JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, Kamishna wa Magereza CP. Jeremiah Yoram Katungu amepandishwa cheo kuwa Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) na kuteuliwa kuwa Mkuu wa Jeshi la Magereza.
CP Katungu anachukua nafasi ya CGP Mzee Ramadhani Nyamka ambaye amestaafu.
Uteuzi huu umeanza tarehe 28 Julai, 2024.