Rais Samia ashuhudia utiaji saini Ujenzi wa SGR kipande cha Nne (Tabora - Isaka 165km), aeleza kutoridhishwa na utendaji wa TPA

Rais Samia ashuhudia utiaji saini Ujenzi wa SGR kipande cha Nne (Tabora - Isaka 165km), aeleza kutoridhishwa na utendaji wa TPA



Amos Makalla – RC Dar es Salaam

Mh. Rais SGR itategemea sana bandari. Nikushukuru sana kwa kutoa fedha bilioni 210 za kuboresha Bandari. Fedha zile ulizozitoa zimeleta manufaa makubwa. Hapa Dar es Salaam wanasema Bandari sasa ni mgodi – yaani ni mgodi kama ilivyo migodi ya madini. Kwa maana Bandari yetu sasa mizigo imeongezeka. Meli zimeongezeka.

Mh. Rais, nilikuwa napitiapitia; Congo mizigo yao ilikuwa tani milioni 1.9, sasa ni milioni 2.6. Burundi wanategemea Bandari ya Dar kwa asilimia 99.

Uganda walikuwa hawatumii Bandari yetu lakini kwa ziara zako nchini Uganda umemshawishi Rais Museveni. Wametoka tani laki 1 na 40 sasa wapo tani laki 3.

Mbona bandari ya Dar huonekana mabehewa ya Uganda Railway ya kubeba mizigo!
 
Kuna kitu hakiko sawa kabisa Nchini kwetu hapa, kuna miradi inafanyika bila kufanya tathimini ya kina na mwisho wa siku inakuwa white elephant. Tuwe wakweli Bandari yetu inapokea mizigo mingi ya DRC na Burundi. Halafu leo hii badala upeleke reli Kigoma ambapo utatrap soko ya DRC na Burundi unapeleka Isaka unamupelekea nani?
 
Kauli zake za kuwapa kipau mbele sekta binafsi ajue sekta binafsi yetu imejaa wahuni wala hawakidhi sifa. Wengi ni wababaishaji wanaotaka kudandia mtaji wa serikali na kupora kutoka umma badala ya kuwekeza mtaji wao.

Samia awe macho na wababaishaji wenyeji. Bora kuleta wawekezaji wa nje wa kweli, yaani wana mtaji kuliko wababaishaji wa ndani. Hao watavuruga badala ya kupata matokeo yaliyotarajiwa wataibia umma.
 
Mimi katika tembeatembea zangu nimeona SGR inakimbilia Tabora ila hiyo ya Kigoma Gitega kupasua hiyo Milima itachukua muda mtefu sana na hienda isiwe na faida.
 
Hakuna Nchi yenye mipango dhabiti yenye barabara pekee bila kuwa na reli.

Marekani yenye sekta kubwa ya usafiri kwa njia ya barabara bado ina railway network nchi nzima na zenye ubora wa viwango.

Ni ubinafsi tu wa wafanyabiashara wa malori ila Treni haitaathiri biashara zao. Kama ipo ipo tu.
Tunataka barabara kwanza, hizo siasa zenu za reli zitafuata mkituletea barabara maana ma reli yenu hayasaidii kutoa Mazao yangu kijijini.
 
Hongera zake. Kila siku anatia tu saini! Kipande cha kutoka Dar Moro, mwaka wa 2 huu, ni sound tu.

Mara treni itaanza rasmi safari zake mwezi fulani! Ukifika huo mwezi wanasogeza tena!
Aliyekaa nayo miaka 6 kila siku reli reli na hakumaliza utiaji saini vipande vingine je?
 
Watanzania tunaona kazi kubwa anayo ifanya Rais wetu, tupo pamoja naye kila hatua, jukumu letu kubwa ni kutekeleza yale yote anayo yaelekeza haswa kwa watendaji.

watendaji tuache uzembe, kuanzia sasa mtendaji yeyote atakaye zembea kutimiza wajibu wake tutamchukulia kama anahujumu jitihada za Rais.
 
