KERO Rais Samia alivyokuja Geita tulipata maji, tangu kaondoka shida imerudi palepale

KERO Rais Samia alivyokuja Geita tulipata maji, tangu kaondoka shida imerudi palepale

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Unakumbuka Ile video Magufuli anaulizwa katika mkutano,hapa kwetu wakuu wakifika maji yanatoka,lakini wakiondoka maji yanakatika.
Magufuli anamwita mhandidi kujibu hilo swali.
Mhandidi anasema,"Viongozi wakija,tunaweka mabomba ambayo yanadumu kwa siku mbili au tatu halafu yanachakaa"
Ina maana Magufuli alimvua nguo mhandisi hadharani.
 
Mta
Mimi Mkazi wa Geita kwa muda mrefu sasa mkoa wetu umekuwa na changamoto ya mgao wa maji.

Maji yamekuwa yakitoka mara moja kwa wiki. Hii ni kwa Mtaa wetu na maeneo mengine mengine.

Kila tukiuliza shida ni nini viongozi wetu wamekuwa wakitoa visingizio. Kila mara wamekuwa wakisema kuwa wapo kwenye mchakato wa kutengeneza mfumo na kutanua mtandao wa maji

Ajabu ni kwamba juzi hapa wakati Rais Samia alipotutembela Wanageita katika ziara yake maji yalikuwepo vizuri tu.

Maji yalikuwa yanatoka na tulipata maji karibu sehemu zote, maji yalikuwa yanamwagika, karibu sehumu zote maji yalikuwepo lakini baada ya Rais kuondoka na maji nayo yakaondoka hayakutoka tena.

Kiukweli kabisa tunapata shida. Imefikia hatua tunanunua maji dumu moja 500 au 1,000 mpaka 1500.

Sasa hiki wanachozungumza viongozi ni ukarabati na matengenezo gani yasiyoisha? Ninachojiuliza mimi na wenzangu ni kuwa Mamlaka ya maji na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA) kwani shida ni nini?

Baadhi yenye changamoto ni Mtakuja Mwatulole, Nyankumbu, wale wanaopata nafuu wao wanapata maji ya bomba mara moja kwa wiki.

Pia, soma: √ - Tatizo la Maji kwa Mji wa Geita kuwa Historia kufikia Oktoba 2025
Mtahiniwa wenyewe si ndio nyingi mnaoshabikia ccm?sasa mnalialia nini?mkachote maji ziwani.mkiambiwa hiki chama hakifai hamuelewi.pigeni chini hao wabunge wa ccm lina bado mnawakumnatia sasa mpambano na hali zenu.chimbeni visima.
 
Hapo ndio ujue watu wanaweza kupata huduma zao akiwepo kiongozi makini.
Kwa sasa mpaka apatikane ndio mtapata hayo maji.
 
Pale katoro kuna wahaya, wamesahau mila na tamaduni? Hili sio jambo kubwa kwao
 
Back
Top Bottom