Kumbe Rais Samia alikuwa na mkutano na kundi fulani la watu! Sikufuatilia aliongea nini, kwa sababu huwa napata taabu sana kufuatilia mikutano ya Wanasiasa iwe wa chama tawala au upinzani.
Hata hivyo, kupitia mijadala mbalimbali nikagundua nikakutana na hoja za SSH "hataki" mikutano ya vyama vya siasa!! Mada hizi zikanilazimisha kutafuta video clip ili nisikie kwa masikio yangu alichosema SSH.
Baada ya kumsikiliza, mosi SSH anakiri hadharani kwamba uchumi umeporomoka, na mambo yanayohusiana na uchumi yapo shakala baghala! Kutokana na hilo, SSH ameweka wazi kwamba, priority yake ni kuweka sawa masuala ya uchumi na uwekezaji, na hayo mengine yatafuata baadae.
SSH hakutumia hard voice kupiga marufuku mikutano ya kisiasa bali ameomba sana, tena sana kwa sasa apewe muda ili aweke mambo sawa kwenye masuala ya kiuchumi na uwekezaji.
Nikiwa kama mdau wa masuala ya kiuchumi na uwekezaji, lazima nimpongeze SSH kwa kuona umuhimu wa kuweka mambo sawa kwenye eneo hilo.
HOWEVER, popote pale ulipo, Mheshimiwa SSH unatakiwa kufahamu ama kukumbuka kwamba suala la mikutano ya hadhara ya kisiasa ni suala la kisheria, na HAKUNA aliye juu ya sheria... HAKUNA.
Suala la kufanya mikutano ya kisiasa halitakiwi kuwa ni favor inayoweza kutolewa na Rais wa nchi, na asipotaka, anaitupia kabatini favor hiyo.
Kama unaomba uwekeze nguvu kwenye mambo uliyotaja na kutoa likizo kwa suala la mikutano ya kisiasa basi ombi hilo hukutakiwa kulitoa kwenye mkutano na Waandishi wa Habari bali ulitakiwa kukutana na vyama vya siasa kwanza, na kutoa ombi hilo kwao, na kuwashawishi ni kwanini unaona kwa sasa tusogeze mbele siasa za majukwaani zisizo na mipaka ya kimajimbo.
Ulichofanya kwenye mkutano wako na Waandishi wa Habari sio ombi hata kama umesisitiza mara kadhaa kwamba "unaomba"! Ulichofanya hapo ni kutoa conclusion ya mikutano kutofanyika.
Hilo halikubaliki kwa sababu kufanya hivyo inakuwa ni uvunjaji wa sheria za nchi moja kwa moja, tena mbele ya kadamnasi.
Kama hufahamu, au umesahau, nakukumbusha tu kwamba, Sheria ya Vyama vya Siasa kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019, Kifungu cha 11 (1) (a) kinasema:-
Utaona hapo sheria inatoa uhuru kwa vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara popote pale ndani ya Jamhuri ili mradi tu wawe wametoa taarifa polisi, na sio kama ulivyosema wewe kwamba "...wanaweza kufanya mikutano ya hadhara" exclusively kwenye majimbo yao TU.
Hiyo ni haki ya kisheria ambayo inatambulika hadi kwenye mabadiliko ya sheria yaliyofanyika wewe ukiwa Makamu wa Rais.
Mheshimiwa SSH popote pale ulipo, hiyo ndiyo Sheria ya Vyama vya Siasa iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2019. Na hapa ningependa kurudia kwamba, kama unadhani unataka watu waelekeze nguvu kwenye masuala ya kiuchumi, na kupeleka likizo mikutano ya kisiasa basi unatakiwa kushauriana na vyama vya kisiasa.
Mkifanya majadiliano bila shaka mtafikia muafaka, ama wa kupeleka likizo mikutano ya hadhara isiyo na mipaka, au wanaweza kuamua kuweka idadi maalumu ya mikutano ya hadhara kwa muda fulani, na kama wataamua kuendelea na mikutano kama inavyoelekezwa na sheria, basi pia hiyo ni haki yao ya kisheria.
Aidha, kama wananchi wenyewe watataka kuwekeza nguvu zao kwenye masuala ya uchumi badala ya siasa, ni wao ndio watakaoamua kupuuzia mikutano hiyo.
