Rais Samia awatakia kila la heri Darasa la Saba walioanza Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi

Rais Samia awatakia kila la heri Darasa la Saba walioanza Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Nawatakia kila la kheri wanafunzi 1,230,780 wa Darasa la Saba mlioanza Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi leo. Mnatoka hatua moja ya elimu na malezi kwenda nyingine katika safari yenu ya kujiandaa kutoa mchango wenu wa maendeleo kwa Taifa letu. Serikali imeandaa mazingira sahihi ili muweze kufikia lengo hili.

Ahadi yangu kwenu katika safari yenu ya elimu na maisha ambayo tayari inatekelezwa ni; nafasi katika shule kwa kila atakayefaulu kuingia Kidato cha Kwanza 2025, miaka minne ya sekondari ya awali bila ada, miaka miwili ya Kidato cha Tano na Sita bila ada, Chuo cha Ufundi katika kila Wilaya kwa mtakaochagua njia hii na mikopo ya Elimu ya Juu kwa mtakaofaulu kwenda Vyuo Vikuu.

Kazi hii inakwenda sambamba na kuendelea kuboresha sera za uchumi wetu ili uweze kuzalisha fursa zaidi kwa kila mmoja wenu kadiri mnavyoendelea kukua na kuingia katika nguvu kazi.

Mwenyezi Mungu awaongoze.

IMG-20240911-WA0090.jpg
 
Kutokana na Utekaji watoto wameshindwa hata kujua kama amewatakia heri
 
Sote tunawatakia matashi mema watoto wetu hao, na ahadi za mh rais kama alivyo eleza ni nzuri na zenye kufaa , wasiwasi ni kwamba utekelezaji ni mdogo na pengine haupo isipokuwa political propaganda!

Watoto milion moja na laki mbili ni wengi kwa kiasi chake , hao milioni na kitu wanaofikia hata robo ya kilele cha mafanikio ni asilimia chini moja.

Wengi watakuja kuungana nasisi kulaumu, kulalamika , kutukana na kila neno baya watatoa na yote ni kwa sababu ya sera zisizo rafiki, na zisizo na vision.
 
Back
Top Bottom