Rais Samia, kuna Fursa nyingine huko 'Kazungula Bridge'

Rais Samia, kuna Fursa nyingine huko 'Kazungula Bridge'

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Amani iwe nawe Mama yangu.

Heri ya sikukuu ya Eid! Na Polee na uchovu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan.

Kama nilivyotoa commitment ya kukuunga mkono Mara tu ulipochukua kiti cha kuongoza nchi yetu, leo napenda kuleta mada nyingine ya ushauri kwako ili tuutumie katika kuijenga na kuipeleka mbele kimaendeleo Tanzania yetu.

Hivi Karibuni, Botswana na Zambia wamezindua daraja la kuunganisha nchi zao linalojulikana kama Daraja la Kazungula. Daraja hili lililojengwa katika Mto Zambezi Lina njia za Magari kwa ajiri ya Magari na Pia wameweka sehemu ya kupitisha reli kwenye njia hii.

kukamilika kwa Daraja hili inaelezwa kuwa ni fursa adhimu ya kiuchumi kwa nchi zenye Bandari kuu za bahari hasa South Africa, Namibia na Tanzania kwa sababu daraja hili litazifanya hizi nchi kufanya biashara kwa kiwango kikubwa sana na kwa urahisi sana.

Tukiacha Namibia na South Africa , kwa Tanzania , nimeona kukamilika kwa daraja hili ni fursa kubwa sana ya kukua kiuchumi kwa Taifa letu endapo tu tutatumia hii kama fursa na kujitengeneza ki strategically hasa ukizingatia tukijipanga vizuri, mizigo yote ya Botswana na Zambia kutoka Middle East na Mashariki ya Mbali hasa Ulaya Mashariki na Asia( China na Japan) inaweza kuwa inapitishiwa Bandari zetu( Dar es Salaam na Bagamoyo Kama itajengwa) na kupelekwa kwao.

Hivyo kutokana na hii fursa, naomba serikali yako ianze kujipanga kufanya yafuatayo either yenyewe kama yenyewe au kwa kushirikiana na sekta binafsi.

1. Kujenga Bandari kubwa Kavu katika Mkoa wa Mbeya au Songwe, itakayokuwa inapokea mizigo yote Kwa ajiri ya nchi za DRC, Zambia, Zimbabwe na Botswana. Bandari hii itapokea mizigo hiyo kwa njia zote( Barabara na Reli kutoka Dar es Salaaam na Bagamoyo hapo badae

2. Kujenga upya miondombinu ya Mikoa ya Songwe na Mbeya. Naomba kwenye kufanikisha hili Mama yetu, angalia hata Kwa kufanya kupitia PPP( Kushirikiana na sekta binafsi) miundombinu ya kuingia Mbeya na Songwe hasa barabara ifumuliwe na kujengwa upya kwa viwango vya kisasa. Miji hii ina barabara nyembamba sana. Kuanzia Makambako hadi Mbeya na Songwe. Naomba mipango na utekelezaji uanze kufumua na kuzijenga kisasa katika viwango vipya vya ubora barabara hizi. Kwenye upana kuanzia makambako hadi songwe( Tunduma) na kuweka barabara zenye njia 3-4 kila line kwenye miji ya Mbeya na Tunduma ili kurahisisha usafiri wa abiria na mizigo. Kumbuka Mama njia hii ndo imeshika uchumi wa usafirishaji kwa Tanzania.

3. Mpango wa kuibadilisha reli ya TAZARA kutoka ilivyo kuwa SGR inayotumia umeme. Naomba kwa mipango ya badae reli hii inayofika Hadi Zambia iangaliwe kubadilishwa iwe kwenye mfumo wa SGR. Iboreshwe na kujengwa upya kisasa kwa viwango vipya vya ubora (SGR)

