Rais Samia atengua uteuzi wa Eric Hamissi, Mkurugenzi Mkuu wa Usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

Rais Samia atengua uteuzi wa Eric Hamissi, Mkurugenzi Mkuu wa Usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

D
ndugu yangu hata ukiweka wachungaji na maaskofu pesa itapigwa tu, TPA ndiyo jiko la nchi Mkuu msosi wote unapikwa hapo - yaani pesa inakutafuta wewe sasa ufanyaje.
Dah, ko wazalendo hatuna nchi hii? Watu weledi wapo sema hawana majina
 
Binafsisha hizi BANDARI, naona zinatupa shida kubwa kuziendesha au recruits freshers kutoka University, peleka wachache pale Durban, Capetown, Rotterdam, Botswana (dry port)wakajifunze kwa 24mth kuhusu uendeshaji wa hizi bandari, na ajira mpya zifanyike yaani we need to start upya
Unafikiri hawajui?

Unachokiona ni roho ya upigaji waliyonayo watz
 
Uzuri alimteua mwenyewe
Kweli aisee, Eric alikuwa MSCL na alifanya kazi nzuri sana ya kulifufua shirika la meli na Mama akamuhamishia bandari, ni jamaa mmoja humble sana na mchapa kazi, mama kaligusia kwenye hotuba yake leo ni kama vile anaona biashara haifanyiki vya kutosha bandari ya DSM...labda Eric anabana sana.
 
Sasa kumtumbua na kumuweka aliyekuwa kaimu wake ndio suluhisho la tatizo?

Bandari inatakiwa ifumuliwe kuanzia chini kabisa mpaka kileleni. Hii mambo ya kuondoa mtu mmoja mmoja huku kuacha mashina na mizizi ni ujinga tu.

Ni ngumu kuamini kama kuna madudu basi yalifanywa na Mkurugenzi peke yake. Kwa vyovyote ni kwa msaada mkubwa kwa waliokuwa chini yake. Sasa leo hii ukisema unamuondosha mkurugenzi na kuacha walio chini yake ambao kiuhalisia ndio watekelezaji wakuu wa hayo madudu hapo unakuwa umefanya nini?

Hiki kinachofanyika ni sawa na kuzima moto kwa kutumia mabua, kwa juu unaona kama moto umezimika ila chini unafukuta vile vile.
Ila bandarini ipo shida kubwa sana,nadhani ulaji wa pale ndio unaowafanya wasidumu,pesa yake ni ndefu sana,naona inafikia mahali mtu anaona wacha tu nile hata nikitumbuliwa nakuwa niko vizuri...
 
Huwa nashindwa kuelewa BANDARINI kuna nini?! mbona huwa hakuishi MATATIZO?!
yaani kunaonekana kama kuna miungu watu/ uttachable!!!

Nashauri Jeshi lipewe Jukumu la kuendesha Bandari au waongeza nguvu hapo naamini kutakaa sawa, kama kuna wabishi tupa pembeni.

Huwa najisikia maumivu kila mara Rais analalamikia utendaji wa Bandari sio wa kuridhisha. kama kuna watendaji wanao fanya hujuma ya kukwaza juhudi za Rais wabainishwe na watolewe mara moja.
Mkuu, bandarini pale sasa hivi mizigo inajipitia free, wapigaji wanafanya yao!

Sasa ukizingatia hangaya alisema yeye siyo simba, hataki kodi za dhuruma, anataka watu walipe kodi kwa hiari.

Yani mtz umwambie alipe kodi kwa hiari[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Haya matozo tuliyolundikiwa kwenye bidhaa ni matokeo ya watu kulipa kodi kwa hiari.
 
Hapo hata umchague Baba paroko ni lazima akulize tu, panashawishi. Hivi zile flow meter zimeshaanza kufanya kazi. ?
Si uliktaka viuno haoa kwamba yule alieondolewa ni sukuma gang amekomeshwa? Vipi tena?
 
Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Ndgu. Eric Hamisi. Nafasi yake inachukuliwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ndgu. Plasduce Mkeli Mbossa.

Bila katiba Mpya tutateuana sana na kufukuzana sana hadi mwisho wa dahali
 
Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Ndgu. Eric Hamisi. Nafasi yake inachukuliwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ndgu. Plasduce Mkeli Mbossa.

Awamu hii ya Sita ukiwa tu ni Team Mstaafu Msoga na ukijuana nae haraka sana ukimtumia Mwanae ( Naibu Waziri ) akukutanishe nae jua Umeula kwani 'Mama' hapindui kwa Mswahili.
 
Yes, tukubali tu kwamba tumeshindwa tumpe mwekezaji aendeshe ili sisi atulipe kodi yetu. Kuna muda Kagame aliomba tumpatie ili awe anatupatia kwa mwezi Trillion 1, tukagoma. 🙂
Au Kagame anatuhujumu pale ili tuonekane hatuwezi aichukue?
 
Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Ndgu. Eric Hamisi. Nafasi yake inachukuliwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ndgu. Plasduce Mkeli Mbossa.

Hizi kazi kama wataendelea kuzitoa kwa kuteuwa teiwa basi watafukuzana kila siku.

Kazi za Wakurungenzi wote inatakiwa zitangazwe na wenye uwezo wanyanyiwe interview na wapewe kwa mikataba ya miaka tano 5 for a maximum of 15 years kwenye kampuni moja.
 
Back
Top Bottom