Rais Samia hawezi kushinda urais 2025 kirahisi kama Wakurugenzi na Tume ya Uchaguzi watadhibitiwa

Kwa katiba hii Samia ataenda hadi twenty thirty bisha at your own risk
 
Kwamba unakataa mtaani hali sio ngumu?
 

Kwa bahati mbaya sioni wapiga kura kujitokeza kwa wingi tena kwani box la kura limepuuzwa rasmi. Mnaweza kuzungumzia kushinda, ila sio kwa idadi ya wapiga kura kama wapiga kura. Nina hakika wapiga kura watakuwa wachache kuliko kipindi chochote ndani ya nchi hii. Wengi wa watakaojitokeza kupiga kura ni wenye uelewa mdogo.
 
Wenye uelewa mdogo ni wachache, wengi wa watakaopiga kura ni wale wanaofaidika moja kwa moja na mapinduzi ya kilimo yanakwenda kufanyika nchini.

Wengi wa watakaopiga kura ni wale wanaojishughulisha na maisha halisi huko mtaani. Mimi na wewe wa mitandaoni huwa hatuoni maana ya kupiga kura, tunaishia kulalamika huku tukizeeka na malalamiko yetu.
 
Ngoja chodomo waendeleee kujiaminisha kwenye mitandao πŸ˜„πŸ˜„

Sio tuu Kilimo bali wamama kwa maelfu watampigia kura kwa sababu anawapa ile mikopo isiyo na riba kupita Halmashauri na Banks,amewatua ndoo kichwani na kuwajengea vituo vya afya .
 
Kina Tindo wanakariri maisha hawajui kuwa kuna mabadiliko makubwa ya kimtazamo yanayoendelea ndani ya CCM hivyo nchi nzima.

Huyu ni rais mwanamama, anayo huruma ya asili, hana kiburi wala hana ule ujinga wa kutaka kuwakomoa baadhi ya watu wanaokupigia kura.
 
Mama akimaliza miradi ya Mwendazake atashinda kirahisi maana maisha yatakuwa mazuri ila miradi ikimshinda wapinzani ndani na nje ya chama chake watatumia kigezo cha kudai "tumechoka kuongozwa na mwanamke"

Hii ni nchi ya mfumo dume na wanaume wengi wametii katiba tu ila mioyo yao inaungua na kwasasa maji yametuama walafi wa urais wanahesabu miaka tu amalize waanze kumnanga na kumparura!!

Mama needs to go extra miles!!
 
Sio kila mwaka ni 2020. CCM ikidhibitiwa wizi wake inashindwa.

Wizi unafanywa kwa kutumia vyombo vya dola na usalama, utadhibiti vipi? Tungekuwa na vyombo vya dola vinavyofuata sheria hapo sawa, lakini hivi vyombo vya dola vinavyomtii rais labda kutokee machafuko.
 

Hayo mabadiliko ya kimtazamo ni kwakuwa vyama vya upinzani hasa CDM hawafanyi ushawishi wake kwa umma. Lakini sasa hivi CDM wakianza uhamasishaji na watu wakajaa, utaona yale yale. Inshort CCM sio chama cha kizazi hiki, na kwa bahati mbaya hakikubaliani na ukweli huo, ndio maana kinatumia vyombo vya dola kukaa madarakani kwa shuruti.
 
Hao raia wa kawaida/wauza karanga wana uwakilishi wa nguvu ndani ya kamati kuu ya CCM? Huko ndiko Rais wa Tanzania anateuliwa na kusimikwa. Kule kwa Mahera ni bra bra tu na ulaji vinafanyika.
 

Sibahatishi ninachoongea, nimeona ni kwa kiwango gani watu hawajitokezi kupiga kura, na ule uhayawani uliofanyika 2019 uchaguzi SM, na 2020 uchaguzi mkuu ule ndio rasmi ulikata rasmi hamu ya wananchi kupiga kura. Chungu za chaguzi zote za marudio zilivyokuwa na wapiga kura wachache, na chaguzi nyingine za marudio zitakavyokuwa na wapiga kura wachache.

Kwa huku bara wangalau CDM wakiamua kushiriki uchaguzi unaweza kuongeza idadi ya wapiga kura, lakini wasiposhiriki ndio utaona idadi ya wapiga kura halisi ambao ndio huwa wanaipa kura CCM, na hawa kimsingi huwa ni wachache kisha wanajazia na za wizi.
 
Hujui nguvu ya umma. Ipo siku itanyanyuaka hata hao wanausalama watakubali.

Hilo la nguvu ya umma liko kwenye watu kususia uchaguzi, lakini la kuingia mtaani sio leo wala kesho kwa woga huu uliopo.
 
Uwadhibiti WAKURUGENZI walioteuliwa na Mama ili wamdhibiti Mama Mwenyewe??? 🀣 🀣

Ndo maana tunataka SERIKALI ya Majimbo yaani hawa Wakurugenzi wawe wanaajiriwa na Jimbo husika yaani ukiharibu Serikali ya Jimbo ndo ikushtaki na hakuna tena ishu ya UHAMISHO kama hii ya CCM kufunikiana madhambi.
 
Zipo sababu nyingi zenye kuchangia upungufu wa wapiga kura, sio ajabu uchaguzi ujao idadi ya wapiga kura ikaongezeka kulinganisha na miaka iliyopita.

Bajeti ya kilimo kutoka bilioni 200 mpaka bilioni 700 ni ongezeko kubwa sana, linakwenda kugusa sekta nyeti sana, inayogusa maisha ya watanzania wengi.
 
Hata CDM sio wa kizazi cha sasa wanapitwa na wakati kila kukicha. Mbinu zao hazibadiliki bora hata CCM wanao uzoefu wa kushughulika na watu wakiwa na jukumu la kuongoza nchi, kulinganisha na CDM.

Uongozi wa CDM tangu 2004 ni ule ule, miaka 18 sasa endeleeni kujidanganya kwamba nyinyi ni chaguo la kizazi kipya wakati huo CCM wanafanya mapinduzi ya kimtazamo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…