Pre GE2025 Rais Samia nakuomba tena utekeleze haya kuelekea 2025

Pre GE2025 Rais Samia nakuomba tena utekeleze haya kuelekea 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Yusufu R H Sabura

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2020
Posts
355
Reaction score
486
Your Excellency,

Nakusalimu kwa jina la Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Raisi, Ninaamini umzima wa afya na unaendelea kutekeleza majukumu yako kwa kadri Mwenyezimungu alivyokujaalia.

Mheshimiwa Raisi, hii itakuwa ni mara yangu ya pili kuzungumza na wewe kupitia maandiko haya ya majukwaani, bila shaka salamu zangu za awali zilikufikia na kama bado naamini zitafika tu. Nimechukua tena uamuzi wa kukuandikia hili kwa vile, kama Kijana na shabiki wako kisiasa, nimeona ipo haja ya wewe kulitekeleza hili ili twende kwa ulaini zaidi hapo kwenye kampeni za uchaguzi mkuu 2025.

Jina langu ni YUSUFU R H SABURA.

Mheshimiwa Raisi, kwa dhamana uliyopewa na wananchi, kuliongoza taifa hili la Tanzania, inakuwa ni wajibu kwako kwanza kama Raisi, lakini pia kama mzazi au mlezi au hata mama, kuhakikisha kwamba si Tanzania ya leo tu, bali hata ya miaka mia moja baadae inakuwa katika mpangilio mzuri wa kimaisha yaani kijamii, kiuchumi na kisiasa. Mheshimiwa Raisi kuna ufa mkubwa sana hapa kwenye jamii yetu ukijaribu kutizama maisha ya vijana. Naam ni Sheria ya ndoa ya mwaka 1971.

Mheshimiwa Raisi, hivi karibuni kumekuwa na vuguvugu la vijana kukataa ndoa, na vuguvugu hili nimeanza kulionea hapahapa jamii forums!, wakisindikizwa na maneno hasi kama vile NDOA NI UTUMWA, NDOA NI UTAPELI nk. Kwa namna nilivyojaribu kuwaelewa kwa nafasi yangu, moja ya sababu ya vuguvugu hili ni muundo wa sheria yetu ya ndoa ya 1971. kwa vile sio mtaalamu sana wa masuala ya kisheria sifahamu kama kuna ammendments zozote zilizowahi kufanyika, na kama zipo basi nikwambie tu bado haijatosha.

Mheshimiwa Raisi, nakushauri waagize wabunge wa chama cha mapinduzi wakapitie na kuunda upya sheria ya ndoa. Tena katika zoezi hilo wawe watulivu sana zaidi ya utulivu aliokuwa nao mheshimiwa waziri Hussein Bashe alipokuwa akijibu hoja ya sukari ya ziada iliyoibuliwa na mheshimiwa mbunge, Luhaga Mpina.

Mheshimiwa Raisi, ninafahamu kabisa kwamba, wakati sheria hii inatungwa, lengo lilikuwa ni kuondoa kama sio kupunguza unyanyasaji wa kina mama ama kwa lugha ya hapa jinsia ya kike wanapokuwa katika maisha ya ndoa. Lengo lilikuwa jema na tunaona hali ilivyo sasa sio kama zamani, sasa utu wa mwanamke unaonekana na wanaume wamegundua aaah kumbe mwanamke naye ni mtu.
Lakini changamoto ya moto kwelikweli iliyojitokeza hapa ni kwamba, wakemia waliochanganya mseto wa sheria hii sijui walikuwa wamefumba macho !, kiukweli sheria ya ndoa imevuka katika kurekebisha na sasa inaharibu ndoa, mheshimiwa Raisi hii dozi ni kali sana na imekuwa sumu kwani familia zinakufa kwa kasi ya ATCL.

Mheshimiwa Raisi, hivi sasa vijana wanaamua kukataa ndoa na kuanzisha mifumo mipya ya kimaisha ambayo ni ya hovyo ukilinganisha na utamaduni wetu, zimesikika sauti mitaani kwamba kupitia sheria hizi wanawake wamekuwa wajeuri kwelikweli na wamekuwa tishio hata kwa mali za familia, ndio kusema kwamba wakigombana kidogo tu silaha yao kubwa ni kuvunja ndoa ili wagawane mali. tafsiri ya hili ni kuwa, badala ya kufanya kazi wapo watu kila siku wanabuni ndoa ili wakapore vilivyotafutwa huko.

