Che mittoga
JF-Expert Member
- Mar 28, 2017
- 12,658
- 16,205
Hakuna pahala amevunja katiba......Mkuu waliotengeneza katiba walikuwa na maana kubwa....muda unavyokwenda tutajua.Rais Samia kwa Lile alilolifanya Jana kaivunja katiba aliyoapa kuilinda.Nikipata muda hapa nitaweka vifungu.Lazima spade iitwe hivo.
Unaruka ruka tu tuliza ball gem bado mbichiAnapambana na Coronavirus ??
Kafungua wafungwa wa kisiasa ?
Twitter iko hewani ??
Wamekufa watu 45 taifa katia hata pole ??
Azory Gwanda, Ben Saanane, Lissu, Kanguye, viroba: Ukweli ukoje ???
Kuna Jipya gani ???
Usiwe na matumaini sana utakuja very disappointed.
Huyo mama hana Jipya wala vision yoyote.
Katage kwanzaUnaruka ruka tu tuliza ball gem bado mbichi
Jitenge vizuri nikutagieKatage kwanza
Na wewe ni mmoja wa wanaosoma katiba kwa kupinda pinda na kuruka ruka; hujui tofauti baina ya na rais anayechukua madaraka kutokana na uchguzi na rais anayechukua madaraka kwa kurithishwa kutokana na vifungu vingine vya katiba. Vifungu unavyolazimisha vifuatwe ni vile vinavyohusu Rais Mteule- anayepatikana baada ya uchaguzi kabla ya kupishwa, wakati mama Samia hajapawahi kuwa Rais Mteule bali alikuwa Makamu wa Rais mpaka pale alipoapishwa kushika madaraka ya uraisi.
Kwani mbona JPM alitumia wale wale wa JK na bado aliwanyoosha. JK naye alitumia wa Mkapa, na chain inaendelea hadi kwa Nyerere.Kwa kutumia walewale wa Jpm atawanyoshaje?
MadarakaHivi Kigogo2014 ni nani? Nabii? Mtabiri wa Taifa? Whistle blower? Mshauri? Mkosoaji? Au mtukanaji? Natamani kujua hasa nini kusudi, dhamira ya taasisi hiyo kwa Taifa letu.
Utawala wa Magufuli na Nyerere ndio utakuwa standards ya viongozi wajao, pengine na Samia
hata kiongozi mbaya zaidi kuwahi kutokea duniani alikuwa na mazuri yake....huwezi kusema mtu hana jipya wala vision yeyote na tayari ni binadamu mwenye akili timamu.....dharau na ku underrate wengine sio tabia njema ukizingatia hata siku 30 kwenye madaraka bado hajafikisha...be humble mkuu..Anapambana na Coronavirus ??
Kafungua wafungwa wa kisiasa ?
Twitter iko hewani ??
Wamekufa watu 45 taifa katia hata pole ??
Azory Gwanda, Ben Saanane, Lissu, Kanguye, viroba: Ukweli ukoje ???
Kuna Jipya gani ???
Usiwe na matumaini sana utakuja very disappointed.
Huyo mama hana Jipya wala vision yoyote.
Anazo karama zote hizo.Hivi Kigogo2014 ni nani? Nabii? Mtabiri wa Taifa? Whistle blower? Mshauri? Mkosoaji? Au mtukanaji? Natamani kujua hasa nini kusudi, dhamira ya taasisi hiyo kwa Taifa letu.
44. Kupora mademu na wake za watuMambo makubwa aliyofanya Magufuli:
1.Kuondoka duniani wakati hahitajiki.
2.Kuteka wapinzani wake kama akina Azory Gwanda.
3.Kutesa wapinzani wake kwa kuwaweka ndani kila siku.
4.Kuua wapinzani wake na wakosoaji wake kama akina Ben saanane na kuwapiga wapinzani wake risasi kama ilivyokuwa kwa Tindu Lissu.
5.Kuua uhuru wa vyombo vya habari.
6.Kuua uhuru wa kujieleza kwa wananchi kama vile kufungia mitandao ya kijamii kama twitter na kukamata wanaotumia mitandao mingine kumkosoa.
7.Kuiba kura kwa kutumia Polisi,jeshi,TISS pamoja na tume ya uchaguzi.
8.Kuua biashara za watu kupitia sera mbovu za uchumi.
9.Kudanganya katika takwimu za ukuaji wa uchumi wa nchi.
10.Kuweka mihimili yote mitatu mfukoni mwake,yaani mhimili wa urais,bunge na mahakama.
11.Kuua uchumi wa nchi kupitia sheria mbovu za uwekezaji.
12.Kuua watu kwa Corona kupitia leadership negligence.
13.Kuhakikisha kuwa akina Ben Saanane na Azory Gwanda walikipata cha mtema kuni.
14.Ukabila kwa kuhamishia rasilimali nyingi za nchi katika wilaya ya Chato na kujaza wasukuma serikalini.
15 Ukanda kwa kupeleka SGR mwanza wakati siyo economic viable zone.
16.Ubaguzi wa rangi kwa kuwakandia wanawake weusi.Imagine mtu anafanya ubaguzi wa rangi karne ya 21!Is this not insane?
17.Kugandamiza demokrasia kwa kukataza vyama vya upinzani kufanya siasa wakati CCM kufanya siasa ni ruksa.
