Rais Samia: Serikali yenu ni sikivu, tutaangalia njia nzuri tunayoweza kufanya ili kikokotoo kisilete maneno mengi

Rais Samia: Serikali yenu ni sikivu, tutaangalia njia nzuri tunayoweza kufanya ili kikokotoo kisilete maneno mengi

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Akizungumzia kuhusu malalamiko yaliyopo kwenye kikokotoo katika ufunguzi wa Kikao kazi cha Maafisa waandamizi wa Jeshi la Polisi, Oysterbay, leo Septemba 4, 2023, Rais Samia amesema Serikali inafanyia kazi suala hilo na itaangalia njia nzuri ili kuondoa maneno mengi.

"Tupo tunakifanyia kazi na kuona jinsi tutakavyoenda vizuri kwa sababu masuala ya kikokotoo haya si tu matakwa ya Serikali kutaka kuja na kikokotoo, ni hali ya uchumi na hali ya mifuko yenu ilivyo. Ni hali ya mifuko ilivyo. Tukisema kila anayetoka boom lako hilo hapo, boom lako hilo hapo, miaka 2 tu mifuko ile imekauka." Amesema Rais Samia.

Ameongeza, "Tuliweka hivi ili kuweka sustainability ya mfuko, sasa kwa sababu imepigiwa kelele sana sio tu na jeshi la polisi lakini na wengine, tutakwenda kuangalia sababu tunasema siku zote Serikali yenu ni sikivu. Tutakwenda tuangalie njia nzuri tunayoweza kufanya ili kikokotoo kisilete maneno mengi"
 
Mifuko inakaushwa na sera mbovu na matumizi yasiyofaa ya pesa za wafanyakazi. Hizo pesa si wamekuwa wamezichanga wenyewe tena kwa kulazimishwa? Badala ya kipaumbele kiwe ni kumjali mwenye pesa zake cha kushangaza serikali inajilinda yenyewe. Kila siku tunaambizana tukajiajiri, kwa nini hizi hela watu wasizikope maadam ni zao? Kwa nini wasiruhusiwe kuzichukua walau baada ya miaka 2 wakawekeze na kuajiri wengine ili waacbe kazi na wengine waajiriwe?
 
Bado hajausema ule ukweli wenyewe wa serikali kuchukua hela za wafanyakazi na kwenda kuanzishia miradi ya hovyo na ya kifisadi, na hela nyingine kukopeshana wenyewe kwa wenyewe kinyume na utaratibu!!

Halafu baada ya kuifilisi sasa hiyo mifuko, ndiyo wakaja sasa na hicho kikokotoo chao cha kipuuzi! Na kuwalazimisha wafanyakazi wakikubali. All in all, muda ni rafiki mzuri.
 
Safi sana Rais Samia,kwanza nimeona pssf wanasema Serikali imelipa nusu ya deni ya pesa zake ambazo Mwendazake alichukua baada kuunganishwa na kuleta haya ma kikokotoo ya upigaji.

Pia msisahau na Fao la Kujitoa
 
Bado hajausema ule ukweli wenyewe wa serikali kuchukua hela za mifuko ya hifadhi ya jamii na kwenda kuanzishia miradi ya hovyo, na hela nyingine kugawana wenyewe kwa wenyewe!!

Halafu baada kuifilisi hiyo mifuko, ndiyo wakaja sasa na hicho kikokotoo chao cha kipuuzi! Na kuwalazimisha wafanyakazi wakikubali. All in all, muda ni rafiki mzuri.
Sema Mwendazake ndio alifabya huu upumbavu,ila juzi nimeona pssf wanasema Serikali imelipa nusu ya Madeni Yao hivyo Kwa Sasa ukistaafu sio kesi.

Yule katili ulikuwa ukistaafu unakaa miaka 3 au 2 unasubiria mafao
 
Asante mama SAMIA
Ni mapema mno kumshukuru huyu mama. Hachelewi kujikausha na kupotezea.

*Aliahidi nyongeza ya mishahara....tukapiga shangwe.
*Aliahidi maridhiano....tukapiga shangwe.
*Aliahidi 4Rs .....tukapiga shangwe.
*Aliahidi katiba mpya ....tukapiga shangwe.


Lkn yoote hayo amejikausha na kuyapotezea. Simuamini hata chembe huyu mama.

Naungana na wimbo wa Ney wamitego...."Mungu awapumzishe na hawa"
 
Akizungumzia kuhusu malalamiko yaliyopo kwenye kikokotoo katika ufunguzi wa Kikao kazi cha Maafisa waandamizi wa Jeshi la Polisi, Oysterbay, leo Septemba 4, 2023, Rais Samia amesema Serikali inafanyia kazi suala hilo na itaangalia njia nzuri ili kuondoa maneno mengi.

"Tupo tunakifanyia kazi na kuona jinsi tutakavyoenda vizuri kwa sababu masuala ya kikokotoo haya si tu matakwa ya Serikali kutaka kuja na kikokotoo, ni hali ya uchumi na hali ya mifuko yenu ilivyo. Ni hali ya mifuko ilivyo. Tukisema kila anayetoka boom lako hilo hapo, boom lako hilo hapo, miaka 2 tu mifuko ile imekauka." Amesema Rais Samia.