Kipande cha kutokea Morogoro mpaka Makutupora kimefikia asilimia ngapi za ujenzi wake?
Kadogosa kasema hapo juu "asili mia 87", sijui kama ni kweli.
Kama ni kweli, hiyo ni hatua nzuri.
 
Ingawa urais ni taasisi lakini lazima apatikane mtu mwenye weledi wa kusimamia hiyo taasisi iwe imara.
 
Ingawa urais ni taasisi lakini lazima apatikane mtu mwenye weledi wa kusimamia hiyo taasisi iwe imara.
Sio lazima,weledi wa kuua Wananchi na kuwapoteza, Weledi wa kuwafanya Wapinzani Watanzania wenzako kuwa Maadui wa Taifa.

Taasisi iwe imara tu.
 


AMOS MAKALLA – RC DAR ES SALAAM

Mh. Rais SGR itategemea sana bandari. Nikushukuru sana kwa kutoa fedha bilioni 210 za kuboresha Bandari.

- Bandari zimeboreka, mizigo kibao
Fedha zile ulizozitoa zimeleta manufaa makubwa. Hapa Dar es Salaam wanasema Bandari sasa ni mgodi – yaani ni mgodi kama ilivyo migodi ya madini. Kwa maana Bandari yetu sasa mizigo imeongezeka. Meli zimeongezeka.

Mh. Rais, nilikuwa napitiapitia; Congo mizigo yao ilikuwa tani milioni 1.9, sasa ni milioni 2.6. Burundi wanategemea Bandari ya Dar kwa asilimia 99.

Uganda walikuwa hawatumii Bandari yetu lakini kwa ziara zako nchini Uganda umemshawishi Rais Museveni. Wametoka tani laki 1 na 40 sasa wapo tani laki 3.

MASANJA KADOGOSA – MKURUGENZI MKUU TRC

Mh. Rais, leo tunakutana katika hafla fupi ya kutiliana saini mikataba miwili – Mkataba wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa kipande cha 4 (Tabora – Isaka) na Mkataba wa Mafunzo kwa Vitendo kati ya TRC na Shirika la Reli la Korea (Korea Railway).

- Rais Samia ametekeleza ahadi
Tukio la leo Mh. Rais, linafanya vipande vyote sasa vitano kwa maana ya kutokea Dar mpaka Mwanza, vina wakandarasi. Kwa maana phase ya kwanza.

Wakati ukilihutubia Bunge mwaka 2021 uliahidi kuendelea na kukamilisha ujenzi wa reli ya Dar – Makutupora na kuanza ujenzi wa vipande vingine kikiwemo kipande cha Mwanza – Isaka, Makutupora – Tabora, Tabora – Isaka, na leo tunashuhudia ahadi yako ikikamilika.

Mh. Rais uliahidi pia kuanza ujenzi wa reli awamu ya pili yenye kilomita 1010. Kwa maana ya kipande cha Tabora- Kigoma (km 411); Uvinza-Kitega, Burundi (km282) na baadaye kuendelea na vipande vingine.

Mh. Rais, naomba kutoa taarifa kuwa kazi ya manunuzi inaendelea.

- Thamani ya reli
Thamani ya reli hii, kwa maana ya utiaji saini wa leo, utafikia takribani trilioni 16.7 kwa awamu ya kwanza (Dar – Mwanza) na serikali hadi sasa imelipa malipo ya jumla ya Sh. Trilioni 6.4. Malipo ya kazi yote inayotekelezwa na kuhakikiwa. Kama nilivyotaja hapo, Mkandarasi hatudai kitu chochote.

Maendeleo ya hatua ya ujenzi kwa vipande vitano (km 1219), kipande cha kwanza tunaendelea na majaribio ya mifumo mbalimbali na – tunaendelea vizuri sana. Kwa sasa hivi sehemukubwa ya ujenzi iliyobakia ni kutoka Ilala kuingia Bandarini.

