Rais Samia: Nilimwondoa Kidata TRA sababu niliona mwishoni atadata

Kwa hiyo anataka kidata akadate ikulu
 
ina maana tra wanajulikana waziwazi ni wizi wanaiba hela, naona mama anamuagiza yussuf kama na yeye yumo kwenye hayo mambo sasa akazibe ile mianya
 
Kwa maana nyingine atalewa sifa au siyo!

Tuna mama mwenye sisi kujiuliza maswali mengi na bado tusimwelewe
 
Wakuu nipo na swali

Kwa nini , tukiapa lazima tamka kwamba sitotoa siri, hizo ni siri zipi ? So siri hata kama zinavunja haki za kibidam ?

Napendekeza kiapo kiwe hivi,

Mimi Mbatizaji 4 7 nitatoa siri zote ambanzo zitaenda kinyume na maadili ya viongozi wa umma ,na kwa nchi ,kamwe sitovumilia ufisadi , matamko kutoka juu n.k
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema amemuondoa aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata kwenye nafasi yake kwakuwa aliona atadata kwa jinsi anavyoandamwa lakini amekiri kuwa TRA chini ya Kidata imefanya vizuri na kuongeza mapato hadi kufikia Tsh. trilioni 27.64, ambayo ni sawa na ufanisi wa 97.67% ya lengo la kukusanya Tsh. trilioni 28.30 katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2023/24 ambalo ni ongezeko la 14.50% ikilinganishwa na makusanyo ya Tsh. trilioni 24.14 katika Mwaka wa Fedha uliopita, 2022/23.

Akiongea leo July 05,2024, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar wakati akiwaapisha Viongozi Wateule, Rais Samia amesema โ€œYusuph Mwenda kwanza hongera kwa kazi nzuri uliyofanya Zanzibar, tunakupeleka TRA (kuwa Kamishna mpya), TRA chini ya Kidata imefanya vizuri sana, mapato yamekua sana, sitegemei kama utashuka, kwanini nimemuondoa Kidata?, Kidata nimemuondoa niliona mwisho atadata, kazi kafanya nzuri sana lakini niliona atadata jinsi anavyoandamwa , sasa nakupeleka wewe Kijana wa Dar es salaam
Mtoto wa Mjini, uhuni wote ulioko TRA kule umefanywa na wewe ukiwa mulemule pengine uli-participateโ€

โ€œMipango yote mule ya kupenya, ya kufanyaje na Bandari mnatoa wapi mnapenyeza wapi unaijua Yusuph nenda kaizibe, nenda kaizibe, tunachohitaji ni mapato, tunachohitaji ni kupungua kukopa, tunakopa tunajichetua kila anayekuja akija European Bank yes yes, akija huyu Yes, World Bank wanatunyanyasa tumo tu, nini?, tuna miradi ya maendeleo inataka pesa, pesa hatuna tunakopa, tunakopa tunanyanyasika, je tukiwaomba itakuwaje?, kwahiyo twende tukanyanyue za kwetuโ€

โ€œSerikali imefanya yote, tumeweka mazingira mazuri ya kufanya biashara, mazingira mazuri ya kufanya uwekezaji, Wawekezaji wanakuja, biashara zinafanyika kodi hazilipwi, Kariakoo pale tatizo ni kulipa kodi ukienda leo wanakuambia hiki kesho wanakuambia hiki, Kariakoo pekee yake kuna mapato kama yatakusanywa vizuri kwa mwaka yanaendesha Wizara tatu lakini hamkusanyi kuingia Serikalini, inawezekana mnakusanya kuingia mfukoni lakini hamkusanyi kuingiza Serikalini nenda kazibe hiloโ€

โ€œMwenda unaijua vizuri TRA ulikuwa sijui Mkurugenzi wa kodi zipi lakini ulikuwa unajua mnaibia vipi na wenzio kwahiyo yale mliokuwa mkiiba vichochoro vile nenda kazibe tunahitaji fedha, nimekuamini na najua utakwenda kufanya kaziโ€

#MillardAyoUPDATES

NB: Kiukweli 2025 tugangamale vingine tutakuja kuwa Zimbambwe iliyochangamka.
 
dah inaumiza sana ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ”ฅ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ
 
Kwani kuna shida gani katika maneno hayo? Na je reality ni ipi? Kwani hizo tekniki alizozisema hazipo?

Au kwani wewe hufahamu mtu yeyote anayefanya kazi TRA au ndugu au jirani? Kuna unayemuona ni maskini?

Wanaposema wanataka mtu mwenye experience ya miaka kadhaa kwenye kazi na uzoefu fulani unadhani wanamaanisha uzoefu gani?

Nenda interview za madreva wa mabasi ya mikoani, unadnani kama hujawahi kuangusha gari au kugongana ndiyo utapata kazi kirahisi ? Hakuna mwenye biashara ya basi atakayetaka ukajifunzie kwake kuangusha basi.

Yusuf Juma Mwenda atapewa malengo ya kuvuka makusanyo ya kodi zaidi ya alivyofanya Kidata. Na kwa kuwa anajuwa wanavyoiba na kukwepa basi ndiye mtu sahihi. Kama hatatumia uzoefu wake, basi atampisha mtu mwingine
 
Hakuwa na approach nzuri Kwa wafanyabiashara, yaani wakileta kwere hajali hana dialogue ni kukausha tuu.

Hata hivyo aliyemleta ana ufanisi mkubwa zaidi kule Zanzibar kuliko Kidata na ndio maana amemtahadharusha kwamba Kiongozi asicheke na wafanyabiashara maana Yuko monitored.

Kwa Ajili Yako Kuna mwaka Mapato ya TRA yamewahi kushuka?

Mwisho 2025 mugangamale kwa.kufanyaje labda?๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

View: https://twitter.com/MwananchiNews/status/1809244084726280593?t=OyxMP-Vd9bCm6qwdpOVT0A&s=19
 
โ€œMwenda unaijua vizuri TRA ulikuwa sijui Mkurugenzi wa kodi zipi lakini ulikuwa unajua mnaibia vipi na wenzio kwahiyo yale mliokuwa mkiiba vichochoro vile nenda kazibe tunahitaji fedha, nimekuamini na najua utakwenda kufanya kaz
Uislamu unakataza mwanamke kuwa mtawala. madhara yake ndiyo haya johnthebaptist
 
Reactions: rr4
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