Ameongeza, "Tuliweka hivi ili kuweka sustainability ya mfuko, sasa kwa sababu imepigiwa kelele sana sio tu na jeshi la polisi lakini na wengine, tutakwenda kuangalia sababu tunasema siku zote Serikali yenu ni sikivu. Tutakwenda tuangalie njia nzuri tunayoweza kufanya ili kikokotoo kisilete maneno mengi"
Huyu mama sio wa kuamini...

Husema lakini hakuna vitendo...

MEI MOSI, 2023 aliahidi kuongeza mishahara ya watumishi wa umma, lakini hakufanya hivyo na badala yake baadhi (wachache tu) wakapata statutory annual salary increments huku ahadi kwa ajili ya watumishi wote ikibaki kuwa ni maneno tu ya jukwaani..!

After all, sasa Rais Samia Suluhu Hassan amethibitisha pasipo shaka leo kuwa kumbe kikokotoo hiki kilikuja kama mkakati wa serikali kuwakandamiza watumishi wa umma wa daraja la chini na kati kupunguza mafao yao kwa zaidi ya 67% kwa sababu serikali yenyewe ilifuja pesa za mafao toka ktk mifuko hii ya hifadhi ya jamii na zigo la adhabu wakaangushiwa watumishi wa umma wa daraja la chini na kati Kwa kukatwa mafao yao ya mkupuo!!

Nasema hili Kwa sababu wanasiasa wote ambao tunadhani wanaweza kutetea wananchi wao (kuanzia Rais mwenyewe, mawaziri, wabunge, wakuu wa Mikoa, wilaya, wakuu wa idara na taasisi na mashirika ya umma nk) kikokotoo hiki hakiwahusu lakini watu hawahawa eti ndo wasimamie na watetee maslahi ya watumishi wa umma..

Kwa hiyo hata hili sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kumuamini huyu mama...
 
Bado hajausema ule ukweli wenyewe wa serikali kuchukua hela za wafanyakazi na kwenda kuanzishia miradi ya hovyo na ya kifisadi, na hela nyingine kukopeshana wenyewe kwa wenyewe kinyume na utaratibu!!

Halafu baada ya kuifilisi sasa hiyo mifuko, ndiyo wakaja sasa na hicho kikokotoo chao cha kipuuzi! Na kuwalazimisha wafanyakazi wakikubali. All in all, muda ni rafiki mzuri.
Hili ni tatizo kubwa sana.

Inasikitisha kuona wazi kabisa serikali inatunia vibaya fedha za hii mifuko na mtu makini anaweza kuona kabisa matatizo yatakayokuja.

Nchi kama Marekani pesa za Social Security zinawekwa kwenye US Treasury securities, the safest investment. Kipaumbele ni kuziweka fedha ziwe salama, si kuziweka katika vitegauchumi vyenye risk kubwa.

Kwenye mifuko ya binafsi, mtu unapewa access ya website unaamua mwenyewe pesa zako za mafao ya uzeeni unaziweka wapi, hakuna mtu anayekulazimisha.

Tanzania pia tunaweza kuweka mfumo huu, viongozi wanapenda kutumia hizi hela vibaya tu.
 
Bado hajausema ule ukweli wenyewe wa serikali kuchukua hela za wafanyakazi na kwenda kuanzishia miradi ya hovyo na ya kifisadi, na hela nyingine kukopeshana wenyewe kwa wenyewe kinyume na utaratibu!!

Halafu baada ya kuifilisi sasa hiyo mifuko, ndiyo wakaja sasa na hicho kikokotoo chao cha kipuuzi! Na kuwalazimisha wafanyakazi wakikubali. All in all, muda ni rafiki mzuri.


Serikali hapa hana tofauti na mbwa alieona mfupa mnono halafu upo loose.

Kwenye hili msaliti mkubwa ni chama cha wafanyakazi na baadhi ya wafanyakazi (wengi wao).

Sisi wamachinga ambao ni beneficiaries wenu huku mtaani zaidi ya kuumizwa na kukerwa na mikopo yenu, tunawaombea mufanikiwe.
 
Ni mapema mno kumshukuru huyu mama. Hachelewi kujikausha na kupotezea.

*Aliahidi nyongeza ya mishahara....tukapiga shangwe.
*Aliahidi maridhiano....tukapiga shangwe.
*Aliahidi 4Rs .....tukapiga shangwe.
*Aliahidi katiba mpya ....tukapiga shangwe.


Lkn yoote hayo amejikausha na kuyapotezea. Simuamini hata chembe huyu mama.

Naungana na wimbo wa Ney wamitego...."Mungu awapumzishe na hawa"



Vyote ulivyoweka hako Rais Samia katimiza kwa asilimia 99.99.

*Nyongeza ya mshahara katimiza [emoji817] % - hata elfu 2500 ni nyongeza.


* Maridhiano katimiza [emoji817] % - Mzee Mbowe ni miongoni kwa wajumbe hai wa kamati ya maridhiano mpaka sasa, hakuna tamko lolote la kujitoa.


* 4Rs anatimiza kwa [emoji817] % - Mfumo wa R ya Recycling hujauona kwenye teuzi? Mfumo wa R ya Rebuild hujauona katika ahadi ya TPA na ujenzi mbali mbali wa miundo mbinu ya kimaendeleo na kimkakati huko Zanzibar?


*Katiba mpya amekubali kwa [emoji817] % - wamesema wanaanza na kufundisha Katiba iliyopo sasa nchi nzima kijiji kwa kijiji kwa miaka 3 halafu ndio mchakato wa Katiba mpya uanze.


Yuko vizuri.
 
Back
Top Bottom