Mwisho ingawa wazo hili linaweza kuonekana la kufikirika zaidi kuliko uhalisia naomba Serikali yako ianze kufanya mipango ya kujenga daraja linalokatisha Ziwa Tanganyika na kuingia Congo Moja kwa Moja. Ninajua Kuna changamoto kubwa sana hasa kwenye kina cha lile ziwa Ila kwa kiwango cha teknolojia kilivyofika duniani Nina uhakika wapo watu wanaoweza kufanikisha hili. Ikiwa tutajenga kwa upande wa Rukwa sawa na ikiwa tutajenga kwa upande wa Kigoma sawa Ila naomba iyo mipango ianze sasa. Hata usipokuja kujenga wewe kama Rais wa Awamu ya Sita ila siku moja Rais mwingine atajenga tu. Kikubwa naomba uanzishe hiyo mipango kwa hata kufanyika feasibility studies na kuangalia ni watu gani wataweza kufanya hivyo huko mbeleni. Nasema hivi Kwa sababu, kama Tanzania, tukiweza kupata direct access ya kuingia Congo kibiashara itakuwa na faida kubwa sana kiuchumi kwa Taifa letu kuliko kutegemea kuingia kule kupitia nchi zingine jirani.

Naomba kuwasilisha.

13DD9BAA-32BB-4DBA-BD58-EB2A8EAB12A3.jpeg
5CA1FCFD-7489-46EC-8B23-DD4404290977.jpeg
7D144653-7319-49C0-8F6D-0009F0558ACA.jpeg
 
Pamoja na kwamba umewaza mambo ya kimaendeleo lakini mengi ya uliyowaza kiuchumi hayana tija kwa nchi..kwanza si rahisi kuzifanya Botswana hata malawi kutegemea port za Tz eti kwa kupokea bidhaa zinazotoka mashariki ya kati, south afrika ina kila kitu ambacho nchi hizi zinahitaji, lkn hata tu mila, desturi na utamaduni wa watu wa nchi hizi wanajisikia vzr zaidi kushirikiana na south africa kuliko kutegemea east africa.

Daraja la kazungula limejengwa kuziwezesha nchi za kusini zishirikiane zaidi kibiashara, itakuwa ni kupoteza rasilimali za nchi kutaka kushindania soko la nchi za kusini. Tz inazungukwa na nchi 8 je tayari fursa zilizopo kwny nchi hizo imezitumia kikamilifu? Kama bado basi vyema nguvu kubwa ielekezwe huko na si kucheza pata potea unayopendekeza wewe.
 
Kwani mis

Kwani mishahara imeshaongezeka?

Mzunguko wa fedha je umshakua mkubwa au?

Wewe hapa ulilalamika kwamba miladi imkubwa imehalibu uchumi sasa leo unakuja kutaka miladi wakati zamani mliikosoa
Tuwaeleweje sasa.
 
Samahani ndugu, hiv unavyoaddress haya uliyoandika kwa Rais una uhakika yanamfikia au unajua kuwa humu kuna chawa wake au umemtumia physical letter ama kivipi vipi.

Na sio wewe tu naona watu wengi wanapenda kuandika humu kwa kuaddress public figures as if wanaongea nao muda huo huo, hapo hapo au kama wanacomment kwenye posts zao, au mimi ndio sijui mnachomaanisha?🤔🤔🤔

Naomba mnieleweshe!

Thanks!
 
Pamoja na kwamba umewaza mambo ya kimaendeleo lakini mengi ya uliyowaza kiuchumi hayana tija kwa nchi..kwanza si rahisi kuzifanya Botswana hata malawi kutegemea port za Tz eti kwa kupokea bidhaa zinazotoka mashariki ya kati, south afrika ina kila kitu ambacho nchi hizi zinahitaji, lkn hata tu mila, desturi na utamaduni wa watu wa nchi hizi wanajisikia vzr zaidi kushirikiana na south africa kuliko kutegemea east africa...
Kuwekeza kimiundombinu kwenye mikoa ya Songwe na Mbeya inayohudumia nchi za Zambia, Malawi, Congo na Sasa Botswana zinazobeba uchumi wa biashara Tanzania ndo unadai ni kucheza pata potea??? Utakuwa una mtindio wa Ubongo si bure wewe
 
Mama ameshasema anapitia mitandao. Hivyo hata tukimuandikia humu yanafika tu! Dunia ipo kiganjani saivi bwashee
Samahani ndugu, hiv unavyoaddress haya uliyoandika kwa Rais una uhakika yanamfikia au unajua kuwa humu kuna chawa wake au umemtumia physical letter ama kivipi vipi. Na sio wewe tu naona watu wengi wanapenda kuandika humu kwa kuaddress public figures as if wanaongea nao muda huo huo, hapo hapo au kama wanacomment kwenye posts zao, au mimi ndio sijui mnachomaanisha?🤔🤔🤔
Naomba mnieleweshe!
Thanks!
 
