Rais Samia na CCM kwa busara, sikiliza na ikiwapendeza mfuate ushauri huu juu ya katiba mpya

Rais Samia na CCM kwa busara, sikiliza na ikiwapendeza mfuate ushauri huu juu ya katiba mpya

JERUSALEM 2006

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
527
Reaction score
596
Mhe, Rais, Mhe. Palagamamba M.A. Kabudi waziri mwandamizi katika serikali yako mwaka 2012/13 katika viunga vya Nkurumah Hall chuo kikuu cha Dar Es Salaam, alitoa ushauri huu juu ya katiba Mpya,




Mhe. Rais, Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, na kiongozi mwandamizi katika serikali yako na sasa ni Mbunge wa kuteuliwa na wewe, Mhe. Bashiru A. Kakurwa alipata kunena haya juu ya hitaji la katiba mpya.




Mhe. Rais sitaki kukupangia wala kukulazimisha. Kwa maneno yao wenyewe waliona hitaji la katiba mpya kabla hawajawa na madaraka, baada ya kuyapata midomo yao imefungwa.

Nipende kukuhakikishia Mhe. Rais umezungukwa na wanafiki wa kiwango cha Jupiter kwenye chama chako, hakuna kiongozi ndani ya CCM kwa sasa atakayeona umuhimu wa Katiba Mpya, lakini pindi mtakapomaliza madaraka yenu na mkarithiwa na viongozi sampuli ya Jiwe ndio mnakumbuka umuhimu wa katiba mpya.

Mama kwa sasa mpini uko kwako, wembe unao wewe mama na uchaguzi ni wako wengine tutabaki kukushauri tu.
 
Hitaji la katiba mpya si kubwa sana kulinganisha na hitaji LA maendeleo ya watu. Katiba iliyopo sasa ukiacha madhaifu machache iliyonayo ni bora sana na yaweza kutuletea maendeleo. Hitaji la katiba mpya in hitaji la upinzani kuingia madarakani kwa maslahi
binafsi
 
Huyo Kabudi akili zimeamia tumboni...
 
Hitaji la katiba mpya si kubwa sana kulinganisha na hitaji LA maendeleo ya watu. Katiba iliyopo sasa ukiacha madhaifu machache iliyonayo ni bora sana na yaweza kutuletea maendeleo. Hitaji la katiba mpya in hitaji la upinzani kuingia madarakani kwa maslahi
binafsi

Kwa hiyo kwa akili zako hao ni wapinzani??
Kabudi, Bashiri na wewe na Mhafidhina wa CCM? Au nikewasingizia?
 
Tunataka umeme 24hrs, tunataka Ajira na Elimu Bora

Hayo mambo ya katiba mpya ni kikundi chenu ndio kinataka

Chadema mlipata viti vingi bungen Kwa katiba hii hii
 
Hitaji la katiba mpya si kubwa sana kulinganisha na hitaji LA maendeleo ya watu. Katiba iliyopo sasa ukiacha madhaifu machache iliyonayo ni bora sana na yaweza kutuletea maendeleo. Hitaji la katiba mpya in hitaji la upinzani kuingia madarakani kwa maslahi
binafsi

Absolutely yes
Na hata hiyo katiba mpya itakuwa na vitu ambavyo mtu mwingine hatovipenda ni kama katiba hii Tu, wengine tunapenda na wengine hawapendi
 
Siasa bila unafiki haziendi, ye mwenyewe picha anajionea baada ya mwendazake kwenda watu wanavopiga U-turn.
 
Tunataka umeme 24hrs, tunataka Ajira na Elimu Bora

Hayo mambo ya katiba mpya ni kikundi chenu ndio kinataka

Chadema mlipata viti vingi bungen Kwa katiba hii hii

Sasa huo umeme unaupataje bila uongozi thabiti unaowekwa ma wananchi? Au hayo maendeleo yatapaa bila wananchi kuya demand?

Kama huwezi kumuwajibisha kiongozi akiamua kutokuleta hayo maendeleo utachukua hatua gani?

BTW CCM wenzako wamejieleza hapo juu
 
Absolutely yes
Na hata hiyo katiba mpya itakuwa na vitu ambavyo mtu mwingine hatovipenda ni kama katiba hii Tu, wengine tunapenda na wengine hawapendi

Kwa hiyo mnapingana na Katibu mkuu wenu mstaafu?
 
Tatizo Tanzania watu wamezidisha NJAA na UBINAFSI sijui kwa nini Rais anawasikiliza hawa watu walio shiba miposho minono.

Hakuna Mtanzania ambaye ni mnufaika wa serikali akaongea kitu chochote dhidi ya serikali. Yaani tumekuwa watumwa ndani ya Nchi yetu wenyewe kwa maslahi binafsi.

KAMWE USIFIKIRIE WALIOPO SERIKALINI WATA SUPPORT KATIBA MPYA.
 
Samia akiwaamini hawa kwa kauli tofauti na hizi walizozitoa zamani kabla hawajawa na vyeo basi ajue wanamdanganya kama walivyomdnganya Magufuli.

Akiondoka madarakani akaja rais mwingine anayetaka katiba, hawahawa ndo watakuwa wa kwanza kumsifu rais mpya na kumponda yeye Samia kuwa alipoteza muda wake kutoshughulikia jambo la msingi
 
Alipoongea hakuwa katibu mkuu, alikuwa na mtazamo tofauti kwa kutojua nia thabiti ya Mbowe kutaka katiba mpya. Sasa kajua

Kwa hiyo aliyeongea ni nani? Sio Bashiru??

Hivi mbona unakuwa kichwa maji hivi? Kusoma huwezi bado nimekuwekea video bado hutaki kuamini??

Huyo Kabudi na yeye alikua na mtazamo upi?? Na kilichoubadirisha ni nini kama sio madaraka?
 
Hiyo clip kama kabudi kasingiziwa vile,niyeye na nihuyu wa sasa.
Mimi namkubali sana Msukuma "WASOMI WANATUCHANGANYA"
 
Sasa huo umeme unaupataje bila uongozi thabiti unaowekwa ma wananchi? Au hayo maendeleo yatapaa bila wananchi kuya demand?

Kama huwezi kumuwajibisha kiongozi akiamua kutokuleta hayo maendeleo utachukua hatua gani?

BTW CCM wenzako wamejieleza hapo juu

Uongozi dhabiti ni mpaka katiba mpya?
Mbona now kuna uongozi dhabiti Sana mpaka wakina mdude wanatukana Tu na bado yuko uraiani Tu
 
Hitaji la katiba mpya si kubwa sana kulinganisha na hitaji LA maendeleo ya watu. Katiba iliyopo sasa ukiacha madhaifu machache iliyonayo ni bora sana na yaweza kutuletea maendeleo. Hitaji la katiba mpya in hitaji la upinzani kuingia madarakani kwa maslahi
binafsi
Maendeleo hatayaleta samia peke yake ah yakafikia ukomo.
Mahitani ya maendeleo ni endelevj
 
Back
Top Bottom