Mheshimiwa Raisi, ili ugundue kuwa kuna shida hapa, kwa vile wewe ni mwanamke nitakuomba uvae kimyakimya uhusika wa watu wawili hawa, wa kwanza ni mdada anaejidai kulindwa na sheria ya ndoa ya 1971, lakini uhusika wa pili ni kuwa mama mzazi wa mwanaume anaefanyiwa unyang'anyi wa kisheria na binti kupitia mwamvuli wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971. Sijakuchagulia uhusika wa kiume kwa vile huwezi kuwa na hisia za moja kwa moja za kianaume, wewe ni mtu mzima, ulianza kuwa binti, ukawa mama na hata bibi wa wajukuu zako, kwahio wahusika hawa wote wawili wapo ndani yako.

Mheshimiwa Raisi, ni furaha sana kwa mabinti kujitwalia mali kwa urahisi kabisa na kwa kweli hata ningekuwa mimi ningefurahi maana ni upendeleo wa kipekee, sina maana ya kudhoofisha juhudi za sera ya jinsia ya hamsini kwa hamsini lakini fikiria wanandoa wanapopelekwa madawatini halafu akasikilizwe mwanamke tu na mwanaume akapewe karipio, akaonekana hana akili na jitihada zake zote kuijenga familia zisionekane na ikibidi anyang'anywe bila kujali muda alioutumia. Fikiria kuwa ungekuwa wewe ni mama mzazi wa mwanaume huyu ungepata furaha kama aliyoipata mwanamke mwenzako (mkweo)? kwa kuzingatia tu kwamba sheria imempendelea sana mwanamke na kumuacha nyuma mwanaume badala ya kuleta usawa! .

Mheshimiwa Raisi, nakuomba rudisha imani ya serikali kwa vijana kwa kubadilisha sheria hii iendane na sera ya hamsini kwa hamsini, ili vijana waache uoga wa kunyanyaswa na wake zao na wakimbilie ndoa haraka sana iwezekanavyo kwa maslahi ya taifa. Kama utafanya hivi nakuhakikishia vijana na wakina mama wengi ambao kimsingi ni wote watakukumbatia kwa furaha ambayo hawajawahi kuisikia tangu sheria hiyo ilipoundwa.

Mheshimiwa Raisi nimeandika hili kwa experience kubwa sana, familia yangu sasa (mimi ni mtoto) ipo katika hali ya kusambaratika kwa muda wa miaka karibia kumi chanzo kikiwa ni sheria ya ndoa ya mwaka 1971, Nilikuwa form three, nikaenda high school, nikaenda chuo, nikamaliza na sasa nipo kitaa.

Mheshimiwa Raisi, nimekusikia mara kadhaa ukiimba wimbo wa Political Stability, sisi wataalamu wa sayansi ya siasa tunaamini kuwa familia ndio the smallest political unit in a state. kama huku chini hakutakuwa na stability ya kiutawala nakuhakikishia huko juu mtasumbuka sana, anza na ngazi ya familia, sisi wawakilishi wako katika ngazi ya familia(wanaume) sheria inatunyanyasa mno.

Mheshimiwa Raisi, jambo la pili ambalo binafsi nafikiri litakuwa fyekeo kali sana kuelekea 2025 ni MSAMAHA WA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU KUANZIA MWAKA 2014-2024.

Najua kuna wakosoaji watasema nafanya jitihada za kufutiwa deni langu lakini nakuhakikishia hili ni sahihi na ikibidi samehe wote nchi nzima la kwangu nitalilipa mwenyewe, ni takriban
i kama millioni kumi na tatu na ushee hivi.

Mheshimiwa Raisi, nimeamua kuchagua miaka tajwa hapo hapo juu kwa vile wewe ni shahidi kwamba, tangu mwaka 2014 serikali iliacha kutoa ajira kwa kada nyingi, hadi wewe ulipoingia madarakani mwaka 2021, hata hivyo pamoja na jitihada zako za angalau kupunguzapunguza aibu hii bado kidonda kilichopo ni kikubwa sana na lawama hazitakuwa upande wako hata kidogo.


