Pre GE2025 Rais Samia aligoma alipoambiwa atoke ili wajumbe wapige kura na kumpitisha. Hii ina maanisha CCM wengi hawamtaki?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kile kikao, kikatiba,(ya CCM ya 1977 toleo la Disemba 2022, ibara ya 100, kifungu cha 5 c) hakikuwa cha kumpitisha mgombea urais.

Kile kikao kilikuwa cha kumchagua Makamu Mwenyekiti wa CCM.

Habari ya kupitisha jina la mgombea urais hata haikuwa kwenye ajenda, imelazimishwa tu, tena kwa kuvunja katiba ya CCM.
 
Mwenyekiti ndie mtu anaeendesha kikao. Kikanuni haruhusiwi kutoka kwenye kikao. Maana yenye ndie anaekiongoza kikao.

Pia wanaoruhusiwa kumjadili Rais ni Kamati kuu tu, na ule haukuwa mkutano wa kamati kuu ya ccm.

Wale wajumbe 2000 hawana nguvu ya kumtoa nje Rais na kumjadili , kwa mfumo wa CCM wale ni watoto wadogo sana..
 
Wamteue JJ Mnyika kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzinya Taifa. Ameonyesha weledi wa hali juu jinsi alivyosimamia uchaguzi wa CDM.

Otherwise Samia ataiba, kwa kutofuata kanuni, sheria na taratibu kama alivyofanya hapa kwenye uchaguzi mkuu wa taifa.
 
Mwenyekiti ndie mtu anaeendesha kikao. Kikanuni haruhusiwi kutoka kwenye kikao. Maana yenye ndie anaekiongoza kikao
Wanapomjadili yeye Samia alitakiwa atoke. Yeye ndio alikibadilisha kiwe cha kumjadili yeye, kupitisha wagombea wa urais wakati jukumu lake halikuwa hilo.

Angeweza kusema hiyo sio agenda ya mkutano huu.
 
MaCCM ni majitu ambayo yanapenda kuvunja sheria na kukiuka utaratibu kwa makusudi.
 
Kwakuwa tulikuwa bize na mkutano wa chadema hatukuyaona hata, aibu aisee
 
Nilikuwa nawaza Mama atawezaje kuondoa ibara kwenye Katiba ya ukomo wa urais.Nilimchukilia poa.Kumbe anaweza.Kwa hiyo,mwaka 2029 litapigwa surprise kama lile la juzi.
Watu watabaki na butwaa na sisi tunaotaka aendelee tutabaki na machozi ya furaha.
 
Nilikuwa nawaza Mama atawezaje kuondoa ibara kwenye Katiba ya ukomo wa urais.Nilimchukilia poa.Kumbe anaweza.Kwa hiyo,mwaka 2029 litapigwa surprise kama lile la juzi.
Watu watabaki na butwaa na sisi tunaotaka aendelee tutabaki na machozi ya furaha.

Hata akichoka atamuweka Abdul, au Mchengerwa. Familia iendelee kutawala. Kama koo nyingine za Kisultani duniani.

Nafikiri utaendelea kububujikwa na machozi ya furaha.
 
Hujaandika ukweli,hakugoma ili watu wapige kura,muda wa kura ulikuwa haujafika,aliombwa atoke ili wao wajumbe ndio wajadili hiyo ndipo aliposema kuwa,yeye hatoki kama kumjadili basi wamjadili na yeue yupo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…