Rais Samia, ili hali itulie ndani ya CCM, ukiteua Katibu Mkuu mpya mwambie Makonda huyo ni bosi wake na amheshimu

Rais Samia, ili hali itulie ndani ya CCM, ukiteua Katibu Mkuu mpya mwambie Makonda huyo ni bosi wake na amheshimu

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Usipofanya hivi hata ukiteua Katibu Mkuu mpya wa CCM (kama hizi taarifa za Daniel Chongolo kujiuzuru kama Katibu Mkuu wa CCM Taifa) ni za kweli basi utakuwa hakuna Ulichokifanya na ni sawa tu umepaka Rangi Upepo.

Rais Samia na Mwenyekiti wa CCM Taifa acha kumuonea Aibu Paul Makonda (Katibu Mwenezi na Itikadi CCM) na mwambie kuwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa ndiyo boss wake vinginevyo unavyompa jeuri na kiburi Makonda unaanza kukigawa chama, kutengeneza chuki na makundi na si ajabu hata ukakipasua Chama, hujuma za wenyewe kwa wenyewe zikaanza na zikaja Kukuathiri hadi na wewe pia.

Kuwa nalo makini sana hili Mama.
 
Back
Top Bottom