Isipokuwa ningekushauri, ili upunguze fukuto la hasira na kuvunjikwa mioyo ya wengi waliohitimu, wasamehe mikopo yao na ikibidi watakapopata ajira badala ya kuanza kulipa deni hilo kubwa basi waanze maisha kwa wepesi. wamekaa sana mtaani, Mheshimiwa Raisi kete iliyobaki ni kujenga familia zao hivyo wapunguzieni (sisi) mzigo kwani halikuwa kosa lao(letu).

Mheshimiwa Raisi, ninaamini msamaha kwa mikopo ya elimu ya juu kuanzia mwaka 2014-2024 inawezekana kwa vile, hebu tumia logic hii tu ndogo, mmetupatia mikopo kwa miaka kumi na hatujarudisha na bado nchi unaijenga, na kila mwaka bajeti ya HESLB inapanda hii ni ishara na dalili kwamba elimu bure vyuo vikuu inawezekana lakini anza kwanza na hili la msamaha wa mikopo, NAJUA UNAWEZA MHESHIMIWA RAISI.

Mheshimiwa Raisi, Nakuona ukishinda kwa ushindi wa kimbunga, kura ni za kuokota, tufanyie hayo vijana wako ili waseme umeturoga. hakika utakuwa umewakomboa vijana na ukiwakomboa vijana utakuwa umelikomboa taifa.

Sitapenda kumaliza uzi huu bila kukupongeza kwa mambo makubwa unayolifanyia taifa letu, sisi tunaona kuwa ilivyokuwa jana siyo leo, hivyo wewe chapa kazi, wakikunanga sana wewe niite mimi nitazungumza nao taratibu na wataelewa tu.

Asante na kazi iendelee.

YUSUFU R H SABURA
0750883466/0717934194.
 
Your Excellency,

Nakusalimu kwa jina la Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Raisi, Ninaamini umzima wa afya na unaendelea kutekeleza majukumu yako kwa kadri Mwenyezimungu alivyokujaalia.

Mheshimiwa Raisi, hii itakuwa ni mara yangu ya pili kuzungumza na wewe kupitia maandiko haya ya majukwaani, bila shaka salamu zangu za awali zilikufikia na kama bado naamini zitafika tu. Nimechukua tena uamuzi wa kukuandikia hili kwa vile, kama Kijana na shabiki wako kisiasa, nimeona ipo haja ya wewe kulitekeleza hili ili twende kwa ulaini zaidi hapo kwenye kampeni za uchaguzi mkuu 2025.

Jina langu ni YUSUFU R H SABURA.

Mheshimiwa Raisi, kwa dhamana uliyopewa na wananchi, kuliongoza taifa hili la Tanzania, inakuwa ni wajibu kwako kwanza kama Raisi, lakini pia kama mzazi au mlezi au hata mama, kuhakikisha kwamba si Tanzania ya leo tu, bali hata ya miaka mia moja baadae inakuwa katika mpangilio mzuri wa kimaisha yaani kijamii, kiuchumi na kisiasa. Mheshimiwa Raisi kuna ufa mkubwa sana hapa kwenye jamii yetu ukijaribu kutizama maisha ya vijana. Naam ni Sheria ya ndoa ya mwaka 1971.

Mheshimiwa Raisi, hivi karibuni kumekuwa na vuguvugu la vijana kukataa ndoa, na vuguvugu hili nimeanza kulionea hapahapa jamii forums!, wakisindikizwa na maneno hasi kama vile NDOA NI UTUMWA, NDOA NI UTAPELI nk. Kwa namna nilivyojaribu kuwaelewa kwa nafasi yangu, moja ya sababu ya vuguvugu hili ni muundo wa sheria yetu ya ndoa ya 1971. kwa vile sio mtaalamu sana wa masuala ya kisheria sifahamu kama kuna ammendments zozote zilizowahi kufanyika, na kama zipo basi nikwambie tu bado haijatosha.

Mheshimiwa Raisi, nakushauri waagize wabunge wa chama cha mapinduzi wakapitie na kuunda upya sheria ya ndoa. Tena katika zoezi hilo wawe watulivu sana zaidi ya utulivu aliokuwa nao mheshimiwa waziri Hussein Bashe alipokuwa akijibu hoja ya sukari ya ziada iliyoibuliwa na mheshimiwa mbunge, Luhaga Mpina.