18.Kunyanyasa malaika-watoto wa kike wasirudi shule wakipata mimba.
19.Ufisadi wa kutisha kwa kufanya miradi mikubwa bila budget kupita bungeni.
20.Wizi wa kutisha wa mali ya uma kupitia kampuni yake ya Mayanga constructions LTD.Mfano uwanja wa Chato umetengenezwa na kampuni hii bila tenda kuitwa.
21.Kubambikizia kesi za kuhujumu uchumi wapinzani wake nchi nzima na kuwatupa korokoroni.
22.Kugushi report ya CAG ya hasara za mabilion za ndege za TTCL na kuilazimisha TTCL watoe gawio fake kwa serekali.
23.Kupora utajiri halali na wa jasho wa matajiri wa Tanzania kwa kuwabambikizia kesi fake za kuhujumu uchumi na kuwalazimisha wakiri makosa ya uwongo kisha kuwafilisi mali zao.
Tumpe muda mkuu! Mama akitengeneza maadui au hata makundi kwenye serikali yake atakwama! Kupima loyality ni muhimu sana kwake, Lakini pia kuweka watu wengi wapya anaweza kupoteza vingi. Kuhusu hayo makando kando ya serikali ya mwendazake, hata ungekua Wewe, huwezi kuingia tu kichwa kichwa! Mama amajipanga, na tunatakiwa kuanza kumhukumu kuanzia siku 100 za kukaa kitini!Anapambana na Coronavirus ??
Kafungua wafungwa wa kisiasa ?
Twitter iko hewani ??
Wamekufa watu 45 taifa katia hata pole ??
Azory Gwanda, Ben Saanane, Lissu, Kanguye, viroba: Ukweli ukoje ???
Kuna Jipya gani ???
Usiwe na matumaini sana utakuja very disappointed.
Huyo mama hana Jipya wala vision yoyote.
Ile team, Sisi sote hatuipendi, lakini mama anaitaji kuikita mizizi yake, kwanza kwenye kiti cha urais na pia kwenye chama chake! Tumpe muda, baada ya siku is 100 tumpe kongole au tumponde! La kutoapisha upya baraza, nakubaliana na wewe kwamba ni kitu kidogo, why hakufanya!! Lakini upande huo huo, nachukulia kwamba ni kitu kidogo, hakiwezi kumkwamisha!Ana lengo zuri, tatizo timu inayomzunguka ni chafu hasa AG, badala ya kumshauri kuunda Baraza kwa mujibu wa katiba kamshauri vibaya.Kwangu binafsi kiongozi anayevunja kiapo chake Sina Cha kumsaidia.Hivi inachukua gharama gani mama angemteua pm na kuunda Baraza? Kwangu naona Kama hujuma vile anatengenezewa na wabaya wake ndani ya serikali au chamani.Target ni mchuano wa 2025
Mama kafanya yake, lakini jamaa ana hoja pia kwamba wale mawaziri ni lazima waape kufanya kazi kwenye serikali ya mama! Kuijibu hoja yake, naona mama kaamua kuwapa fursa ya kuonesha kiapo chao kwake kwa vitendo, wakijifanya kujua, atawa-Bashiru taratiiiiibu, mmoja baada ya mwingine!Na wewe ni mmoja wa wanaosoma katiba kwa kupinda pinda na kuruka ruka; hujui tofauti baina ya na rais anayechukua madaraka kutokana na uchguzi na rais anayechukua madaraka kwa kurithishwa kutokana na vifungu vingine vya katiba. Vifungu unavyolazimisha vifuatwe ni vile vinavyohusu Rais Mteule- anayepatikana baada ya uchaguzi kabla ya kupishwa, wakati mama Samia hajapawahi kuwa Rais Mteule bali alikuwa Makamu wa Rais mpaka pale alipoapishwa kushika madaraka ya uraisi.
Hiyo ni extreme! Tusifike kote huko, kuifanya nchi hii kuwa ya dini fulani ni ngumu sana! Kwa taarifa yako, kwa utafiti wangu, Ukristo kwenye nchi hii umekua na tabia ya kuimarika zaidi tunapokua na rais muislamu! Mimi ni vere Mkristo, najua sababu na Nina vifungu vya Maandiko matakatifu ya Biblia, kulidhibitisha hilo!Kazuia sherehe za Pasaka pia ni Mwanzo Mzuri kuigeuza nchi kuwa ya Sheria za Kiislam
Mimi ni Mzalendo, kwa maana halisi ya uzalendo, sitegemei upepo! Kwa miaka 6 nimetaabika pamoja na nchi yangu, lakini kila siku natazamia pambazuko! Kwa hiyo namwombea SSH, hata mwendazake nilimwombeaga pia!Upepo ukivuma kwako vizuri utawala wowote unakuwa poa tu, ila ukipigwa kumbo hata presidenti wangu wa moyo Jeikei kuna watu wanamchukia
Uzalendo upi unaomaanisha mkuu? Njaa haina uzalendo......na kuishi maisha magumu yenye changamoto haimaanishi ndiyo uzalendoMimi ni Mzalendo, kwa maana halisi ya uzalendo, sitegemei upepo! Kwa miaka 6 nimetaabika pamoja na nchi yangu, lakini kila siku natazamia pambazuko! Kwa hiyo namwombea SSH, hata mwendazake nilimbeaga pia!