Rais samia: Majeshi yataongezewa fedha katika bajeti ijayo ili wasijikite kwenye shughuli za uzalishaji

Rais samia: Majeshi yataongezewa fedha katika bajeti ijayo ili wasijikite kwenye shughuli za uzalishaji

Hatua gani tunarudi hapa? Hivi Kazi ya jeshi ni kubeba korosho na kushona viatu?

Bora wawe busy na mambo yao ya ndani ikiwemo kuzalisha zana zao wenyewe.
Haya mambo mnayafikiria kwa upeo mdogo sana, jeshi kwa nafasi yake wana uwezo mkubwa wa kuzalisha kwa wingi na bidhaa zao zikawa bei nafuu kwasababu wana man power ya kutosha, na skilled personnel, hawa watalipwa kwa mishahara yao ile ile wanayolipwa wakiwa kama waajiriwa wa jeshi.

Lakini unapopeleka shughuli kama hizi kwa watu wa nje, kwanza kuna ukiritimba, hizo tenda huko CCM watatoa kwa upendeleo mpaka wahusika wahongwe.

Hawa wahongaji nao lazima watakuja kufidia gharama hizo kwenye mauzo ya bidhaa zao, lakini pia issue ya man power, kuwaajiri wafanyakazi lazima mishahara yao itoke kwenye mfuko wa muajiri, hili nalo litachangia kuongeza bei ya bidhaa.
 
Hawa tunawalipa salary wanahangaika na ujasiriamali matokeo yake tukivamiwa wanaanza kututanguliza eti wanaume wote vitani wakati wenye kiapo na tunaowalisha kwa Kodi zetu wapo na tuliwafindisha.
Hiki ulichoandika hapa ni hisia tu, hazina uhalisia wowote.
 
Hapana, kuna kazi majeshi yanatakiwa kufanya ila sio kazi za kulima nyanya, mahindi, vitunguu n.k au kujenga nyumba, au ufundi seremela n.k. Majeshi yanayatakiwa yajikite kwenye shughuli zao kuu za ulinzi, za ziada labda ziwe utafiti, utabibu, maafa, kujenga madaraja sehemu ngumu, kutunza amani nje ya nchi
Hapa mama amekosea, au labda si msomaji au mfatiliaji...

Binadamu huendelea Kijamii au kiteknolojia kwa sababu ya vita ambayo husabisha maendeleo jeshini...

Kuna msemo unasema Enrich the Army Enrich the country.

Ukitaja nchi zote tajari Duniani kuanzia USA, Europe, Israel e.t.c maendeleo Yao yanaanzia Jeshini kuanzia tafiti Hadi implementation zote...

We need to give our armies such kinds of challenges and not to stop them. Mfano kipindi Cha Corona Hadi Sasa hakuna response ya kitaalam ya Majeshi yetu Kwa sababu hawana aina hii ya wataalaam au focus, Jeshi letu sidhani kama Ina Ina yoyote ya rapid response kama ikitokea Hatari ya kukosekana kwa hydrocarbons.

Samia ni mweupe sana kichwani
 
Haya mambo mnayafikiria kwa upeo mdogo sana, jeshi kwa nafasi yake wana uwezo mkubwa wa kuzalisha kwa wingi na bidhaa zao zikawa bei nafuu kwasababu wana man power ya kutosha, na skilled personnel, hawa watalipwa kwa mishahara yao ile ile wanayolipwa wakiwa kama waajiriwa wa jeshi.

Lakini unapopeleka shughuli kama hizi kwa watu wa nje, kwanza kuna ukiritimba, hizo tenda huko CCM watatoa kwa upendeleo mpaka wahusika wahongwe.

Hawa wahongaji nao lazima watakuja kufidia gharama hizo kwenye mauzo ya bidhaa zao, lakini pia issue ya man power, kuwaajiri wafanyakazi lazima mishahara yao itoke kwenye mfuko wa muajiri, hili nalo litachangia kuongeza bei ya bidhaa.
Tenda zimekuwa zikitolewa miaka yote kabla ya Mwendazake kuliingiza jeshi kuwa kampuni badala ya ku focus kwenye jukumu lao la msingi.

Uzalishaji utafanywa na vitengo husika kama JKT na vitengo vya magereza sio kama ilivyo sasa Jeshi zima linafukuzia tenda.
 
Tenda zimekuwa zikitolewa miaka yote kabla ya Mwendazake kuliingiza jeshi kuwa kampuni badala ya ku focus kwenye jukumu lao la msingi.

Uzalishaji utafanywa na vitengo husika kama JKT na vitengo vya magereza sio kama ilivyo sasa Jeshi zima linafukuzia tenda.
Najua tenda zimekuwa zikitolewa miaka yote, swali, hizo tenda zilizokuwa zikitolewa zilikuwa fair? hapakuwa na malalamiko?
 
Majeshi pia yakijiingiza sana kwenye uzalishaji mali huwa yanakuwa corrupt sana na kuingia hadi kwenye siasa za kiraia jambo ambalo huwa na madhara makubwa sana kwenye demokrasia, mfano mzuri ni Misri, Pakistan, na Myanmar(Burma).
 