Mheshimiwa Raisi, ninafahamu kabisa kwamba, wakati sheria hii inatungwa, lengo lilikuwa ni kuondoa kama sio kupunguza unyanyasaji wa kina mama ama kwa lugha ya hapa jinsia ya kike wanapokuwa katika maisha ya ndoa. Lengo lilikuwa jema na tunaona hali ilivyo sasa sio kama zamani, sasa utu wa mwanamke unaonekana na wanaume wamegundua aaah kumbe mwanamke naye ni mtu.
Lakini changamoto ya moto kwelikweli iliyojitokeza hapa ni kwamba, wakemia waliochanganya mseto wa sheria hii sijui walikuwa wamefumba macho !, kiukweli sheria ya ndoa imevuka katika kurekebisha na sasa inaharibu ndoa, mheshimiwa Raisi hii dozi ni kali sana na imekuwa sumu kwani familia zinakufa kwa kasi ya ATCL.

Mheshimiwa Raisi, hivi sasa vijana wanaamua kukataa ndoa na kuanzisha mifumo mipya ya kimaisha ambayo ni ya hovyo ukilinganisha na utamaduni wetu, zimesikika sauti mitaani kwamba kupitia sheria hizi wanawake wamekuwa wajeuri kwelikweli na wamekuwa tishio hata kwa mali za familia, ndio kusema kwamba wakigombana kidogo tu silaha yao kubwa ni kuvunja ndoa ili wagawane mali. tafsiri ya hili ni kuwa, badala ya kufanya kazi wapo watu kila siku wanabuni ndoa ili wakapore vilivyotafutwa huko.

Mheshimiwa Raisi, ili ugundue kuwa kuna shida hapa, kwa vile wewe ni mwanamke nitakuomba uvae kimyakimya uhusika wa watu wawili hawa, wa kwanza ni mdada anaejidai kulindwa na sheria ya ndoa ya 1971, lakini uhusika wa pili ni kuwa mama mzazi wa mwanaume anaefanyiwa unyang'anyi wa kisheria na binti kupitia mwamvuli wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971. Sijakuchagulia uhusika wa kiume kwa vile huwezi kuwa na hisia za moja kwa moja za kianaume, wewe ni mtu mzima, ulianza kuwa binti, ukawa mama na hata bibi wa wajukuu zako, kwahio wahusika hawa wote wawili wapo ndani yako.

Mheshimiwa Raisi, ni furaha sana kwa mabinti kujitwalia mali kwa urahisi kabisa na kwa kweli hata ningekuwa mimi ningefurahi maana ni upendeleo wa kipekee, sina maana ya kudhoofisha juhudi za sera ya jinsia ya hamsini kwa hamsini lakini fikiria wanandoa wanapopelekwa madawatini halafu akasikilizwe mwanamke tu na mwanaume akapewe karipio, akaonekana hana akili na jitihada zake zote kuijenga familia zisionekane na ikibidi anyang'anywe bila kujali muda alioutumia. Fikiria kuwa ungekuwa wewe ni mama mzazi wa mwanaume huyu ungepata furaha kama aliyoipata mwanamke mwenzako (mkweo)? kwa kuzingatia tu kwamba sheria imempendelea sana mwanamke na kumuacha nyuma mwanaume badala ya kuleta usawa! .

Mheshimiwa Raisi, nakuomba rudisha imani ya serikali kwa vijana kwa kubadilisha sheria hii iendane na sera ya hamsini kwa hamsini, ili vijana waache uoga wa kunyanyaswa na wake zao na wakimbilie ndoa haraka sana iwezekanavyo kwa maslahi ya taifa. Kama utafanya hivi nakuhakikishia vijana na wakina mama wengi ambao kimsingi ni wote watakukumbatia kwa furaha ambayo hawajawahi kuisikia tangu sheria hiyo ilipoundwa.

Mheshimiwa Raisi nimeandika hili kwa experience kubwa sana, familia yangu sasa (mimi ni mtoto) ipo katika hali ya kusambaratika kwa muda wa miaka karibia kumi chanzo kikiwa ni sheria ya ndoa ya mwaka 1971, Nilikuwa form three, nikaenda high school, nikaenda chuo, nikamaliza na sasa nipo kitaa.

