Rais Samia: Mikopo ya Wahisani ina Riba kubwa

Kama Raisi Samia anaona mikopo ya wahisani inaumiza kwa kuwa na riba kubwa, alinganishe riba wanazotoza wahisani na riba zinazotozwa na benki hapa nchini, labda hiyo itamfanya aelewe kwa nini Watanzania tunashindwa kuchukua mikopo toka benki zetu nchini.

Mkuki kwa wananchi sawa lakini kwa taifa uchungu?
 
Na ni mikopo mingapi huwa wanatuambia wakiipokea? Na wanapoipangia matumizi wanatuonyesha mahesabu yake yamekwendaje? Mkuu ubarikiwe umeuliza swali fikirishi sana na lakugusa ndani kabisa.
 
Siyo kweli. Kwa mfano, Swaziland/Eswatini iko kwenye kundi la uchumi wa kati miaka kadhaa kabla ya Tanzania lakini imefaidika sana na mpango wa AGOA. Tukiri tu kwamba tuna viwanda vichache vinavyozalisha bidhaa zenye viwango vya kukubarika kwenye soko la Marekani na mataifa mengine ya Ulaya. Tukitambua udhaifu wetu ndipo tutakapoweza kubuni mikakati, mbinu na mipango ya kujinasua, siyo porojo.
 
Kwani ile mkopo wa kipindi cha Corona usiokuwa na riba wenye kuanza kulipwa baada ya miaka 10 wenzetu walipata na sisi ikawaje vile?
Nahisi kama vile Mama kavuta mkwanja.
 
Hilo la kujitegemea litawezekana vipi kwa utaratibu tulio nao? Nini haswa kitakuwa kimebadilika kama viongozi ni wa chama kile kile na mentality ile ile?

Utofauti wa upatikanaji wa pesa bado siyo solution ya kuwa na vision. Wahisani hawasikilizwi, wananchi hawasikilizwi.
 
alafu anasema eti anasimamaisha uchumi kwanza 🤣
 
Kuna 2.3 trillion ya world Bank na 1.3 trillion ya imf kwa ajili ya corona mpo hapo ?
Hivi JPM alikua anatoa wapi hela za ujenzi wa madarasa ?

Nimeuliza tu jamani
 
..anatakiwa arekebishe uchumi kwanza halafu ndio aongeze tozo na kodi.

..aliahidi kurekebisha uchumi kwasababu alikuta hali ni mbaya.

..sasa badala ya kurekebisha uchumi katuvamia na ongezeko la kodi na tozo.
 
Waseme tu hawawezi kufuata demokrasia. Wahisani wana masharti ambayo wanahofia yatawapoka madaraka na hivyo kunyang’anywa tonge mdomoni.
Amesema mkuu, mchana kweupe, video ipo humu ”siasa za CCM-Tanzania haziwezi kukubali kufuata mashariti ya WAFADHILI /MABEBERU.”

Tunatawaliwa na MAJAMBAZI.
CCM imepoteza uhalali wa kuongoza Nchi.

CCM = Chama Cha MAGAIDI
 
Na ni mikopo mingapi huwa wanatuambia wakiipokea? Na wanapoipangia matumizi wanatuonyesha mahesabu yake yamekwendaje? Mkuu ubarikiwe umeuliza swali fikirishi sana na lakugusa ndani kabisa.
Tena ni afadhali pesa za wahisani huwa wanabanwa kuhusu demokrasia nk. Za wananchi ndiyo hata hawatojali hata kidogo. Almuradi kuna polisi na wananchi hawaruhusiwi kuhoji lolote. Na pia kuwa na tume na katiba mbovu, vitu ambavyo ni nyenzo zao za kubakia madarakani. Hakuna lolote mwananchi analoweza kufanya hata wakitumia hizo pesa wanazotunyonya vibaya kiasi gani.

Ndiyo maana wengi wanataka katiba mpya ambapo kutakuwepo na accountability. Hatuwezi kujitegemea bila kuwaweka viongozi accountable kwa namna wanavyofanya maamuzi ya matumizi ya kodi zetu nk.
 
mambo kama haya unawaambia waendesha bodaboda watakuelewa kweli? waambie kuhusu kupunguza kuteswa na halmashauri, kupunguza ushuru ili wafanye shughuli zao bila kubughudhiwa
 
Mkuu unataka tuendelee kuwategemea wahisani mpaka lini?
Tungekuwa na viongozi makini, tayari ungekuta tumeshaacha kuwategemea wahisani. Tatizo la kusema hatutaki kuwategemea wahisani ni kwasababu wanajuwa kuwa wameshindwa kuondoa umasikini na kufuta ujinga. Wanaogopa Demokrasia itasababisha washindwe kujibu maswali magumu na hivyo uwezekano wa kuondolewa madarakani unakuwa mkubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…