Rais Samia: Polisi angalieni upya taratibu zenu za upelelezi, kuwaweka watu mahabusu muda mrefu ni gharama kwa Serikali

Rais Samia: Polisi angalieni upya taratibu zenu za upelelezi, kuwaweka watu mahabusu muda mrefu ni gharama kwa Serikali

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Rais Samia ameliagiza jeshi la polisi kuhakikisha linakamilisha upelelezi kwa haraka na kuwaachia huru watuhumiwa ambao kesi zao hazina mashiko.
Rais amesema hivi sasa idadi ya wafungwa inakaribiana kuwa sawa na idadi ya mahabusu.

Kadhalika Rais Samia amemtaka IGP Sirro kuhakikisha hawatumii mabavu bila tija na tabia ya mahabusu kufia rumande hayatoi picha nzuri kwa jeshi hilo.

Chanzo: TBC

=======

Rais Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Polisi kukaa na wadau wengine kuangalia uwezekano wa kurekebisha Sheria ya kuweka watu mahabusu, akisema kwenye Nchi nyingine mtu hakamatwi mpaka upelelezi utimie

Ameeleza Kesi nyingi zinakwama Mahakamani kutokana na kucheleweshwa kwa upelelezi au kukosekana ushahidi akisema, "Hizi tunaita kesi za kubambikiza"

Amesisitiza, "Kama kesi haina mwelekeo watu watolewe. Kwa kesi ambazo mna uhakika upelelezi utatimia basi uharakishwe"
 
Hamna jeshi kaka,ni kikundi cha wajinga na wahuni waliofeli shule.Embu angalia matangazo yao ya kazi, huwa wanahitaji watu wenye Div IV kwanzia point 26 na kuendelea sasa unategemea matokeo yake ni nn?
Reasoning yako ipo chini sana, kwa hiyo mtu kupata division 4 ina maana hana akili?
 
WE mama yetu mama wa ajabu. We concern yako ni gharama za serikali na si haki za watu? Very strange indeed. Mungu mbona unatuonea, tuonee huruma wewe.
Ni vyema kabla ya kuhukumu ungesikiliza hotuba yote, huyu John yeye kachomoa kakipande kadogo sana katika hili, Rais kaongea kirefu zaidi, nimemsikiliza mwanzo mwisho, ingia you tube ya tbc kuna hiyo hotuba yote, then utacomment ukiwa full informed
 
Unakuwa na Reasoning alafu unapata assessment IV or zero 🤣 🤣 ? Jeshi la polisi halihitaji mtu smart hata siku moja,na huu ndo ukweli mchungu.
Hujajibu swali, mtu kupata div 4 maana yake hana akili?
 
Kumbe nae anazijua kesi za kubambikiza, natumai Sirro amemsikia bosi wake, aache kutisha wapinzani na kukamata watu bila ushahidi, iwe mwisho.

Vinginevyo anachokiongea Samia hapo ni usanii mtupu, wengi kukamatwa kwa kesi za kubambika huwa ni kwa manufaa yao CCM analijua hilo.
 
Back
Top Bottom