Mheshimiwa Raisi, nimekusikia mara kadhaa ukiimba wimbo wa Political Stability, sisi wataalamu wa sayansi ya siasa tunaamini kuwa familia ndio the smallest political unit in a state. kama huku chini hakutakuwa na stability ya kiutawala nakuhakikishia huko juu mtasumbuka sana, anza na ngazi ya familia, sisi wawakilishi wako katika ngazi ya familia(wanaume) sheria inatunyanyasa mno.

Mheshimiwa Raisi, jambo la pili ambalo binafsi nafikiri litakuwa fyekeo kali sana kuelekea 2025 ni MSAMAHA WA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU KUANZIA MWAKA 2014-2024.

Najua kuna wakosoaji watasema nafanya jitihada za kufutiwa deni langu lakini nakuhakikishia hili ni sahihi na ikibidi samehe wote nchi nzima la kwangu nitalilipa mwenyewe, ni takriban
i kama millioni kumi na tatu na ushee hivi.

Mheshimiwa Raisi, nimeamua kuchagua miaka tajwa hapo hapo juu kwa vile wewe ni shahidi kwamba, tangu mwaka 2014 serikali iliacha kutoa ajira kwa kada nyingi, hadi wewe ulipoingia madarakani mwaka 2021, hata hivyo pamoja na jitihada zako za angalau kupunguzapunguza aibu hii bado kidonda kilichopo ni kikubwa sana na lawama hazitakuwa upande wako hata kidogo.


Isipokuwa ningekushauri, ili upunguze fukuto la hasira na kuvunjikwa mioyo ya wengi waliohitimu, wasamehe mikopo yao na ikibidi watakapopata ajira badala ya kuanza kulipa deni hilo kubwa basi waanze maisha kwa wepesi. wamekaa sana mtaani, Mheshimiwa Raisi kete iliyobaki ni kujenga familia zao hivyo wapunguzieni (sisi) mzigo kwani halikuwa kosa lao(letu).

Mheshimiwa Raisi, ninaamini msamaha kwa mikopo ya elimu ya juu kuanzia mwaka 2014-2024 inawezekana kwa vile, hebu tumia logic hii tu ndogo, mmetupatia mikopo kwa miaka kumi na hatujarudisha na bado nchi unaijenga, na kila mwaka bajeti ya HESLB inapanda hii ni ishara na dalili kwamba elimu bure vyuo vikuu inawezekana lakini anza kwanza na hili la msamaha wa mikopo, NAJUA UNAWEZA MHESHIMIWA RAISI.

Mheshimiwa Raisi, Nakuona ukishinda kwa ushindi wa kimbunga, kura ni za kuokota, tufanyie hayo vijana wako ili waseme umeturoga. hakika utakuwa umewakomboa vijana na ukiwakomboa vijana utakuwa umelikomboa taifa.

Sitapenda kumaliza uzi huu bila kukupongeza kwa mambo makubwa unayolifanyia taifa letu, sisi tunaona kuwa ilivyokuwa jana siyo leo, hivyo wewe chapa kazi, wakikunanga sana wewe niite mimi nitazungumza nao taratibu na wataelewa tu.

Asante na kazi iendelee.

YUSUFU R H SABURA
0750883466/0717934194.
Tafuta kwanza pesa ndiyo uwe na mke huyo mke hawezi kula, kuvaa vizuri na kulala pazuri eti, (kisa), wewe umevaa suruali ama handsome, umasikini unasababishwa na akili za binadamu na ukiwa masikini ni rahisi kutawaliwa na mtu yeyote, above all what we need is national economy and social development strategies of an existing government, (tunahitaji tu aina ya uchumi wenye mikakati ya kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja). Hitimisho wasomi hakikisheni jamii inakuwa na uwezo wa kubuni mbinu zinazoweza kukabiliana na changamoto zitakazo jitokeza kwenye jamii, (adaptbility skills)
 
Tafuta kwanza pesa ndiyo uwe na mke huyo mke hawezi kula, kuvaa vizuri na kulala pazuri eti, (kisa), wewe umevaa suruali ama handsome, umasikini unasababishwa na akili za binadamu na ukiwa masikini ni rahisi kutawaliwa na mtu yeyote, above all what we need is national economy and social development strategies of an existing government, (tunahitaji tu aina ya uchumi wenye mikakati ya kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja). Hitimisho wasomi hakikisheni jamii inakuwa na uwezo wa kubuni mbinu zinazoweza kukabiliana na changamoto zitakazo jitokeza kwenye jamii
Asante kwa uchangiaji wako,

Sijaomba kutafutiwa mke na mtu hapo na wala sijatangaza ndoa na mtu.
Sijafahamu kama umechangia, kupinga, kuongeza nyama ama kutoa maoni kwenye thread hii kwa maana kwa jicho la harakaharaka ni kama vile hujagusa angle yeyote katika thread hii.

