Pre GE2025 Rais Samia awaonya wanasiasa wanaoanzisha vijiji ndani ya hifadhi

Pre GE2025 Rais Samia awaonya wanasiasa wanaoanzisha vijiji ndani ya hifadhi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Rais Samia Suluhu Hassan ameonya Wanasiasa, hususani wabunge na Madiwani kuanzisha vijiji katika maeneo ya hifadhi pindi wanapoona chaguzi zinakaribia na hawakubaliki.

Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu Agosti 5, 2024 katika mkutano wa hadhara alipozungumza na wananchi wa Ifakara katika Uwanja wa CCM Ifakara mkoani Morogoro, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya siku sita mkoani humo.

Unajua zipokaribia chaguzi hizi hasa Madiwani, Mtu akiona yuko vibaya kwa upande mwingine wa eneo lake anakwenda kusogeza watu kuanzisha kijiji, sasa haya ya kuanzisha vijiji bila kujali tunavianzisha maeneo gani, vijiji vingi vilivyoanzishwa ndani ya maeneo ya hifadhi ni kwa ajili ya Wanasiasa.

Soma pia: Rais Samia: Baadhi ya Madiwani wanahusika katika kusababisha Migogoro ya Ardhi



 
This is nothing but all about wananchi wa ngorongoro ambao kituo cha kupigia kura wamekifuta kwa sababu wamasai wameambiwa pale ni eneo la hifadhi.

Justification za kufuta kile kijiji na kufuta kituo cha kupiga kura sababu wanajua wangepoteza kura za wamasai wapatao laki na nusu sababu ya kuwahamisha wenzao na kutangaza kwamba lile ni eneo la hifadhi.

Hata sisi sio wajinga namna hiyo tunaelewa.
 
Aanze yeye kujiwajibisha. Anataka kuanzisha migodi ndani ya hifadhi
 
Mwanasiasa gani ana uwezo wa kuanzisha Kijiji? Kijiji mpk kusajiliwa ni kazi ya mtu mmoja?
Huyu bibi vipi huyu??!
 
Back
Top Bottom