Wakuu,
Binafsi kuna mambo mengine huwa nayatizama kwa chongo mambo mengine kwa kina na mambo mengine kwa kukurupuka. Hapa nakurupuka, hii technology tunatumia kupatiana habari- barua pepe-messeging ni product ya kurugenzi za ulinzi za merika ambapo asilimia kubwa ni wanajeshi pamoja na raia wanayofanya humo, sina uhakika na kwetu kama tuna raia.
Ushauri ambao amepata, inawezekana nae kajikita kwa kukurupuka- nasema hilo kwa sababu kwa mwaka mmoja na mambo lukuki yanayofanyika-hili jambo linahitaji tafakari nzito linahitaji coordination na hao wakuu wa majeshi n.k sasa kama hilo limetokea- mutual approach and coordination basi hilo la Mheshimiwa Raisi kutamka hivyo is just a formality ila kama amewapa sikio watu wenye kutamani products zao, yaani za Jeshi- mashamba na end products zao, basi wako tayari kujikita kwa lile linaloitwa kibiashara 'hostile takeover' kwa vile tu kuna structure nzuri wana maeneo mazuri na kuna profit za kutosheleza au mwelekeo wa kuanza kutengeneza hizo profit basi the highest bidder wins* Kwa kweli sijalitizama kwa ndani kwa vile nimekurupuka lakini the possibility kwamba wapo "mabilionea" neno ambalo sijalizoea(halizoeleki kwangu) wapo wafanyabiashara wanaotaka hayo kwa nguvu zote hence utumiaji wa hili kwangu yaani ''hostile takeover' basi sintoshangaa.
Kwani ni rahisi kwa hao mabilionea kufanya hilo mifano ipo mingi tu, hapa again nimekurupuka na natoa opinion zangu.
Kama hayo juu yakajakuwa na chembe la ukweli, ningemsii afunge sikio kwenye sehemu nyeti na ambazo zinagusa Usalama wa Taifa.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Wakuu,
Binafsi kuna mambo mengine huwa nayatizama kwa chongo mambo mengine kwa kina na mambo mengine kwa kukurupuka. Hapa nakurupuka, hii technology tunatumia kupatiana habari- barua pepe-messeging ni product ya kurugenzi za ulinzi za merika ambapo asilimia kubwa ni wanajeshi pamoja na raia wanayofanya humo, sina uhakika na kwetu kama tuna raia.
Ushauri ambao amepata, inawezekana nae kajikita kwa kukurupuka- nasema hilo kwa sababu kwa mwaka mmoja na mambo lukuki yanayofanyika-hili jambo linahitaji tafakari nzito linahitaji coordination na hao wakuu wa majeshi n.k sasa kama hilo limetokea- mutual approach and coordination basi hilo la Mheshimiwa Raisi kutamka hivyo is just a formality ila kama amewapa sikio watu wenye kutamani products zao, yaani za Jeshi- mashamba na end products zao, basi wako tayari kujikita kwa lile linaloitwa kibiashara 'hostile takeover' kwa vile tu kuna structure nzuri wana maeneo mazuri na kuna profit za kutosheleza au mwelekeo wa kuanza kutengeneza hizo profit basi the highest bidder wins* Kwa kweli sijalitizama kwa ndani kwa vile nimekurupuka lakini the possibility kwamba wapo "mabilionea" neno ambalo sijalizoea(halizoeleki kwangu) wapo wafanyabiashara wanaotaka hayo kwa nguvu zote hence utumiaji wa hili kwangu yaani ''hostile takeover' basi sintoshangaa.
Kwani ni rahisi kwa hao mabilionea kufanya hilo mifano ipo mingi tu, hapa again nimekurupuka na natoa opinion zangu.
Kama hayo juu yakajakuwa na chembe la ukweli, ningemsii afunge sikio kwenye sehemu nyeti na ambazo zinagusa Usalama wa Taifa.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Aisee !!!!!

Majeshi / Ulinzi / Vita vya sasa vinapambana/ kuendeshwa Kisayansi n.k. haviitaji manpower kubwa...., Kwahio Jeshi kuliko kula Pesa zetu za kodi kwa mlango wa nyuma kama zinaweza kuzalisha baadhi ya mambo kwanini wasifanye hivyo na kujiendesha ? Huko Magereza kwanini wasitengeneze nguo zao, furniture n.k.

Sio kwamba wapewe tenda kwa upendeleo hapana ila waingie kwenye ushindani pia wanachoweza kufanya na wafanye.., Hayo mambo ya Sekta Binafsi (Entrepreneurship kazi yako moja ni kutafuta masoko) sio kulialia serikali iwape kazi..., kama hawawezi kutafuta markets basi they are not good enough..., na Masoko sio tu ndani waende mpaka nje (mbona wengine wanakuja huku kufanya kazi zetu, kwanini na sisi tusiende) ?
 
Hizi unazosema ndio kazi za Uzalishaji, Serikali inatakiwa iwaongezee pesa wawe na uwezo wa kushindana na si kuwazuia
Majeshi yakijikite kwenye medani na uvumbuzi wa zana zinazoendana na majukumu yao....

Mambo ya uzalishaji mali waachiwe sekta binafsi na sekta zingine za umma.
 
Kwa hiyo hiyo Dunia ya kwanza hayo majeshi yanafanya hizo shughuli uraiani au ndani huko kwenye ishu zao?

Kazi ya majeshi sio kusomba korosho wala kuuza vitalu sijui kusogeza kokoto site.
We mbona umeng'ang'ania korosho tu?? huo ni ufala
 
Back
Top Bottom