Rais Samia, maisha ya vijana kwa sasa hayaridhishi. Nguvu kubwa itumike kubadili mfumo wao wa maisha

Mkuu uwezi kusema jambo lolote linaloikumba nchi hii kwa sasa ukawasahau CCM na siasa kwa ujumla kwasababu ata Rais uliyempa hizo nondo apo juu anafata ilani ya chama......
Hakuna nchi kwenye ulimwengu huu inatawaliwa bila vyama. Hicho ni kitu kinacho eleweka. Labda kama nchi inatawaliwa kifalme. Kwa maana hii namaanisha kuwa viongozi wote kwenye karne hii ambao nchi zao ni member wa UN wamekuwa elected democratically.

Sasa nikija kwenye maelezo ya hoja yako kuhusu vyama, ninachoweza kukueleza ni kuwa kiongozi yoyote anapochaguliwa na nchi yake kuwa kiongozi wa serikali, yeye kuanzia hapo anakuwa ndiye mwajibikaji kwa mwenendo mzima wa maendeleo ya nchi yake kwa mujibu wa katiba, sheria za nchi na pia utashi wake, usilisahau hili.

Nikupe tu baadhi ya mifano ambayo pengine inaweza kukusaidia kunielewa vizuri;
1. Watendaji wa serikali kama mawaziri, manaibu waziri, makatibu, wakurugenzi na kadhalika wanachaguliwa na Rais mwenyewe na sio chama.
2. Policy ya serikali yeye ndiye anaamua iwe ya aina gani na sio chama.
3. Priorities ya mambo ya kufanya, yeye ndiye anayeamua nini kifanyike kwanza na kipi baadae na kama kweli kitafanyika.

Niendelee zaidi. Nikimchukulia Hayati Rais Magufuli, ndiyo chama chake kilipendekeza au kiliweka sera ya kununua ndege. Hakikuweka sera ya kununua ndege za aina gani. Tumepata ndenge kutokana na utashi wa Hayati Rais Magufuli mwenyewe.

Chama kilipendekeza kuwa na SGR lakini hakiku-specify SGR ya aina gani. Ni maamuzi ya Hayati Rais Magufuli na serikali yake kuwa na SGR ya umeme. Bwawa la Nyerere na miradi mingine mingi kama; daraja la Kigongo-Busisi, Ubungo Flyover, Newe Surrender Bridge na kadhalika na kadhalika. Ningeweza kuendelea hivi kwa mifano mingi zaidi lakini naona ngoja niishie na hiyo, nikitegemea kuwa umenielewa, kwanini sijazungumzia mambo ya chama wala itikadi za chama. Kwani maamuzi mengi yanafaywa na Rais aliyepo madarakani
 
Asante sana mkuu kwa hoja yako iliyo jaa hekima na maswali mengi juu ya mada yangu.

Nianze tu kujibu kwa uzuri na hekima yangu kwako kwa madai au lawama ulizozitoa juu ya mada yangu kama ifuatavyo;
Kama kweli umeisoma vizuri na kuelewa nilicho kidhamiria nadhani usingekuja na lawama hizo. Ni kweli theme kubwa ya mada yangu ilikuwa ni ajira kwa vijana na niliendelea kutoa maelezo kwa undani kidogo juu ya hatua za kuchukua ili kufikia lengo hilo. Nadhani katika hili huku ni quote vizuri.

Mimi sijamsifu Hayati Magufuli peke yake bali nimewasifu wote kwa jitihada zao za kujenga miundo mbinu ya usafiri na uchukuzi, elimu na afya. Kwenye ile clip ya Hayati Magufuli nililenga kwenywe swala la chuma. Sio kumsifu yeye.

Na nikaendelea kusema kuwa pamoja na jitihada kubwa hizi za kutoa huduma, bado mkazo mkubwa ulitakiwa uwekwe kwenye kujenga misingi bora ya kuhakikisha vijana wanapo maliza masomo yao na kupata knowledge za kinadhalia shuleni na vyuoni, serikali ilitakiwa pia kuwa na mkakati kabambe wa kushirikiana na sekta binafsi na Diaspora katika kuwekeza kwenye viwanda ambavyo vitawawezesha vijana wetu kupata maarifa mapana zaidi kwa vitendo kwenye hivyo viwanda.

