanga - Pangani tutaijenga yote kwa lami. [..]. Aidha lipo pendekezo la kupanua barabara ya Segera – Tanga, tayari tumeanza kufanya upembuzi yakinifu wa barabara hii na mbele huko tunakwenda kuiweka kwenye ilani na kuijenga."

"Wanaoijua Tanga wanafahamu kwamba hata wahamiaji wengi wa hapa Tanga walikuja kwa sababu ya bandari yake. Tayari tumeanza kuifufua bandari hiyo, mizigo imeongezeka kutoka tani laki nne hadi tani milioni 1.2. Ongezeko hili limeongeza ajira za vijana kwa wana Tanga. Mipango yetu ya baadaye ni kuifanya bandari ya Tanga kuwa maalum kwa mbolea na mazao ya kilimo."

"Kuhusu uwanja wa michezo, tutaanza na maboresho makubwa ya uwanja wa Mkwakwani kwa kuongeza ukubwa wa majukwaa, mara baada ya kukamilisha viwanja vipya vya AFCON 2027."
 
Hii nyomi, ni ushahidi wa kazi nzuri ya Mama. Wengine wamewekewa Screen kwenye viwanja vya nje. Mfano Bandari ya Tanga Sasa inaingiza mapato B100 kwa mwezi

Hongera kwa kazi nzuri Mama Dkt Samia S Hassan.
 
Kwa jinsi wanafunzi walivyosombwa na malori haijapata kutokea
 
Haa Gen Z
Watawanyoosha CCM
Mchana CCM, Usiku CDM
 
Kwa jinsi wanafunzi walivyosombwa na malori haijapata kutokea
Hawana Uwezo Wa Kujaza Huo Uwanja Wa Mkwakwani
CCM Ni Mafundi Leo Walimu Mahudhurio Yamechukuliwa Uwanjani
RC MOROGORO Kaenda Na Lori La Watu
 
Watumishi wote wa Tanga wamefunga ofisi.
 
Can't waste my bundle 🏃🏿🏃🏿🏃🏿🏃🏿🏃🏿🏃🏿
 

Attachments

  • 1000068996.jpg
    1000068996.jpg
    118.6 KB · Views: 1
Hii nyomi, ni ushahidi wa kazi nzuri ya Mama. Wengine wamewekewa Screen kwenye viwanja vya nje. Mfano Bandari ya Tanga Sasa inaingiza mapato B100 kwa mwezi

Hongera kwa kazi nzuri Mama Dkt Samia S Hassan.
wamesombwa na kila aina ya usafiri unaoweza kufikiri....kujza uwanja.
wanafunzi wote wamepewa likizo ya kuja uwanjani...take note
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Tanga katika muendelezo wa ziara yake ya kikazi mkoani humo tarehe 28 Februari, 2025.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Tanga katika muendelezo wa ziara yake ya kikazi mkoani humo tarehe 28 Februari, 2025.
Anahutubia nini na Wanajeshi kule Rwanda/DRC wametekwa, angerudi ikulu ashughulikie hili jambo la Wanajeshi.
 
Mama piga kazi, wengi wanakuelewa na wako bega kwa bega na wewe. 2025 Ushindi ni 90+%

Huu ndio ukweli mchungu saanaa
 
Back
Top Bottom