Mchango wa kwanza kabisa unaofikirisha.Bandari bado wahusika wanashindwa kuteua watu educated na experienced na mambo ya bandari. Wapo wasomi wazuri pale DMI wengine mpaka wamestaafu akina Mzee Mayagilo hawa wameanza kwenye Ubahari to Marine engineering to Management PHDs.
Serikali inahitaji kuwekeza kwenye Teknolojia ambayo italeta newly improved controls. Mfano Port of Durban .
Suala la Hamisi kwa uzoefu wangu na hisia ni kwamba alijitahidi kutenda na kujali wafanyakazi lakini pia alikula kwa kamba yake ila kilichomtoa pale ni kwamba kuna matajiri fulani ambao wanafanya shughuli zao za mizigo wameibuka awamu hii ya mama nadhani alishindwa kwenda nao sawa wakaamua wamwage ugali kwa bosi wake. Bandarini kuna matajiri hawa kama hawa wanaofadhili team ya wananchi wale kama hutoweza kwenda nao sawa wanauwezo wa kukujengea fitina ukatolewa wale huwa mazungumzo yao ni magogoni, kwa katibu au kwa mzee wa uongo wakisha kuchongea huko lazima utatolewa tuu.
Nadhani kazi hiyo ingetangazwa na watanzania wenye vigezo wakaiomba. Yupo kijana wa Liundi anapiga sana kazi pale TPA kama Business dev manager sijui au Port manager. Wapo wasomi wamepita DMI wamekaa scandinavia na wamecheza na bandari wanajua nini kifanyike tusione ubaya kuchukua diasporas.
JF nako kumekuwa sehemu ya kushangilia tu, uchambuzi wa kutumia akili umekuwa adimu.
Anayejua sababu za Eric kutumbuliwa, tofauti na haya aliyoeleza hapa mkuu 'Mookiesbad98' ayaweka hapa tuyajadili.