Siafiki kitendo cha kuwaacha vijana pindi wanapo maliza masomo yao kuwasweka kwenye uchuuzi wa cheap comodities za kutoka Asia, kitu ambacho kinaifanya nchi kupoteza nguvu kazi na hatimaye kujitengenezea bomu sisi wenyewe ambalo mwisho litatudhuru sisi wenyewe. Ndiyo maana nikatoa mfano wa vurugu linalo tokea Afrika ya kusini, kuwa vurugu hilo linaweza tusipoangalia likaja kwetu.

Katika hiyo mada nimejaribu pia kuelezea njia halisi ambazo zingeweza saidia kuamsha hisia za wahusika juu ya mambo ya kufanya kulingana na potential ya rasilimali nyingi ambazo tunazo.


[emoji23] [emoji23] [emoji23] Kuna mkuu mwngine pia aligusia kilimo. Any way ni kweli sijakigusa kilimo kwani, najua kilimo ni wimbo wa wanasiasa ili wapate cha kuzungumza wakiwa Bungeni. Ukweli wa mambo tunazungumzia kilimo toka taifa hili lianzishwe. Hakuna kitu ambacho kinafanyika.

Kitu kingine zingatia kuwa kilimo hakitoa ajira kubwa kama unavyofikiri. Kwa Amerika, Australia na Europe kilimo kinatoa seasonal ajira. Kama huku Europe mara nyingi watu wengi wanakuwa mashambani katika misimu ya kuvuna badhi ya mazao. Vingenevyo kila kitu kinafanywa na mashine. Chukua mazao kama mahindi. Mtama, ngano na alizeti kwa mfano. Kazi za kupanda, kuvuna na mengineyo yote zinafanywa na mashine. Na inawezekena hiyo kazi ikafanywa na familia moja tu, baba, mama na watoto wao wawili au watatu.

Labda kama unazungumzia kilimo in a classical way kama huko kwetu sawa. Huwezi ukamtoa mtu aliyesoma mechanical engineering kwenda kulima, atafanya nini kwani? Navyo jua mimi basic ya masomo yake ni kujifunza kutumia knowledge aliyoipata ku-solve natural problems technically.

Hata mashambani, ni kweli yeye anahitaji kutengeneza dhana ambazo zitamsaidia mkulima kulima au kuzalisha mazao yake kwa urahisi na bila matatizo na kwa ubora zaidi. Sasa ili awe katika position ya kuzalisha hizo dhana lazima awe na vetendea kazi. Sasa hivi vitendea kazi kama material na products nyingine ambazo atahitaji katika kutengeneza hizo dhana za kilimo atazipata wapi, wakati nchi haina infrastructure nzuri?

Ndiyo maana nikasema kuwa kwa uzoefu wangu kitu muhimu ambacho watanzania tunahitaji ni steel na dhana zinazo tokana na steel. Kama uliiangali vizuri ile video yangu ya mwisho ungetambua nini nilikuwa na maanisha kuwa na viwanda mama kwa kujenga Blast furnace yetu wenyewe na viwanda vya kuchakata chuma ambayo itatumika katika kutengeneza products nyingine.

Of course nakubaliana na wewe kuwa hayati Magufuli amechangia kwa kiasi kikubwa sana katika kutoa taswira nzuri ya mazingira ya miji kwa ku-promote umachinga, lakini zingatia kuwa kwa kipindi kile hakuwa na jinsi, ilibidi lazima afanye hivyo kwa namna moja kuondoa uonevu ambao wamachinga walikuwa wanatendewa kwenye nchi yao na wakati huo huo kujaribu kupunguza athari za matatizo ambayo yangeweza kutokea kwa kuwakandamiza wamachinga.

Kwa jinsi nilivyo mwelewa ni kwamba hili lilikuwa jambo la dharura kulifanya kuwasaidia vijana ili mipango thabiti itakapo kamilika waweze ondokana na hali hiyo. Sikubaliani na kuendeleza mfumo huu wa maisha kwa mda mrefu. Hatimaye hautakuwa na tija kwa taifa aidha.