Serikali inajenga mifumo ya umeme ya kupitisha umeme wa kilowatts 220 kwa maana ya kwamba kipande cha Dr – Morogoro kimekamilika asilimia 100, na kipande cha Makutupora- Dodoma kimekamilika asilimia 90. Na chenyewe tunaendelea vizuri sana.

Thamani ya mkataba tunaosaini leo ilakuwa dola milioni 900.1 (Tsh. Trilioni 2.094) na hii inajumuisha kodi.

- Capacity building kwa watendaji
Kwenye uendeshaji tutapata capacity-building kutoka kwa Korea Railway. Tutakaokuwa tukiendesha huu ni sisi Watanzania (Kwa maana ya TRC) kuhakikisha hakuna kitu kinakwenda kinyume na matarajio yako Mh. Rais lakini pia na matarajio ya Wananchi.

Tuliamua kutafuta Shirika la Reli ambalo ni bora zaidi ili wakati tutakapoanza uendeshaji kutakuwa na watendaji wenye uzoefu. Baada ya kushindanisha, wenzetu wa Korea walipata hiyo kazi. Kwahiyo kule kwenye maintenance kutakuwa na mainjia behind, kwenye signory tutakuwa na mainjinia behind, kwenye operations tutakuwa na mainjinia behind, kwenye control kutakuwa na mainjinia behind. Kila sehemu ya uendeshaji kwa miaka mitatu.

Treni yetu itakuwa ni hi-tech, yaani itaendeshwa kwa teknolojia ya juu. Ni lazima tuwe na tahadhari ya kuhakikisha kuwa uwekezaji huu mkubwa unakuwa na tija.

Wengine watajengewa uwezo hapahapa ndani na wengine nje ya nchi.

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

- Sheria za 'PPP' na Manunuzi ziangaliwe

Hizo Sheria kazitazameni, badala ya kutupeleka mbele zinaturudisha nyumq. Dunia ya sasa amekuja mtu, mnaelewana, ana uwezo, mnamuamini, mnasaini na kwenda mbele. Kuanza kuzunguka Sheria ya PPP haikufuatwa, mtu na Fedha anatafuta kwingine pa kwenda

- Siridhishwi kabisa na utendaji wa bandari zetu
Wale tuliowakabidhi uendeshaji wa bandari zetu wafanye kazi kwa kasi mno, siridhishwi kabisa na kazi za bandari, siasa na longolongo zilizopo. Huko nje wanaendesha kwa kasi mno sisi bado tunasuasua, wawekezaji wanakuja tunawazungusha

Nasema bandari watu wafanye kazi, tutatupia jicho, waliokabidhiwa bandari nataka tuelewane vizuri. Bandari ya Dar ikifanya kazi vizuri nusu ya bajeti itatokana na bandari hiyo. Wale mliokabidhiwa bandari nataka tuelewane

- Mwanza, Tabora kuwa Vitovu vya Biashara nchini
Lengo ni kuifanya Dar es Salaam kuwa kitovu kikuu cha biashara Afrika, baada ya hapo Mwanza itafuata katika Kanda ya Ziwa Victoria, pia Tabora kuna reli, bomba la mafuta na barabara

- Wenye akili za kawaida wanalaumu Rais anasafiri tu
Wale wenye akili za kawaida ni rahisi kulaumu, wanasema ‘Rais anasafiri tu, hakai, hatembelei mikoa’, nikienda mkoani tajenga siasa ya ndani hakuna maendeleo, nikienda nje nakwenda kutafuta fedha za maendeleo.

Rais Samia ashuhudia utiaji saini Ujenzi wa SGR kipande cha Nne (Tabora - Isaka 165km ikulu badala ya kufika Tabora kwenye eneo la mradi?​

 
Back
Top Bottom