Rais Samia Hassan Suluhu wapunguzie adhabu Wafugwa hawa

Rais Samia Hassan Suluhu wapunguzie adhabu Wafugwa hawa

Notorious thug

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2021
Posts
2,817
Reaction score
10,667
Poleni na majukumu ya kila siku wana jukwaa.

Wiki mbili zilizopita nilikua Kanda ya Kaskazini mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Tanga nilipata bahati ya kutembelea Magereza ya Karanga(Kilimanjaro-Moshi) Kisongo(Arusha) na Maweni(Tanga) niliona vijana wadogo umri miaka 19-23 wakiwa gereza washahukumiwa katika kudodosa dodosa kati yangu na baadhi ya Maaskari Jela wengi wa wale Vijana wanatumikia vifungo virefu miaka 30 hadi maisha kwa makosa ya dawa za kulevya(Bangi na Mirungi) ambapo kwa mujibu wa sheria ya kupambana na kudhibiti madawa ya kulevya Tanzania(Marekebisho-2017) Wengi wamejikuta wakitiwa hatiani na kuhukumiwa vifungo virefu.

Ombi langu kwako Raisi Samia Hassan Suluhu naomba uwaangalie kwa jicho la huruma wale wote waliokwisha kutumikia kuanzia miaka 5-10 waweze kuandaliwa utaratibu maalumu wa kuachiliwa huku vienendo yao ikifuatiliwa wengi wanajutia makosa waliyoyafanya na wapo tayari kubadilika. Kutokana na kesi hizi wengi wameuza Viwanja na Nyumba kuhonga kumaliza kesi ila imeshindikana Familia,Wazazi na ndugu wamekua Maskini kutokana na kesi hizi.

Kwako Raisi Samia Suluhu naomba usikilize kilio hichi cha Vijana wako walioko Magerezani wanakulilia Mama wanaomba waione tena nuru Magereza imewafundisha wanajutia makosa yao pia Mama angalia na Wazee waliopo Magerezani na Walemavu waliopo magerezani wape msamaha waje kuliona jua uraia wakielekea mwishoni mwa maisha yao.
 
Poleni na majukumu ya kila siku wana jukwaa. Wiki mbili zilizopita nilikua Kanda ya Kaskazini mikoa ya Kilimanjaro,Arusha na Tanga nilipata bahati ya kutembelea Magereza ya Karanga(Kilimanjaro-Moshi) Kisongo(Arusha) na Maweni(Tanga) niliona vijana wadogo umri miaka 19-23 wakiwa gereza washahukumiwa katika kudodosa dodosa kati yangu na baadhi ya Maaskari
Nadhani ili kuacha kutegemea 'huruma' ya kiongozi, ni vyema sheria irekebishwe katika hilo la muda wa kutumikia kifungo
 
Hao wengine wakija uraiani ni maafa tu.

Watandeleza walipoishia, na kuhakikisha wanalipiza kisasi kwa yale waliuotendewa
 
Wewe hao wahalifu wakitolewa wataleta uharibifu. Inaonekana una ndugu yako unamtafutia aachiwe.

Wahalifu kwao ni jela.
 
Aisee ukiona kijana mdogo amefungwa jela, au kifungo cha muda mrefu fikiri mara mbili, wazazi, walezi wake na majirani walichoka kabisa wakaona bora aende jela. Kuna watoto ni hatari sanaa ni watukutu vibaya sana. Naamini wako wachache wanastahili msamaha ila wengi wao ni moto wakitoka mtaa utawatambua.
 
Vifungo kama hivyo walaitakiwa wafungwe mafisadi na wala rushwa sugu. Kuwafunga vijana wanaojihusisha na bangu, ni uonevu mkubwa!

Maana bangi hiyo hiyo ukienda kwa mabeberu, ni bidhaa muhimu! Sasa iweje kwetu iwe haramu? Mashoga na wasagaji wanaachwa tu bila ya kuchukuliwa hatua! Ila wapiga ganja, wanafungwa miaka 30 jela!
 
Jela ni kubaya,kama wamejifunza na kujutia makosa yao,naunga mkono hoja wasamehewe na warudi uraiani kulijenga taifa.
 
Wanaiba mabilioni hata hwafugwi,Ila waliodakwa wa kivuta bangi miaka 20 jela ,dah
Sheria hii imekaa kiuonevu zaidi mabwana wa madwa ya kulevya yaani drug lords wanajulikana hawaguswi punda na wavuta misokoto ndio wamejaa magerezani pamoja na waliobambikiziwa kesi na polisi
 
Back
Top Bottom