Kuhusiana na ndege hilo nalo linaulazima wake. Ukitaka kupata wawekezaji au watalii ambao wanadhamira nzuri ya kuja kuwekeza au kutalii nchini, nchi yeye mali asili za kitalii kubwa kama Tanzania, haina budi kuwa na infrastructure nzuri ya usafiri ambayao itawawezesha hao wawekezaji na watalii kuwa na mobility nzuri. Vinginevyo usitegemee chhochote kutoka kwao.

Kama unaijua tabia ya mzungu akitaka kufanya ziara yoyote ile iwe ya ndani au nje, kitu cha kwanza anacho angalia ni usafiri, yaani mobility. Kitu cha pili ni usalama na tatu ndiyo mazingira halisi ya hilo eneo. Zaidi ya hayo ndege ni nyenzo ya kuitangaza nchi. Utaitangazaje nchi yako bila kuwa na kitu cha kumfanya mtu avutiwe na vitu vilivyomo nchini mwako?

Sikiliza ndugu yangu kama umesoma mambo ya energy cusumption nafikiri utajua pia mambo ya cost reduction, vinginevyo huwezi fanya biashara matokeo yake utajikuta unapata hasara kwani mteja hata weza lipa hiyo gharama.

Ukichukua gharama za mitambo ya kufua umeme kwa njia ya gesi asilia, utaona kuwa mahesabu ya [EFFICIENCE = OUT PUT/ IN PUT= <1 au <100%]. Maana yake ni kwamba uwiano wa nguvu za umeme ulizo zalisha kwa nguvu za gesi iliyotumika ukijumlisha na nguvu za kuchakaa kwa mitambo na kadhalika kimahesabu ni ndogo ukilinganisha na uwiano wa nguvu za umeme unazozalisha kwa kutumia nguvu zinazotokana na maji.

Kwa maana nyingine ni kwmba ili upate faida katika umeme unao zalisha ni lazima uweke kiwango cha kuwatoza wateja wako ili kuuendesha mtambo wako kwa faida itakayo kuwezesha kulipa gharama zote za uzalishaji. Kwa hiyo utaona kuwa uzalishaji wa umeme kwa mitambo ya gesi (Gas turbines) ni kubwa kuliko mitambo ya maji. Ni mahesabu mengi sana ambayo nikikufanulia kwa ufasaha itachua mehesabu na maandishi mengi. Katika mambo kama haya Usiangalie gharama za uwekezaji tu, bali angalia pia gharama za uzalishaji, uendeshaji na pia uwezo wa mlaji ku-afford kulipa. Umeme wa maji ni bei nafuu sana duniani kwote asikudanganye mtu.

Daraja la Busisi litadumu miaka karibu 100 bila kuligusa tena na litawarahisishia wafanya biashara wa kutoka kaskazini kupeleka bidhaa zao kwenye soko Mwanza na kwingine kwa bei nafuu. Halita haribu mazingira kwa kiasi kikubwa kuliko vivuko. Mobility itakuwa kubwa sana. Vivuko vinaweza poteza maisha ya watu kama tunavyojua. Umezingatia gharama za uendeshaji vivuko; vikiharibika kama maintanence na kadhalika.

Hayo mengine ya viwanda, pamba na kadhalilika sitaweza kadiria cost zake. Ila la kuzingatia tu ni kwaba hivyo viwanda hutaweza endesha bila low costs za energy. Kwasabu lazim u compete na wazalishaji wengine wa nchi nyingine.
 
KINACHOTAKIWA SS MAMA AKUBALI TU MCHAKATO WA KATIBA MPYA (RASIM YA WARIOBA) UENDELEE NA KUKAMILIKA.....Hapo tutaachana na maisha ya chama hiki (CCM) chakav.....na vingine vitakavyoshka hatam havitaishi maisha hayo tena .....hapo tutakuwa tumepga hatua kubwa sanaa Kisiasa, kiuchumi hasaaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…