Vijana tupunguze ujuaji usio wa lazima, kama huoni cha kuchangia soma uzi nenda zako nyuzi zipo za kutosha humu, yaani na hili tusubiri kuambiwa ?
 
Sasa unayeomba atekeleze hayo, Yeye ni mke wa nne kwenye NDOA yake.

Sasa itakuwaje 🤔
Ukiachana na kuwa ni mke wa nne, yeye ni Raisi na Mkuu wa serikali hivyo nafasi hiyo anayo, vilevile ni mwenyekiti wa chama cha siasa, anaweza kushape sera.

tuambie ndugu mchangiaji ni kwa vipi mke wa nne hawezi kutekeleza niliyoyaomba iwapo tu atakuwa na nafasi ya kufanya hivyo.
 
Asante kwa uchangiaji wako,

Sijaomba kutafutiwa mke na mtu hapo na wala sijatangaza ndoa na mtu.
Sijafahamu kama umechangia, kupinga, kuongeza nyama ama kutoa maoni kwenye thread hii kwa maana kwa jicho la harakaharaka ni kama vile hujagusa angle yeyote katika thread hii.

Vijana tupunguze ujuaji usio wa lazima, kama huoni cha kuchangia soma uzi nenda zako nyuzi zipo za kutosha humu, yaani na hili tusubiri kuambiwa ?
Imegusia kuhusu kukataa ndoa kwenye thread yako inamaana umesha sahau wenzenu kujibu hizi threads tunatumia pia, social inference
 
Imegusia kuhusu kukataa ndoa kwenye thread yako inamaana umesha sahau wenzenu kujibu hizi threads tunatumia pia, ocial inference
Ndugu mchangiaji hapa jukwaani kuna watu wa aina mbalimbali,
waambie nini maana ya social inference,
lakini pia je ! katika uchangiaji wako ulikumbuka kutaja maneno ya msingi kama yalivyotumika kwenye kifungu? kwa mfano neno KATAA NDOA, ama ulitembea na biti la kaswida kwenye nyimbo za kisabato?
 
Ndugu mchangiaji hapa jukwaani kuna watu wa aina mbalimbali,
waambie nini maana ya social inference,
lakini pia je ! katika uchangiaji wako ulikumbuka kutaja maneno ya msingi kama yalivyotumika kwenye kifungu? kwa mfano neno KATAA NDOA, ama ulitembea na biti la kaswida kwenye nyimbo za kisabato?
Nini chimbuko la kataa ndoa, Kwanza lazima usiwe mtoto Pili lazima uwe na kipato, (uwe na njia ya uhakika ya kujiingizia kipato), kama huna vigezo hivyo KATAA NDOA, if you do not know where you are going any path,(road), will take you there
 
Nini chimbuko la kataa ndoa, Kwanza lazima usiwe mtoto Pili lazima uwe na kipato, (uwe na njia ya uhakika ya kujiingizia kipato), kama huna vigezo hivyo KATAA NDOA, if you do not know where you are going any path,(road), will take you there
Najaribu kuzingatia maoni yako lakini sielewi kabisa unachoandika ndugu mchangiaji,
Nakushauri na wewe, uwe unatulia, jitahidi walau kidogo kuzingatia taratibu za kiuandishi.
 
