Rais Samia asihurumiwe kwakuwa ni mwanamke; kiongozi wa nchi lazima awe na ngozi ngumu. Wapambe acheni kulialia

Rais Samia asihurumiwe kwakuwa ni mwanamke; kiongozi wa nchi lazima awe na ngozi ngumu. Wapambe acheni kulialia

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Kama kuna mtu anadhani kuwa kwa sababu tu Rais Samia ni mama basi atahurumiwa pale anapovurunda kutokana na jinsia yake basi anajidanganya.

Siasa ni ngumu na unatakiwa kuwa himilivu kweli kweli. Ukitaka kujua hilo angalia siasa za wenzetu kama Kenya ama Marekani. Kiongozi anaangaliwa kama kiongozi na siyo jinsia yake.

Watanzania neno kunyoa tu nanga zimewapaa wakati safari bado ni ndefu. Hilo ni neno la kawaida sana kwenye siasa. Nimeanza kuamini kuwa watanzania wengi ni watu wa huruma huruma sana. Mama kusemwa kuwa atanyolewa basi imekuwa tabu kweli kweli.

Yani inawezekana hata siku akivurunda kisha akaja mbele yetu akalia tutaishia kumuomba sisi msamaha (?) Emb mufike mahali mbadilike maana mnakuwa nyuma mno kwenye vilinge vya siasa.

Tujiandae kukutana na kauli nzito nzito zaidi ya kijikauli chepesi sana cha Mdude Nyangali. Kumbukeni kuwa serikali iliyomshughulikia Mdude na Lissu basi Samia alikuwemo ndani. Usitarajie maneno mepesi tena kwa mtu aliyepotezewa malengo na muda kwa zaidi ya mwaka.

Hivi ni nani kati yenu akicheleweshewa tu mshahara wake anakuwa na furaha kwa boss wake? Sembuse kufungwa? Kumiminiwa risasi? Ukiwa unawalaumu hawa watu jichunguze kwanza ni jambo gani kubwa amewahi kukufanyia mwenzako kwa ubaya na jinsi ulivyomkasirikia? Halafu linganisha na lililowakuta hawa. Unajua ni kitu gani Chadema walifanyiwa kwenye uchaguzi mkuu uliopita? Bado unataka wawe soft soft?

Emb jiangalieni bwana. Mama kama mnataka kumsaidia mwambieni ahimarishe mifumo ikiwemo katiba yenye meno na inayoeleweka. Vinginevyo basi jiandaeni kuwa kina watu wa huruma sana. Mnakera eti mama mama mama!
 
Mambo yanazidi kutaradadi..na hii awamu kwa kweli watuache na sisi tutambe!wahuni
 
Hiyo mbegu aloipanda hayupo.

Aliyepo hajaonyesha kuimwagilia ile mbegu.

Hoja zijengwe watu waelewe sio matusi
Yeye ameanza kwa mtindo uleule wa kukwepa jukumu la katiba. Watu wanachukua tahadhari mapema maana walishaumwa na nyoka.
 
Moja ya mbinu muhimu kwenye siasa ni kujua nini cha kusema, kwa wakati gani, kwa namna gani na wapi pa kukaa kimya.

Yawezekana kabisa kudai katiba mpya kistaarabu, na uthibitisho upo kwenye mchakato uliopita wa kudai katiba mpya chini ya mwavuli wa UKAWA.

Mna uhuru wa kutumia lugha mbovu lakini athari yake kubwa ni kutengwa na kundi muhimu kwenye siasa za Tanzania: watu wasio na chama. CCM pamoja na mbinu zake chafu hujihangaisha sana ili ikubalike kwenye kundi hilo.

Sasa busara kidogo tu zilipaswa kuwaambia kuwa japo Mama Samia ni Rais lakini pia ni MWANAMKE. Na mkiendelea kujitoa ufahamu, mtongea hoja za msingi lakini Watanzania wengi watawaona kuwa ninyi mnam-bully Mama Samia.

Kujaribu ku-justify lugha isiyo ya kistaarabu ya Mdude kunazidi kuonyesha how hopeless you people are. Lakini sio la kushangaza maana hata yule "mwanaharakati" aliyewahi kumtukana Mwenyekiti wenu na kumuita "jambazi" leo ni swahiba wenu, na mwakalia kimya unyanyasaji anaoufanya dhidi ya watu wasio na hatia. Birds of a feather?

Finally, katiba mpya wanayostahili Watanzania ni ya Watanzania wote na sio ya "Chadema na wanaharakati." Mpo sahihi kuipigania kwa sababu nanyi ni Watanzania lakini msibinafsishe suala hili kuwa lenu peke yenu. Na msitukane pindi mnapokutana na hoja zinazokinzana na hoja zenu.