Wewe si ulikua unampinga mwendazake analeta maendeleo ya vitu sio watu imekuaje tena mkuu ghafla na wewe unataka maendeleo ya vitu
Nilichopinga ni ujenzi wa uwanja wa ndege kijijini Chato Kwa mamilioni ya fedha za walipakodi bila Bunge kuindhinisha. Hadi Leo napinga na kulaani yale matumizi mabaya ya fedha yaliyolitia hasara Taifa letu!
 
Niliwai kulalamika wapi kuhusu mradi kama Stigglers au SGR??? Acha kuchanganya mafile. Hoja zangu zilikuwa kupinga miradi ya chato Kwa sababu yale yalikuwa matumizi mabaya ya fedha za wananchi Kwa sababu haikuwa na faida.

hoja zangu zilikuwa ni kutesa watu kwa kigezo cha miradi pia
Kwani mis

Kwani mishahara imeshaongezeka?
Mzunguko wa fedha je umshakua mkubwa au?

Wewe hapa ulilalamika kwamba miladi imkubwa imehalibu uchumi sasa leo unakuja kutaka miladi wakati zamani mliikosoa
Tuwaeleweje sasa.
 
Kuwekeza kimiundombinu kwenye mikoa ya Songwe na Mbeya inayohudumia nchi za Zambia, Malawi, Congo na Sasa Botswana zinazobeba uchumi wa biashara Tanzania ndo unadai ni kucheza pata potea? Utakuwa una mtindio wa Ubongo si bure wewe
Nmesoma akili yako imevutiwa kuona daraja la kazungula ukaokota okota mawili matatu kuonyesha Tz inaweza faidika na uwepo wa hilo daraja. Kiuhalisia HAIWEZEKANI layman tu ndio anaweza fikiri uliyoandika..fursa za east africa hatujazitumia licha ya uwepo wa miundombinu wezeshi..barabara, reli na usafiri wa majini, halafu unawaza ya mbali ambako hatuwezi kufika huo ni zaidi ya ujinga.
 
Ushauri mzuri wa kimaendeleo.

Ni mzuri lakini hauna tija ya kiuchumi, huko anakotaja ukumbuke kuna Bandari za Afrika kusini, Namibia, Angola na sisi bado Upande wa bandari hatuna ufanisi kwani malalamiko kwa nchi tunazohudumia ikiwapo Malawi yenyewe, Burundi, Rwanda, mashariki ya Congo na Zambia bado wanatulalamikia sana juu ya ufanisi plus usumbufu, nadhani tungejikita hapo tungefika mbali sana maana geografia ya Tanzania Mwenyezi Mungu alitupendelea sana,
 
Nmesoma akili yako imevutiwa kuona daraja la kazungula ukaokota okota mawili matatu kuonyesha Tz inaweza faidika na uwepo wa hilo daraja..kiuhalisia HAIWEZEKANI layman tu ndio anaweza fikiri uliyoandika..fursa za east africa hatujazitumia licha ya uwepo wa miundombinu wezeshi..barabara, reli na usafiri wa majini, halafu unawaza ya mbali ambako hatuwezi kufika huo ni zaidi ya ujinga.
Braza kumkosoa mtu kwa staili hiyo inaonesha wewe pia ni mjinga na ridiculously emotional, kama angekuwa amefanya hiyo kitu mara kadhaa licha ya ushauri it could have been worth it! Tunaweza kweli tukawa na great thinkers lakin wenye disparities kama zako! Change!
 
Tungekua na Bandari kavu hata singida Malori ya Rwanda na Burundi yakaishia pale, inamaana tungeweza kuaccomodate mizigo mingi ya Uganda pia maana umbali ungekua umepungua na hapo tungewanyemelea Sudan kusini kwa hivo reli na mabehewa ya express ya kusogeza mizigo kutoka Dar port hadi mfano dry port singida ingekua kitu kizuri sana
 
Mada nzuri mno welldone mtoa hoja ILA daraja hili la Kazungula ni bad news kwetu,sasa DRC itasukuma zaidi Mizigo kule kuliko kuileta hapa Dar es salaam port,tumechelewa mno maana future ya Africa kibiashara ni DRC
 
Back
Top Bottom