Rais Samia onesha pia Uchungu wako katika Sekta ya Ardhi kwani Wanyonge wanadhulumiwa mno

Rais Samia onesha pia Uchungu wako katika Sekta ya Ardhi kwani Wanyonge wanadhulumiwa mno

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Mheshimiwa Rais kama kuna Sekta ambayo kwa sasa inatajwa na Dhambi ya Kudhulumu Watanzania Wanyonge basi ni ya Ardhi.

Na kama kuna Mkoa ambao unaongoza kwa Watanzania Wanyonge Kudhulumiwa Ardhi yao ni Mkoa wa Dar es Salaam.

Na kama kuna Mkuu wa Mkoa ambaye anapewa Lawana ya Kutetea Wapora Ardhi ya Watanzania Wanyonge basi ni Amos Makalla wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Rais lifanyie Kazi hili ila Kilio ni Kikubwa kwa Watanzania Wanyonge Kuporwa na Kudhulumiwa Ardhi yao kwa Baraka zote za Wizara ya Ardhi.
 
Ardhi ni mikoa yote mikubwa KUMEOZA

Ni UTAPELI ULIOKUBUHU.

Ila mijitu Kama Rizioni na Mabula ipo IPO tu bora kumekucha.

Takataka kabisa
 
Kuna dhulma kubwa sana kwenye ardhi. Watu wanaporwa ardhi mchana kweupe.
 
Kuna dhulma kubwa sana kwenye ardhi. Watu wanaporwa ardhi mchana kweupe.
Haki inanunuliwa siku hizi, maana watoa haki,wamekuwa wauzaji wa haki za watu!!
 
Mheshimiwa Rais kama kuna Sekta ambayo kwa sasa inatajwa na Dhambi ya Kudhulumu Watanzania Wanyonge basi ni ya Ardhi.

Na kama kuna Mkoa ambao unaongoza kwa Watanzania Wanyonge Kudhulumiwa Ardhi yao ni Mkoa wa Dar es Salaam.

Na kama kuna Mkuu wa Mkoa ambaye anapewa Lawana ya Kutetea Wapora Ardhi ya Watanzania Wanyonge basi ni Amos Makalla wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Rais lifanyie Kazi hili ila Kilio ni Kikubwa kwa Watanzania Wanyonge Kuporwa na Kudhulumiwa Ardhi yao kwa Baraka zote za Wizara ya Ardhi.
Wamemuweka Prince na genge lake sijui kama tutasalimika
 
Mheshimiwa Rais kama kuna Sekta ambayo kwa sasa inatajwa na Dhambi ya Kudhulumu Watanzania Wanyonge basi ni ya Ardhi.

Na kama kuna Mkoa ambao unaongoza kwa Watanzania Wanyonge Kudhulumiwa Ardhi yao ni Mkoa wa Dar es Salaam.

Na kama kuna Mkuu wa Mkoa ambaye anapewa Lawana ya Kutetea Wapora Ardhi ya Watanzania Wanyonge basi ni Amos Makalla wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Rais lifanyie Kazi hili ila Kilio ni Kikubwa kwa Watanzania Wanyonge Kuporwa na Kudhulumiwa Ardhi yao kwa Baraka zote za Wizara ya Ardhi.
alipomtoa lukuvi tulitarajia haya kutokea
 
Kwenye lipi ameonyesha uchungu na uzalendo zaidi ya kulalamika na kulaumu tu?.
 
Kama aliwaambia mawaziri wake wale kwa urefu wa kamba yake atawezaje kuonesha uchungu kwa namna yoyote tena kwa wananchi.
 
Hayaaa yooootee shida ni yeye anaewateua na bado anakua kimya ht kwenye mambo yanayotesa wananchiii
Mpk 2030 hakuna rangi hatujaona
 
Hasa kigoma kuna huyu jamaa wanamuita Makolo ni hatari ni mwizi afu na kesi anashinda pale kigoma
 
Aisee kama kuna kipindi watu wamedhulumiwa ardhi yao ni kipindi hiki. Huku Kinondoni sehemu za mabwe, malolo, mji mpya, kinondo, mbopo na maeneo ya jirani kuna migogoro inatengenezwa na wakubwa kupitia diwani wa mabwepande na wenyeviti wa serikali za mitaa halafu wanatumia watu wao wanawadhulumu masikini viwanja vyao na wengine nyumba zao zinavunjwa. Kahamishwa mkuu wilaya Gondwe lakini bado hayo mambo yanaendelea.

Ila bado washirika wawili wakihamishwa hao mwenye mkoa wake na mkurugenzi wa manispaa ya kinondoni nadhani hii migogoro itapungua sana kama sio kuisha kabisa. Haiwezekani mtu eneo la kwake na analimiliki kihalali lakini kwa kuwa tu hana hati eti anapimiwa anauziwa tena kiwanja chake mwenyewe square meter 1 kwa TZS 6,500 wakati inajulikana gharama za serikali kupima kiwanja kimoja (na sio square meter) ni kati ya TZS 150,000 - 250,000 bei elekezi ya serikali iliyotangazwa na aliyekuwa waziri wa ardhi ndugu Lukuvi. Masikini gani atakuwa na hizo hela kama sio kunyanga'nywa kijanjajanja. Hizi pesa mamilioni kwa mabilioni zinaenda wapi na ni mradi wa nani? Na kama huna pesa za kulipa unanyanganywa kwa gia kuwa eneo hilo unaambiwa mali ya NSSF au DDC. Kama ni mali ya NSSF au DDC vipi anyanganywe masikini halafu auziwe mwenye pesa?

Na ni kwanini wanakataa wakaazi wa huko wasitumie kampuni binafsi kupima ardhi yao kuna ni nini nyuma ya pazia? Na waziri wa ardhi yupo wapi au mpaka raisi atembelee mwenyewe kuzungumza na na wanachi ndio atajifanya kushtuka. Mbunge Gwajima suala hili analijua na amepambana sana kuwapigania wananchi lakini inaonekana kuna genge kubwa linamzunguka na linataka kumzidi nguvu. Makubaliano yakifanyika kwenye mikutano ya hadhara na mbunge akiwepo akiondoka tu huku nyuma viongozi wenzake na wenyeviti wa mitaa wanakuja na maazimio tofauti kabisa.

Mwisho mhemshimiwa raisi tunaomba utume wasaidizi wako waje kwa siri maeneo hayo kwa kweli taarifa watakazokusanya hautoamini kujua kile ambacho watanzania wanapitia kwenye nchi yao tena hapa hapa mjini na wala sio mikoani huko.
 
Back
Top Bottom