Tate Mkuu
JF-Expert Member
- Jan 24, 2019
- 33,092
- 96,127
Lengo kuu la hili bandiko langu humu jukwaani, ni kukuomba tu kwa heshima na taadhima! Mheshimiwa Rais kuangalia namna ya kuvirejesha kwenye Halmashauri zetu baadhi ya viwanja vya michezo nchini mfano Sokoine Mbeya, Samora Iringa, Nelson Mandela Rukwa, Ali Hassan Mwinyi Tabora, Jamhuri Morogoro na Dodoma, Mkwakwani Tanga, na vinginevyo vingi kutoka kwenye umiliki wa chama chako cha CCM, ili viboreshwe kama ule uwanja wa Kaitaba Kagera! na hivyo kuendelea kutumika kwenye ligi yetu, lakini pia kwenye uibuaji wa vipaji vya wana michezo nchini, (na ukichukulia michezo ni moja ya vyanzo vizuri sana vya ajira kwa vijana), hivyo jambo hili halikwepeki.
Natambua fika siyo jambo jepesi kihivyo, ukichukulia kwamba hivi viwanja pia ni moja ya vyanzo vya mapato ya chama chako, na makada wachache. Lakini ifikie wakati tutangulize kwanza maslahi ya Taifa, na yale ya mtu binafsi/chama yafuate baadaye. Maana hivi viwanja vilijengwa enzi za mfumo wa chama kimoja kupitia kodi za Watanzania wote. Hivyo sioni sababu ya CCM kuvimiliki! Na huku ikishindwa kabisa kuviendeleza kwa miaka 30 sasa! Yaani karibia viwanja vyote viko mahututi kwa kukosa matunzo! Na badala yake imevigeuza tu kuwa chanzo chake kimojawapo cha mapato.
Ni matarajio yangu kuwa hili ombi litafanyiwa kazi kwa wakati.
Kwa niaba ya wapenda michezo wote nchini. Naomba kuwasilisha. ✍️
Natambua fika siyo jambo jepesi kihivyo, ukichukulia kwamba hivi viwanja pia ni moja ya vyanzo vya mapato ya chama chako, na makada wachache. Lakini ifikie wakati tutangulize kwanza maslahi ya Taifa, na yale ya mtu binafsi/chama yafuate baadaye. Maana hivi viwanja vilijengwa enzi za mfumo wa chama kimoja kupitia kodi za Watanzania wote. Hivyo sioni sababu ya CCM kuvimiliki! Na huku ikishindwa kabisa kuviendeleza kwa miaka 30 sasa! Yaani karibia viwanja vyote viko mahututi kwa kukosa matunzo! Na badala yake imevigeuza tu kuwa chanzo chake kimojawapo cha mapato.
Ni matarajio yangu kuwa hili ombi litafanyiwa kazi kwa wakati.
Kwa niaba ya wapenda michezo wote nchini. Naomba kuwasilisha. ✍️