Hata hivyo, kupitia mijadala mbalimbali nikagundua nikakutana na hoja za SSH "hataki" mikutano ya vyama vya siasa!! Mada hizi zikanilazimisha kutafuta video clip ili nisikie kwa masikio yangu alichosema SSH.
Baada ya kumsikiliza, mosi SSH anakiri hadharani kwamba uchumi umeporomoka, na mambo yanayohusiana na uchumi yapo shakala baghala! Kutokana na hilo, SSH ameweka wazi kwamba, priority yake ni kuweka sawa masuala ya uchumi na uwekezaji, na hayo mengine yatafuata baadae.
SSH hakutumia hard voice kupiga marufuku mikutano ya kisiasa bali ameomba sana, tena sana kwa sasa apewe muda ili aweke mambo sawa kwenye masuala ya kiuchumi na uwekezaji.
Nikiwa kama mdau wa masuala ya kiuchumi na uwekezaji, lazima nimpongeze SSH kwa kuona umuhimu wa kuweka mambo sawa kwenye eneo hilo.
HOWEVER, popote pale ulipo, Mheshimiwa SSH unatakiwa kufahamu ama kukumbuka kwamba suala la mikutano ya hadhara ya kisiasa ni suala la kisheria, na HAKUNA aliye juu ya sheria... HAKUNA.
Suala la kufanya mikutano ya kisiasa halitakiwi kuwa ni favor inayoweza kutolewa na Rais wa nchi, na asipotaka, anaitupia kabatini favor hiyo.
Kama unaomba uwekeze nguvu kwenye mambo uliyotaja na kutoa likizo kwa suala la mikutano ya kisiasa basi ombi hilo hukutakiwa kulitoa kwenye mkutano na Waandishi wa Habari bali ulitakiwa kukutana na vyama vya siasa kwanza, na kutoa ombi hilo kwao, na kuwashawishi ni kwanini unaona kwa sasa tusogeze mbele siasa za majukwaani zisizo na mipaka ya kimajimbo.
Ulichofanya kwenye mkutano wako na Waandishi wa Habari sio ombi hata kama umesisitiza mara kadhaa kwamba "unaomba"! Ulichofanya hapo ni kutoa conclusion ya mikutano kutofanyika.
Hilo halikubaliki kwa sababu kufanya hivyo inakuwa ni uvunjaji wa sheria za nchi moja kwa moja, tena mbele ya kadamnasi.
Kama hufahamu, au umesahau, nakukumbusha tu kwamba, Sheria ya Vyama vya Siasa kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019, Kifungu cha 11 (1) (a) kinasema:-
Every political party provisionally or fully registered shall be entitled to hold and address public meetings in any area in the United Republic after giving notification to the police officer in charge of the area concerned for purposes of publicising itself and soliciting for membership.
Utaona hapo sheria inatoa uhuru kwa vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara popote pale ndani ya Jamhuri ili mradi tu wawe wametoa taarifa polisi, na sio kama ulivyosema wewe kwamba "...wanaweza kufanya mikutano ya hadhara" exclusively kwenye majimbo yao TU.
Hiyo ni haki ya kisheria ambayo inatambulika hadi kwenye mabadiliko ya sheria yaliyofanyika wewe ukiwa Makamu wa Rais.
Mheshimiwa SSH popote pale ulipo, hiyo ndiyo Sheria ya Vyama vya Siasa iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2019. Na hapa ningependa kurudia kwamba, kama unadhani unataka watu waelekeze nguvu kwenye masuala ya kiuchumi, na kupeleka likizo mikutano ya kisiasa basi unatakiwa kushauriana na vyama vya kisiasa.
Mkifanya majadiliano bila shaka mtafikia muafaka, ama wa kupeleka likizo mikutano ya hadhara isiyo na mipaka, au wanaweza kuamua kuweka idadi maalumu ya mikutano ya hadhara kwa muda fulani, na kama wataamua kuendelea na mikutano kama inavyoelekezwa na sheria, basi pia hiyo ni haki yao ya kisheria.
Aidha, kama wananchi wenyewe watataka kuwekeza nguvu zao kwenye masuala ya uchumi badala ya siasa, ni wao ndio watakaoamua kupuuzia mikutano hiyo.