Rais Samia: Nayahakikishia Makampuni yote yaliyowekeza Tanzania usalama wa Mali Biashara zao

Rais Samia: Nayahakikishia Makampuni yote yaliyowekeza Tanzania usalama wa Mali Biashara zao

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua kiwanda cha uzalishaji vioo vya ujenzi cha Saphire Float Glass - Mkuranga Mkoa wa Pwani leo tarehe 20 Septemba, 2023.


Rais Samia amesema Kiwanda hiki kitakuwa kikubwa zaidi Afrika Mashariki na Kati, na cha 4 kwa Ukubwa barani Afrika kwa uzalishaji wa vioo vya ujenzi. Pia, 75% ya bidhaa zake zitauzwa nje ya nchi hivyo kuongeza mapato kwa nchi na kutoa ajira 1650 kitakapokamilika kuanza kufanya uzalishaji kamili.

Uwekezaji huu nchini ni mapinduzi makubwa ya kuimarisha uchumi wa nchi.

Serikali imefanya maboresho mengi ya kisera, kisheria na kikanuni ili kufanya mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kuwa bora zaidi.

China na Tanzania zinafurahia urafiki wa kidiplomasia ambao unakaribia kufikia miaka 60, uwepo wa wawekezaji hawa ni mfano halisi wa mahusiano mema kati ya nchi hizi mbili. Nayahakikishia makapuni yote yaliyowekeza Tanzania kutoka ndani na nje ya nchi, mali zenu zipo salama, na serikali itaendelea kuwekeza au kuweka mazingira mazuri kwa biashara zenu kufanikiwa.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua kiwanda cha uzalishaji vioo vya ujenzi cha Saphire Float Glass - Mkuranga Mkoa wa Pwani leo tarehe 20 Septemba, 2023.


Rais Samia amesema Kiwanda hiki kitakuwa kikubwa zaidi Afrika Mashariki na Kati, na cha 4 kwa Ukubwa barani Afrika kwa uzalishaji wa vioo vya ujenzi. Pia, 75% ya bidhaa zake zitauzwa nje ya nchi hivyo kuongeza mapato kwa nchi na kutoa ajira 1650 kitakapokamilika kuanza kufanya uzalishaji kamili.

Uwekezaji huu nchini ni mapinduzi makubwa ya kuimarisha uchumi wa nchi.

Serikali imefanya maboresho mengi ya kisera, kisheria na kikanuni ili kufanya mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kuwa bora zaidi.

China na Tanzania zinafurahia urafiki wa kidiplomasia ambao unakaribia kufikia miaka 60, uwepo wa wawekezaji hawa ni mfano halisi wa mahusiano mema kati ya nchi hizi mbili. Nayahakikishia makapuni yote yaliyowekeza Tanzania kutoka ndani na nje ya nchi, mali zenu zipo salama, na serikali itaendelea kuwekeza au kuweka mazingira mazuri kwa biashara zenu kufanikiwa.

Naunga mkono hoja ✔️!! But mikataba mibovu noo ❌❌❌❌
 
Hutasikia watanzania wakihakikishiwa usalama wa mali zao. Hutasikia watanzania wakihakikishiwa usalama wa rasilimali zao. Hutasikia watanzania wakihakikishiwa uhakika wa haki zao, zikiwepo za kuchagua viongozi wanaowataka kwa uhuru.
Mama aache ulevi wa madaraka. Usalama wa uwekezaji utawezekana tu pale wananchi wenye nchi nao watakapokuwa na uhakika wa usalama wa haki zao zote za msingi na usalama wa rasilimali zao.

Mara ya mwisho kauli kama hii aliitoa Muamar Ghadafi alipoona machafuko yamepamba moto yakichochewa na Rais Barak Obama wa Marekani aaliyefadhuli mapinduzi ya umma akitumia mwanya wa ukandamizaji aliofanya Ghadafi kwa muda mrefu dhidi ya wapinzani na wananchi wake.

Mama kama unaamini kuwa wewe unaweza kulinda wawekezaji wa nje kwa mtutu wa bunduki, basi nakupa Pole nyingi. Yatakushinda siku yaja.

Itazame Niger waliomwondoa kwa fedheha rais kibaraka aliyeihakikishia Ufaransa kuwa anawagawia rasilimali bure bure ili nao wamlinde. Ameishia kuwa mfungwa, huku mabwana zake wakishindwa kumsaidia kwa lolote.

Tujitafakari kwa kauli zetu.
 
Back
Top Bottom