Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Habari ni kuwa Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hasssan Mwenyekiti wa CCM Taifa, ambaye pia ndiye Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama, ataongoza vikao vya Kamati kuu na Halmshauri kuu ya CCM Taifa Tarehe 29 na 30 Mwezi huu jijini Dar.
Vikao hivyo vitatanguliwa na vikao vya Secretarieti ya CCM vitakavyoketi na kufanyika Tarehe 27 na 28 Mwezi huu jijini.
Chama ni vikao, huko ndiko masuala mbalimbali huzungumzwa na mipango na mikakati mbalimbali kuwekwa katika kukiimarisha chama na kukipa nguvu kuanzia ngazi ya shina, Tawi, kata, wilaya, mkoa mpaka Taifa ndio maana CCM Inaendelea kuimarika na kuwa na nguvu kila uchwao.
Tofauti na vyama kama CHADEMA vinavyoendelea kudumaa kila uchwao na kupoteza muelekeo,vinakwenda tu utafikiri gari lililokatika breki pamoja na usukani.hakuna cha utaratibu wala mfumo unaoeleweka ,ndio maana unakuta kila mtu anajadili na kuweka msimamo wake juu ya jambo fulani kupitia ukurasa wake wa kijamii Kabla hata ya vikao rasmi vya chama.
Utaona kiongozi huyu anatoka hadharani mbele ya camera anaongea mambo yaliyotakiwa kuzungumzwa na kujadiliwa kwenye vikao vya ndani vya chama,anaita waandishi wa habari na kuanza kuzungumza yanayomjia kichwani mwake tu bila breki ya mdomo.
utoto wa namna hiyo huwezi kuukuta ndani ya CCM wala kuona au kusikia ukifanyika..ndio maana CCM kinaitwa chama kiongozi na tumaini la watanzania.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Habari ni kuwa Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hasssan Mwenyekiti wa CCM Taifa, ambaye pia ndiye Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama, ataongoza vikao vya Kamati kuu na Halmshauri kuu ya CCM Taifa Tarehe 29 na 30 Mwezi huu jijini Dar.
Vikao hivyo vitatanguliwa na vikao vya Secretarieti ya CCM vitakavyoketi na kufanyika Tarehe 27 na 28 Mwezi huu jijini.
Chama ni vikao, huko ndiko masuala mbalimbali huzungumzwa na mipango na mikakati mbalimbali kuwekwa katika kukiimarisha chama na kukipa nguvu kuanzia ngazi ya shina, Tawi, kata, wilaya, mkoa mpaka Taifa ndio maana CCM Inaendelea kuimarika na kuwa na nguvu kila uchwao.
Tofauti na vyama kama CHADEMA vinavyoendelea kudumaa kila uchwao na kupoteza muelekeo,vinakwenda tu utafikiri gari lililokatika breki pamoja na usukani.hakuna cha utaratibu wala mfumo unaoeleweka ,ndio maana unakuta kila mtu anajadili na kuweka msimamo wake juu ya jambo fulani kupitia ukurasa wake wa kijamii Kabla hata ya vikao rasmi vya chama.
Utaona kiongozi huyu anatoka hadharani mbele ya camera anaongea mambo yaliyotakiwa kuzungumzwa na kujadiliwa kwenye vikao vya ndani vya chama,anaita waandishi wa habari na kuanza kuzungumza yanayomjia kichwani mwake tu bila breki ya mdomo.
utoto wa namna hiyo huwezi kuukuta ndani ya CCM wala kuona au kusikia ukifanyika..ndio maana CCM kinaitwa chama kiongozi na tumaini la watanzania.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.