Baadhi ya wanachama wenu wamemtukana Prof Issa Shivji kwa "kosa" la kutahadharisha kuwa katiba mpya si jambo la kukurupuka. Baadhi yenu mmedai "anazeeka vibaya" huku wengine wakidai anatafuta u-DC. Ieleweke tu kuwa kamwe katiba mpya haitopatikana kwa niia za kihuni
 
Si bora hiyo damu kuliko huu ujinga uliotamalaki.
Ujinga uliotamalaki? Mlipoibiwa kura Oktoba mwaka jana na Lissu akawaomba mfanye maandamano, mlitokea? Ndugai na NEC wamelazimisha wabunge 19 mpaka leo, mmefanya nini?
 
Moja ya mbinu muhimu kwenye siasa ni kujua nini cha kusema, kwa wakati gani, kwa namna gani na wapi pa kukaa kimya.

Yawezekana kabisa kudai katiba mpya kistaarabu, na uthibitisho upo kwenye mchakato uliopita wa kudai katiba mpya chini ya mwavuli wa UKAWA.

Mna uhuru wa kutumia lugha mbovu lakini athari yake kubwa ni kutengwa na kundi muhimu kwenye siasa za Tanzania: watu wasio na chama. CCM pamoja na mbinu zake chafu hujihangaisha sana ili ikubalike kwenye kundi hilo.

Sasa busara kidogo tu zilipaswa kuwaambia kuwa japo Mama Samia ni Rais lakini pia ni MWANAMKE. Na mkiendelea kujitoa ufahamu, mtongea hoja za msingi lakini Watanzania wengi watawaona kuwa ninyi mnam-bully Mama Samia.

Kujaribu ku-justify lugha isiyo ya kistaarabu ya Mdude kunazidi kuonyesha how hopeless you people are. Lakini sio la kushangaza maana hata yule "mwanaharakati" aliyewahi kumtukana Mwenyekiti wenu na kumuita "jambazi" leo ni swahiba wenu, na mwakalia kimya unyanyasaji anaoufanya dhidi ya watu wasio na hatia. Birds of a feather?

Finally, katiba mpya wanayostahili Watanzania ni ya Watanzania wote na sio ya "Chadema na wanaharakati." Mpo sahihi kuipigania kwa sababu nanyi ni Watanzania lakini msibinafsishe suala hili kuwa lenu peke yenu. Na msitukane pindi mnapokutana na hoja zinazokinzana na hoja zenu.

Baadhi ya wanachama wenu wamemtukana Prof Issa Shivji kwa "kosa" la kutahadharisha kuwa katiba mpya si jambo la kukurupuka. Baadhi yenu mmedai "anazeeka vibaya" huku wengine wakidai anatafuta u-DC. Ieleweke tu kuwa kamwe katiba mpya haitopatikana kwa niia za kihuni
Deep sana hii Mkuu naomba nitumie hili bandiko lako kama utaniruhusu.
 
Moja ya mbinu muhimu kwenye siasa ni kujua nini cha kusema, kwa wakati gani, kwa namna gani na wapi pa kukaa kimya.

Yawezekana kabisa kudai katiba mpya kistaarabu, na uthibitisho upo kwenye mchakato uliopita wa kudai katiba mpya chini ya mwavuli wa UKAWA.

Mna uhuru wa kutumia lugha mbovu lakini athari yake kubwa ni kutengwa na kundi muhimu kwenye siasa za Tanzania: watu wasio na chama. CCM pamoja na mbinu zake chafu hujihangaisha sana ili ikubalike kwenye kundi hilo.

Sasa busara kidogo tu zilipaswa kuwaambia kuwa japo Mama Samia ni Rais lakini pia ni MWANAMKE. Na mkiendelea kujitoa ufahamu, mtongea hoja za msingi lakini Watanzania wengi watawaona kuwa ninyi mnam-bully Mama Samia.

Kujaribu ku-justify lugha isiyo ya kistaarabu ya Mdude kunazidi kuonyesha how hopeless you people are. Lakini sio la kushangaza maana hata yule "mwanaharakati" aliyewahi kumtukana Mwenyekiti wenu na kumuita "jambazi" leo ni swahiba wenu, na mwakalia kimya unyanyasaji anaoufanya dhidi ya watu wasio na hatia. Birds of a feather?

Finally, katiba mpya wanayostahili Watanzania ni ya Watanzania wote na sio ya "Chadema na wanaharakati." Mpo sahihi kuipigania kwa sababu nanyi ni Watanzania lakini msibinafsishe suala hili kuwa lenu peke yenu. Na msitukane pindi mnapokutana na hoja zinazokinzana na hoja zenu.

Baadhi ya wanachama wenu wamemtukana Prof Issa Shivji kwa "kosa" la kutahadharisha kuwa katiba mpya si jambo la kukurupuka. Baadhi yenu mmedai "anazeeka vibaya" huku wengine wakidai anatafuta u-DC. Ieleweke tu kuwa kamwe katiba mpya haitopatikana kwa niia za kihuni
Neno "Kunyoa" ni tusi? In fact inategemea umelichukulia katika muktadha upi. Chadema walishakomazwa na kila aina ya uhuni kutoka awamu ya tano hivyo wanajua wanafanya nini. Wanachukua tahadhari kwani hata Magufuli alianza hivi hivi mwisho yaliyotokea kila mmoja wetu ni shahidi.
 
Back
Top Bottom