Pre GE2025 Rais Samia hazijui 4R zake mwenyewe, Reform anayosema Mh.Lissu ni kati ya zile 4R!!

Pre GE2025 Rais Samia hazijui 4R zake mwenyewe, Reform anayosema Mh.Lissu ni kati ya zile 4R!!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
images (2).jpeg


Hii nchi na viongozi wake wanasikitisha sana. Moja kati ya 4R alizokuja nazo Rais Samia ni Mabadiliko (Reforms). Samia alisisitiza mabadiliko katika sekta mbalimbali ili kuboresha maisha ya wananchi.

Katika maendeleo na maisha ya wananchi huwezi kuweka pembeni Siasa. Siasa ndio inaamua hatma ya maendeleo na maisha ya wananchi. Katika siasa huwezi kuweka pembeni Uchaguzi. Uchaguzi ndio mkakati mkubwa wa wananchi kuchagua watu wa kuwaletea maendeleo. Kwa lugha rahisi ni sekta muhimu.

Sekta ya siasa na uchaguzi limekuwa eneo linalopigiwa sana kelele sio tu na upinzani bali hata CCM kwenyewe wameonyesha kuna mapungufu. Wote tumesema uchaguzi wa 2020 ulikuwa wa hovyo kabisa na ulizaa chuki kubwa na kusababisha majeraha. Maana yake ilihitajika Reform ikiwa integrated na R nyingine ya Maridhiano.

Ajabu ni kwamba yule mtu anayemkumbusha Rais Samia juu ya Reform anaonekana kituko. GT tunajua Tundu Lissu hana jipya kuhusu Reform kwa sababu ameiba kwenye 4R za Mama. Researchers tunasema Lissu kafanya Plagiarism kwa Mama (maana hakuwahi ku-acknowledge).

Ajabu ni kwamba Mama mwenyewe anashangaa huyu Tundu Lissu vipi anayatoa wapi haya mambo ya ajabu? Waliofuatilia bunge maalumu la katiba wanakumbuka jinsi Mwakyembe alivyogeuka kituko. Kwenye tafiti yake aliandika mambo mazuri kuhusu serikali tatu. Lakini ajabu lilipokuja suala la utekelezaji kikatiba akaipinga serikali tatu. Hiki ndicho anachofanya Rais Samia, kwenye makaratasi ameandika 4Rs ikiwemo Maridhiano na Mabadiliko lakini anapotakiwa kutekeleza anashangaa hivyo ni vitu gani!

My Take
Nimekuja hapa kuwakumbusha tu. Sina ushauri wowote kwa sababu naelewa The governance of this country is damaged beyond repair

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
4Rs ulikuwa ni uhuni wa s100 kupata nafasi kidepromasia kwamba anashirikiana na wapinzani ili apate mikopo. Ila kiuhalisia hajui hata maana ya reforms.
 
Zile 4R zilikuwa porojo tu, kilichofuatia sote tunakijua Uchafuzi wa Serikali za Mitaa.
 
viongozi wetu wanapewa ajenda na wanakaririshwa japokuwa wanakuwa bado hawajazielewa vizuri.....zinaimbwa tu kama mapambio 😛
 
Kwa akili za wana ccm walio wengi. Yumkini hata huyo mama hazijui kabosa hizo 4 R
Ni kama vile DR. MOHAMED SEIF KHATIBU AREHEM) alivyoshindwa kughani kitabu chake cha fungate hadhani.
Ni lawaida kwa WANA CCM
 
Reform sio jambo la siku moja, hata mambo yanayofanyiwa reform, pia yanaweza kuhitaji reform, it's an on-going process
 
Back
Top Bottom