Najaribu kuzingatia maoni yako lakini sielewi kabisa unachoandika ndugu mchangiaji,
Nakushauri na wewe, uwe unatulia, jitahidi walau kidogo kuzingatia taratibu za kiuandishi.
Kwakifupi hizo changamoto ulizo ziainisha tatizo liko kwenye jamii yetu kuto kubuni mbinu za kukabiliana na changamoto tulizonazo ama zitakazo kuja hayo mabadiliko unayo yatamani yanatokana na jamii, (society), je jamii inauwezo wa kupokea mfano mabadiliko ya teknolojia, kukabiliana na changamoto yaani jamii tunayo ishi ikoje, ,(social demographic variables) wewe huishi peke yako je unacho kijua na kukiami wengine wanacho?, Mfano hai kuna wengine kwenye jamii zetu hawawezi kufanya muamala kwenye simu zao za mkononi
 
Kwakifupi hizo changamoto ulizo ziainisha tatizo liko kwenye jamii yetu kuto kubuni mbinu za kukabiliana na changamoto tulizonazo hayo mabadiliko unayo yatamani yanatokana na jamii, (society), je jamii inauwezo wa kupokea mfano mabadiliko ya teknolojia, kukabiliana na changamoto yaani jamii tunayo ishi ikoje, ,(social demographic variables)
Asante,

Wakati tunaendelea kukubaliana taratibu, naomba unifungulie ufahamu ni kwa namna gani sheria mpya ya ndoa(iwapo itatungwa) pamoja na msamaha wa deni kwa wanafunzi wa elimu ya juu vinahusiana na teknolojia kama ulivyoandika katika mfano wako.

yaani ni sawa na kusema kuwa, kuna uhusiano gani kati ya teknolojia na sheria mpya ya ndoa pamoja na msamaha wa deni kwa wahitimu wa vyuo vikuu.

Aidha kwa uelewa wako, ni kwa vipi jamii itashindwa kupokea sheria mpya ya ndoa pamoja na msamaha wa deni la mkopo kwa wahitimu wa vyuo vikuu? (nakuuliza kulingana na ninavyojaribu kukuelewa !.

Ndugu mchangiaji je 1 unafikiri serikali haina uwezo wa kuyatimiza hayo?
 
Asante,

Wakati tunaendelea kukubaliana taratibu, naomba unifungulie ufahamu ni kwa namna gani sheria mpya ya ndoa(iwapo itatungwa) pamoja na msamaha wa deni kwa wanafunzi wa elimu ya juu vinahusiana na teknolojia kama ulivyoandika katika mfano wako.

yaani ni sawa na kusema kuwa, kuna uhusiano gani kati ya teknolojia na sheria mpya ya ndoa pamoja na msamaha wa deni kwa wahitimu wa vyuo vikuu.

Aidha kwa uelewa wako, ni kwa vipi jamii itashindwa kupokea sheria mpya ya ndoa pamoja na msamaha wa deni la mkopo kwa wahitimu wa vyuo vikuu? (nakuuliza kulingana na ninavyojaribu kukuelewa !.

Ndugu mchangiaji je 1 unafikiri serikali haina uwezo wa kuyatimiza hayo?
Swali zuri nimeongelea mfano wa teknolojia nilidhani itakuwa rahisi kwako mfano ili uweze kuitengeneza televisheni lazima uwe umejifunza basic electronics basic electronics ni elimu msingi inayo kuwezesha kuvitambua vipuli muhimu kwenye vifaa vya kidijitali jinsi vinavyo fanya kazi na tabia zake, vipimo, vikiwa vibovu na vizima inamaana kama ujuzi huo umeboreshwa na wewe unatakiwa kusasisha, (update) usipofanya hivyo vifaa vipya huwezi kuvitengeneza turudi kwenye sheria na mengineyo kama jamii ni mbumbumbu itaburuzwa na ndiyo maana nimekuwa naongelea kuhusu mapokeo ya jamii kama ni mbumbumbu itakuwa ni jamii ya bora liende na hapo ndiyo patamu sana nimesema yote unayo yatamani tatizo liko kwenye jamii, kama ni jamii ambayo ni ya kupokea kila kitu hatuwezi kupiga hatua ndiyo maana mlipo hoji kuhusu tozo mliambiwa muende burundi, tuliandaliwa kuto kuhoji na tatizo la kuhoji linaanza kwenye ngazi ya familia kuna vitu ukivihoji utaambiwa kama umekua uondoke
 
Aliye na summary jamani! Jamaa anataka ndoa ziweje!?
 
Alichopost jamaa.. anatakeje!? Sijasoma
Kavunja barafu, kwa muheshimiwa Rais kwa kuandika barua ya wazi asimamie sera ya ndoa, iruhusu vijana kuoana haraka, (mapema), kwasababu yeye ni mhanga wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 pia kufuta mikopo vyuoni
 
Back
Top Bottom